< 2 Wakorintho 13 >
1 Hii ni mara ya tatu kwamba nakuja kwenu. “Kila shitaka lazima lijengwe na uthibitisho wa mashahidi wawili au watatu.”
This intended visit of mine is my third visit to you. "On the evidence of two or three witnesses every charge shall be sustained."
2 Nimekwishashasema kwa hao waliotenda dhambi kabla na kwa wengine wote wakati nilipokuwa huko mara ya pili, na ninasema tena: Nitakapokuja tena, sitawavumilia.
Those who cling to their old sins, and indeed all of you, I have forewarned and still forewarn (as I did on my second visit when present, so I do now, though absent) that, when I come again, I shall not spare you;
3 Nawaambia ninyi hili kwa sababu mnatafuta ushahidi kwamba Kristo ananena kupitia mimi. Yeye sio dhaifu kwenu, badala yake, yeye ni mwenye nguvu ndani yenu.
since you want a practical proof of the fact that Christ speaks by my lips--He who is not feeble towards you, but powerful among you.
4 Kwa kuwa alisulibiwa katika udhaifu, lakini yu hai kwa nguvu za Mungu. Kwa kuwa sisi pia tu dhaifu ndani yake, lakini tutaishi naye kwa nguvu za Mungu miongoni mwenu.
For though it is true that He was crucified through weakness, yet He now lives through the power of God. We also are weak, sharing His weakness, but with Him we shall be full of life to deal with you through the power of God.
5 Jichunguzeni wenyewe muone kama mko katika imani. Jipimeni wenyewe. Hamgundui kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu? Yeye yumo, vinginevyo kama hamjathibitishwa.
Test yourselves to discover whether you are true believers: put your own selves under examination. Or do you not know that Jesus Christ is within you, unless you are insincere?
6 Na nina ujasiri kwamba ninyi mtagundua kwamba sisi hatukukataliwa.
But I trust that you will recognize that we are not insincere.
7 Sasa tunaomba kwa Mungu kwamba msiweze kufanya chochote kibaya. Siombi kwamba sisi tuweze kuonekana tumepita jaribu, badala yake ninaomba kwamba muweze kufanya kilicho sahihi, Ingawa tunaweza kuonekana tumeshindwa jaribu.
And our prayer to God is that you may do nothing wrong; not in order that our sincerity may be demonstrated, but that you may do what is right, even though our sincerity may seem to be doubtful.
8 Kwa kuwa sisi hatuwezi kufanya lolote kinyume na kweli, lakini ni kwa ajili ya kweli tu.
For we have no power against the truth, but only for the furtherance of the truth;
9 Kwa kuwa tunafurahi wakati tunapokuwa dhaifu nanyi mkiwa na nguvu. Tunaomba pia kwamba muweze kufanywa wakamilifu.
and it is a joy to us when we are powerless, but you are strong. This we also pray for--the perfecting of your characters.
10 Nayaandika mambo haya wakati nikiwa mbali nanyi, ili kwamba wakati nikiwa pamoja nanyi sihitaji kuwaonesha ukali ninyi. Sihitaji kutumia mamlaka Bwana aliyonipaa mimi niwajenge na siyo kuwaharibu chini.
For this reason I write thus while absent, that when present I may not have to act severely in the exercise of the authority which the Lord has given me for building up, and not for pulling down.
11 Hatimaye, ndugu wa kiume na wa kike, furahini! fanyeni kazi kwa ajili ya urejesho, mtiwe moyo, kubalianeni ninyi kwa ninyi, muishi katika amani. Na Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi.
Finally, brethren, be joyful, secure perfection of character, take courage, be of one mind, live in peace. And then God who gives love and peace will be with you.
12 Salimianeni kila mmoja kwa busu takatifu.
Salute one another with a holy kiss.
13 Waumini wote wanawasalimu.
All God's people here send greetings to you.
14 Neema ya Bwana Yesu Kristo, upendo wa Mungu, na ushirika wa Roho Mtakatifu uwe pamoja nanyi nyote.
May the grace of the Lord Jesus Christ, the love of God, and the fellowship of the Holy Spirit, be with you all.