< 2 Wakorintho 12 >

1 Ni lazima nijivune, lakini hakuna kinachoongezwa na hilo. Bali nitaendelea kwenye maono na mafunuo kutoka kwa Bwana.
Sem dúvida não é rentável para mim vangloriar-me, mas chegarei a visões e revelações do Senhor.
2 Namjua mtu mmoja katika Kristo ambaye miaka kumi na minne iliyopita ambaye—ikiwa katika mwili, au nje ya mwili, mimi sijui, Mungu anajua—alinyakuliwa juu katika mbingu ya tatu.
Conheço um homem em Cristo que foi arrebatado ao terceiro céu há catorze anos - seja no corpo, não sei, ou fora do corpo, não sei; Deus sabe.
3 Na ninajua kwamba mtu huyu—ikiwa katika mwili, au nje ya mwili, mimi sijui, Mungu anajua—
Conheço tal homem (se no corpo, ou fora do corpo, não sei; Deus sabe),
4 alichukuliwa juu hadi paradiso na kusikia mambo matakatifu sana kwa mtu yeyote kuyasema.
como ele foi pego no Paraíso e ouviu palavras indescritíveis, o que não é lícito para um homem proferir.
5 Kwa niaba ya mtu kama huyo nitajivuna. lakini kwa niaba yangu mwenyewe sitajivuna. Isipokuwa kuhusu udhaifu wangu.
Em nome de tal pessoa eu me gabarei, mas em meu próprio nome não me gabarei, exceto em minhas fraquezas.
6 Kama nikitaka kujivuna, nisingekuwa mpumbavu, kwa kuwa ningekuwa ninazungumza ukweli. Lakini nitaacha kujivuna, ili kwamba asiwepo yeyote atakayenifikiria zaidi ya hayo kuliko kinachoonekana ndani yangu au kusikika kutoka kwangu.
Pois se eu quiser me vangloriar, não serei tolo; pois falarei a verdade. Mas eu me abstenho, para que ninguém pense mais em mim do que aquilo que vê em mim ou ouve de mim.
7 Sitajivuna pia kwa sababu ya hayo mafunuo ya aina ya ajabu. Kwa hiyo, hivyo sitajawa na kiburi, mwiba uliwekwa ndani ya mwili wangu, mjumbe wa shetani kunishambulia mimi, ili nisigeuke kuwa mwenye majivuno.
Em razão da grandeza excessiva das revelações, de que eu não deveria ser exaltado excessivamente, foi-me dado um espinho na carne: um mensageiro de Satanás para me atormentar, de que eu não deveria ser exaltado excessivamente.
8 Mara tatu nilimsihi Bwana kuhusu hili, ili yeye kuundoa kutoka kwangu.
Com relação a esta coisa, supliquei três vezes ao Senhor que pudesse afastar-se de mim.
9 Naye akaniambia, “Neema yangu inatosha kwa ajili yako, kwa kuwa nguvu hufanywa kamili katika udhaifu. Hivyo, ningetamani zaidi kujivuna zaidi kuhusu udhaifu wangu, ili kwamba uwezo wa Kristo uweze kukaa juu yangu.
Ele me disse: “Minha graça é suficiente para você, pois meu poder se torna perfeito na fraqueza”. Portanto, de bom grado me gloriarei em minhas fraquezas, para que o poder de Cristo possa repousar sobre mim.
10 Kwa hiyo ninatosheka kwa ajili ya Kristo, katika udhaifu, katika matukano, katika shida, katika mateso, katika hali ya masikitiko. Kwa kuwa wakati nikiwa dhaifu, kisha nina nguvu.
Portanto, tenho prazer em fraquezas, em ferimentos, em necessidades, em perseguições e em angústias, por amor de Deus. Pois quando sou fraco, então sou forte.
11 Mimi nimekuwa mpumbavu! ninyi mlinilazimisha kwa hili, kwa kuwa ningekuwa nimesifiwa na ninyi. Kwa kuwa sikuwa duni kabisa kwa hao waitwao mitume—bora, hata kama mimi si kitu.
Eu me tornei tolo em me vangloriar. Você me obrigou, pois eu deveria ter sido elogiado por você, pois não sou de forma alguma inferior aos melhores apóstolos, embora eu não seja nada.
