< 2 Wakorintho 2 >

1 Kwa hiyo niliamua kwa sehemu yangu mwenyewe kwamba nisingekuja tena kwenu katika hali ya uchungu.
That's why I decided that I would avoid another sad visit with you.
2 Kama niliwasababishia ninyi maumivu, ni nani angenifurahisha mimi, lakini ni yule ambaye aliumizwa na mimi?
For if I make you sad, who will be there to make me happy? It won't be those I've made sad!
3 Niliandika kama nilivyofanya ili kwamba wakati nikija kwenu nisiweze kuumizwa na wale ambao wangekuwa wamenifanya nifurahi. Ninao ujasiri kuhusu ninyi nyote kwamba furaha yangu ni furaha ile ile mliyonayo ninyi nyote.
That's why I wrote what I did, so that I wouldn't be sad over those who should make me happy. I was so sure that all of you would share in my happiness.
4 Kwa kuwa niliwaandikia ninyi kutokana na mateso makubwa, na dhiki ya moyo, na kwa machozi mengi. Sikutaka kuwasababishia ninyi maumivu. Badala yake, nilitaka mjue upendo wa kina nilionao kwa ajili yenu.
I was crying many tears when I wrote to you, in great anguish and with a heavy heart—not to make you sad, but so you would know how much love I have for you.
5 Kama kuna yeyote amesababisha maumivu, hajasababisha tu kwangu, lakini kwa kiwango fulani - bila kuweka ukali zaidi - kwenu ninyi nyote.
Not to put it too strongly, but the person caused more pain to all of you than to me.
6 Hii adhabu ya mtu huyo kwa wengi inatosha.
This person suffered enough punishment from the majority of you,
7 Kwa hiyo sasa badala ya adhabu, mnapaswa kumsamehe na kumfariji. Fanyeni hivi ili kwamba asiweze kushindwa na huzuni iliyozidi.
so now you should forgive him and be kind to him. Otherwise he may sink into despair.
8 Kwa hiyo ninawatia moyo kuthibitisha upendo wenu hadharani kwa ajili yake.
So I urge you to publicly affirm your love towards him.
9 Hii ndiyo sababu niliandika, ili kwamba niweze kuwajaribu na kujua kuwa kama ni watii katika kila kitu.
That's why I wrote: so I could discoverer your true character and whether you're doing everything you were told to do.
10 Kama mkimsamehe yeyote, na mimi pia namsamehe mtu huyo. Kile nilicho kisamehe - kama nimesamehe chochote-kimesamehewa kwa faida yenu katika uwepo wa Kristo.
Anyone you forgive, I forgive too. What I have forgiven, whatever it may be, I have forgiven before Christ for your benefit.
11 Hii ni kwamba Shetani asije akatufanyia madanganyo. Kwa kuwa sisi sio wajinga kwa mipango yake.
In this way Satan will not be able to take us in, because we know the tricks he thinks up.
12 Mlango ulifunguliwa kwangu na Bwana nilipokuja kwenye mji wa Troa kuhubiri injili ya Kristo pale.
Now when I arrived in Troas to spread the good news of Christ, the Lord opened a door of opportunity for me.
13 Hata hivyo, sikuwa na amani ya moyo, kwa sababu sikumkuta ndugu yangu Tito pale. Hivyo niliwaacha na nikarudi Makedonia.
But my mind wasn't at peace because I couldn't find my brother Titus. So I said goodbye and went over to Macedonia.
14 Lakini ashukuriwe Mungu, ambaye katika Kristo mara zote hutuongoza sisi katika ushindi. Kupitia sisi husambaza harufu nzuri ya maarifa yake mahala pote.
But praise be to God, who always leads us in a triumphal procession in Christ, and reveals through us the sweet scent of his knowledge wherever we go!
15 Kwa kuwa sisi kwa Mungu, ni harufu nzuri ya Kristo, wote kati ya wale waliookolewa na kati ya wale wanaoangamia.
We are like a fragrance of Christ to God, rising up from among those who are being saved as well as those who are dying.
16 Kwa watu ambao wanaangamia, ni harufu kutoka kifo hadi kifo. Kwa wale wanaookolewa, ni harufu nzuri kutoka uzima hadi uzima. Ni nani anayestahili vitu hivi?
To those who are dying it is the smell of decay, while to those who are being saved it is the scent of life! But who is up to such an assignment?
17 Kwa kuwa sisi sio kama watu wengi wanaouza neno la Mungu kwa faida. Badala yake, kwa usafi wa nia, tunanena katika Kristo, kama vile tunavyotumwa kutoka kwa Mungu, mbele ya Mungu.
We are not like the majority who trade in the word of God for profit. Quite the opposite: we are sincere in sharing the word of God in Christ, knowing God is watching us.

< 2 Wakorintho 2 >