< 2 Wakorintho 4 >

1 Kwa hiyo, kwa sababu tuna huduma hii, na kama ambavyo tumeipokea rehema, hatukati tamaa.
C'est pourquoi, étant revêtus de ce ministère par la miséricorde qui nous a été faite, nous ne nous laissons point décourager.
2 Badala yake, tumekataa njia zote za aibu na zilizofichika. Hatuishi kwa hila, na hatulitumii vibaya neno la Mungu. Kwa kuwasilisha iliyo kweli, tunajionyesha wenyewe kwa dhamiri ya kila mtu mbele ya Mungu.
Nous rejetons loin de nous les manoeuvres secrètes et honteuses, n'agissant point avec fourberie, n'altérant point non plus la parole de Dieu. Nous nous rendons recommandables à toute conscience d'homme, devant Dieu, par la franche révélation de la vérité.
3 Lakini kama injili yetu imefichika, imefichika kwa wale tu wanaoangamia.
Si, malgré cela, notre évangile est encore voilé, il n'est voilé qu'à ceux qui se perdent,
4 Katika uchaguzi wao, mungu wa ulimwengu huu amewapofusha fahamu zao zisizoamini. Matokeo yake, hawawezi kuona nuru ya injili ya utukufu wa Kristo, ambaye ni mfano wa Mungu. (aiōn g165)
à ces incrédules dont le Dieu de ce siècle a aveuglé l'esprit, afin qu'ils ne soient point illuminés des splendeurs de l'évangile, on brille la gloire de Christ, qui est l'image de Dieu. (aiōn g165)
5 Kwa kuwa hatujitangazi wenyewe, bali Kristo Yesu kama Bwana, na sisi wenyewe kama watumishi wenu kwa ajili ya Yesu.
Ce n'est pas nous, c'est Jésus-Christ que nous prêchons comme Seigneur; quant à nous, nous donnons nous-mêmes pour vos serviteurs, à cause de Jésus,
6 Kwa kuwa Mungu ndiye ambaye aliyesema, “Mwanga utaangaza toka gizani.” Ameangaza katika mioyo yetu, kutoa mwanga wa maarifa ya utukufu wa Mungu katika uwepo wa Yesu Kristo.
parce que le Dieu qui a dit, «que la lumière jaillisse des ténèbres, » a fait luire sa lumière dans nos coeurs, pour que nous fassions briller la connaissance de sa gloire, laquelle resplendit en la personne de Christ.
7 Lakini tuna hazina hii katika vyombo vya udongo, ili kwamba ieleweke kuwa nguvu kuu sana ni ya Mungu na sio yetu.
Nous portons ce trésor dans des vases de terre, afin que la force extraordinaire qui est en nous, paraisse, non venir de nous, mais appartenir à Dieu:
8 Tunataabika katika kila hali, lakini hatusongwi. Twaona shaka lakini hatujawi na kukata tamaa.
nous sommes pressés de toute manière, mais non pas réduits à la dernière extrémité; nous sommes perplexes, mais non pas désespérés;
9 Tunateswa lakini hatujatelekezwa. Twatupwa chini lakini hatuangamizwi.
nous sommes persécutés, mais non pas abandonnés; abattus, mais non perdus.
10 Siku zote tunabeba katika mwili wetu kifo cha Yesu, ili kwamba uzima wa Yesu uonekane pia katika miili yetu.
Nous portons toujours dans notre corps la mort de Jésus, afin que la vie de Jésus se montre aussi dans notre corps;
11 Sisi tulio hai siku zote tumetolewa kufa kwa ajili ya Yesu, ili kwamba uhai wa Yesu uonekane katika miili yetu ya kibinadamu.
car nous qui vivons, nous sommes toujours livrés à la mort à cause de Jésus, afin que la vie de Jésus se manifeste aussi dans notre chair mortelle;
12 Kwa sababu hii, kifo kinafanya kazi ndani yetu, bali uzima unafanya kazi ndani yenu.
de sorte que la mort agit en nous, tandis que la vie agit en vous.
13 Lakini tuna roho ileile ya imani kulingana na kile kilicho andikwa: “Niliamini, na hivyo nilinena.” Sisi pia tunaamini, na hivyo pia tunanena.
Or comme nous avons l'esprit de foi qui a dicté cette parole, «j'ai cru, c'est pourquoi j’ai parlé, » nous aussi, «nous croyons, c'est pourquoi nous parlons, »
14 Tunajua kuwa yule aliye mfufua Bwana Yesu pia atatufufua sisi pamoja naye. Tunajua kuwa atatuleta sisi pamoja nanyi katika uwepo wake.
étant persuadés que Celui qui a ressuscité le Seigneur Jésus, nous ressuscitera aussi avec lui, et nous fera paraître avec vous en sa présence;
15 Kila kitu ni kwa ajili yenu ili kwamba, kwa kadri neema inavyo enea kwa watu wengi, shukurani zizidi kuongezeka kwa utukufu wa Mungu.
car tout cela est pour vous, afin que la grâce, en s'étendant à un plus grand nombre, provoque de plus nombreuses actions de grâces à la gloire de Dieu.
16 Hivyo hatukati tamaa. Japokuwa kwa nje tunachakaa, kwa ndani tunafanywa upya siku hadi siku.
C'est pourquoi, nous ne nous laissons point décourager; au contraire, alors même que notre homme extérieur se détruit, notre homme intérieur se renouvelle de jour en jour.
17 Kwa kipindi hiki kifupi, mateso haya mepesi yanatuandaa sisi kwa ajili ya umilele mzito wa utukufu uzidio vipimo vyote. (aiōnios g166)
Nos légères et passagères afflictions nous procurent une gloire infinie et éternelle, (aiōnios g166)
18 Kwa kuwa hatutazami kwa ajili ya vitu ambavyo vinaonekana, bali kwa ajili ya vitu visivyoonekana. Vitu tunavyoweza kuviona ni vya muda tu, bali vitu ambayo havionekani ni vya milele. (aiōnios g166)
attendu que nous regardons non aux choses visibles, mais aux choses invisibles; car les choses visibles ne sont que pour un temps, au lieu que les invisibles sont éternelles. (aiōnios g166)

< 2 Wakorintho 4 >