12 Ishara za kweli za mtume zilifanyika katikati yenu kwa uvumilivu, ishara na maajabu na matendo makuu.
Verdadeiramente os sinais de um apóstolo foram trabalhados entre vocês em toda perseverança, em sinais e maravilhas e obras poderosas.
13 Kwa namna gani mlikuwa wa muhimu wa chini kuliko makanisa yaliyobaki, isipokuwa kwamba sikuwa mzigo kwenu? Mnisamehe kwa kosa hili!
Pois o que há em que vocês foram feitos inferiores ao resto das assembléias, a menos que eu mesmo não tenha sido um fardo para vocês? Perdoem-me este erro!
14 Tazama! mimi niko tayari kuja kwenu kwa mara ya tatu. Sitakuwa mzigo kwenu, kwa kuwa sitaki kitu kilicho chenu. Nawataka ninyi. Kwa kuwa watoto hawapaswi kuweka akiba kwa ajili ya wazazi. Badala yake, wazazi wanapaswa kuweka akiba kwa ajili ya watoto.
Eis que esta é a terceira vez que estou pronto para ir até você, e não serei um fardo para você, pois não busco seus bens, mas você. Pois os filhos não devem poupar para os pais, mas os pais para os filhos.
15 Nitafurahi zaidi kutumia na kutumiwa kwa ajili ya nafsi zenu. Kama ninawapenda zaidi, natakiwa kupendwa kidogo?
Terei o maior prazer em gastar e ser gasto por suas almas. Se eu vos amo mais abundantemente, serei menos amado?
16 Lakini kama ilivyo, sikuwalemea mzigo ninyi. Lakini kwa kuwa mimi ni mwerevu sana, mimi ni yule aliyewashika ninyi kwa nimekuwa ambaye aliyewapata kwa udanganyifu.
Mesmo assim, eu mesmo não vos sobrecarreguei. Mas você pode dizer que sendo astuto, eu o peguei com engano.
17 Je, nilichukua kwa kujifanyia faida kwa yeyote niliyemtuma kwenu?
Será que aproveitei de você por alguém daqueles que lhe enviei?
18 Nilimsihi Tito kuja kwenu, na nilituma ndugu mwingine pamoja naye. Je, Tito aliwafanyia faida ninyi? Je, hatukutembea katika njia ile ile? Je, hatukutembea katika nyayo zile zile?
Eu exortei Titus, e enviei o irmão com ele. Titus tirou alguma vantagem de você? Não andamos com o mesmo espírito? Não andamos nos mesmos passos?
19 Mnadhani kwa muda huu wote tumekuwa tukijitetea sisi wenyewe kwenu? Mbele za Mungu, na katika Kristo, tumekuwa tukisema kila kitu kwa ajili ya kuwaimarisha ninyi.
Again, você acha que estamos nos desculpando para você? Aos olhos de Deus, nós falamos em Cristo. Mas todas as coisas, amados, são para vossa edificação.
20 Kwa kuwa nina hofu kwamba nitakapokuja naweza nisiwapate ninyi kama ninavyotamani. Nina hofu kwamba mnaweza msinipate mimi kama mnavyotamani. Nahofia kwamba kunaweza kuwa na majadiliano, wivu, milipuko ya hasira, tamaa ya ubinafsi, umbeya, kiburi, na ugomvi.
Pois tenho medo de que talvez, quando eu vier, eu possa não encontrar você como eu quero, e que eu possa ser encontrado por você como você não deseja, que talvez houvesse contendas, ciúmes, explosões de raiva, facções, calúnias, sussurros, pensamentos orgulhosos, ou motins,
21 Nina hofu kwamba nitakaporudi tena, Mungu wangu anaweza kuninyenyekeza mbele yenu. Nina hofu kwamba ninaweza kuhuzunishwa na wengi ambao wamefanya dhambi kabla ya sasa, na ambao hawakutubu uchafu, na uasherati na mambo ya tamaa wanayoyatenda.
que novamente quando eu viesse meu Deus me humilharia diante de vocês, e choraria por muitos daqueles que antes pecaram e não se arrependeram da imundícia, imoralidade sexual e luxúria que cometeram.

< 2 Wakorintho 12 >