< 2 Wakorintho 13 >

1 Hii ni mara ya tatu kwamba nakuja kwenu. “Kila shitaka lazima lijengwe na uthibitisho wa mashahidi wawili au watatu.”
This the third time I am coming to you: in the mouth of two or three witnesses every word shall be established.
2 Nimekwishashasema kwa hao waliotenda dhambi kabla na kwa wengine wote wakati nilipokuwa huko mara ya pili, na ninasema tena: Nitakapokuja tena, sitawavumilia.
I have told you beforehand, and I am speaking to you in advance, as being present the second time, even now absent, that, if I may come to you again, I will not spare those who have previously sinned, and all the rest;
3 Nawaambia ninyi hili kwa sababu mnatafuta ushahidi kwamba Kristo ananena kupitia mimi. Yeye sio dhaifu kwenu, badala yake, yeye ni mwenye nguvu ndani yenu.
since you are seeking the approval of Christ, who is speaking in me, who is not weak towards you, bit mighty among you.
4 Kwa kuwa alisulibiwa katika udhaifu, lakini yu hai kwa nguvu za Mungu. Kwa kuwa sisi pia tu dhaifu ndani yake, lakini tutaishi naye kwa nguvu za Mungu miongoni mwenu.
For indeed he was crucified from weakness, but he lives by the power of God: for we indeed are weak in him, but we shall live with him through the power of God unto you.
5 Jichunguzeni wenyewe muone kama mko katika imani. Jipimeni wenyewe. Hamgundui kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu? Yeye yumo, vinginevyo kama hamjathibitishwa.
Prove your own selves, if you are in the faith; examine yourselves; whether do you not know yourselves, that Christ Jesus is in you? unless indeed you are reprobates.
6 Na nina ujasiri kwamba ninyi mtagundua kwamba sisi hatukukataliwa.
But I hope that you shall know that we are not reprobates.
7 Sasa tunaomba kwa Mungu kwamba msiweze kufanya chochote kibaya. Siombi kwamba sisi tuweze kuonekana tumepita jaribu, badala yake ninaomba kwamba muweze kufanya kilicho sahihi, Ingawa tunaweza kuonekana tumeshindwa jaribu.
But we are praying unto God, that he may do you no evil, not in order that we may appear approved, but that you may do that which is good, and we may be as disapproved.
8 Kwa kuwa sisi hatuwezi kufanya lolote kinyume na kweli, lakini ni kwa ajili ya kweli tu.
For we are not able to do any thing against the truth, but for the truth.
9 Kwa kuwa tunafurahi wakati tunapokuwa dhaifu nanyi mkiwa na nguvu. Tunaomba pia kwamba muweze kufanywa wakamilifu.
For we rejoice when we may be weak, and you may be strong: we are praying for even this, your perfection.
10 Nayaandika mambo haya wakati nikiwa mbali nanyi, ili kwamba wakati nikiwa pamoja nanyi sihitaji kuwaonesha ukali ninyi. Sihitaji kutumia mamlaka Bwana aliyonipaa mimi niwajenge na siyo kuwaharibu chini.
Therefore being absent I write these things, in order that being present, I may not use severity, according to the power which the Lord has given me for edification, and not for destruction.
11 Hatimaye, ndugu wa kiume na wa kike, furahini! fanyeni kazi kwa ajili ya urejesho, mtiwe moyo, kubalianeni ninyi kwa ninyi, muishi katika amani. Na Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi.
Finally, brethren, farewell. Be perfect; be of good comfort; think the same thing, live in peace: and the God of love and peace will be with you.
12 Salimianeni kila mmoja kwa busu takatifu.
Salute one another with a holy kiss.
13 Waumini wote wanawasalimu.
All the saints salute you.
14 Neema ya Bwana Yesu Kristo, upendo wa Mungu, na ushirika wa Roho Mtakatifu uwe pamoja nanyi nyote.
The grace of the Lord Jesus Christ, and the love of God, and the fellowship of the Holy Spirit, be with you all.

< 2 Wakorintho 13 >