< 2 Wakorintho 11 >

1 Nahisi kwamba mngevumiliana na mimi katika baadhi ya upumbavu. Lakini kwa kweli mnavumiliana na mimi.
Esebha huje mwenjeshelanaje nane humambo egeshilema hwahuje lyoli muhwenjeshelana nane. Hwa huje endinokelo namwe.
2 Kwa kuwa ni mwenye wivu kuhusu ninyi. Nina wivu wa Mungu kwa ajili yenu, tangu nilipowaahidi ninyi kwenye ndoa ya mume mmoja. Niliahidi kuwaleta ninyi kwa Kristo kama bikra safi.
Endinokelo ogwa Ongolobhe humbombo yenyu, awande isiku palwafishile hulimwi ulwegano ogwa lume omo. Naidie abhatwale amwe hwa Kristi nashi walendu amwiza.
3 Lakini ninaogopa kwamba kwa namna fulani, kama nyoka alivyomdanganya Eva kwa hila yake, mawazo yenu yanaweza kupotoshwa mbali kutoka kwenye ibada halisi na safi kwa Kristo.
Lakini ehwogopa huje engabhomba nashi ezoha ehahopeye o Eva hwihenga lyakwe esebho zyenyu zigabhatezya hutali afume mubada shesho nyiza hwa Kristi.
4 Kwa kuwa kwa mfano kwamba mtu fulani akaja na kutangaza Yesu mwingine tofauti na yule tuliyewahubiri. Au kwa mfano kwamba mkapokea roho mwingine tofauti na yule mliyempokea. Au kwa mfano kwamba mkapokea injili nyingine tofauti na ile mliyoipokea. Mkavumilia mambo haya vema inatosha!
Hwa huje ufwani gwa muntu uwenje ageza huhombelele uYesu owamwabho owenjenola watalumbeleye. Hushifwani huje mwaposhela opepo owenje nula wamwaposheye nashi ufwani huje mwaposhela izu elyenje nalila lyamwahovyezye. Mwanjimba goti ego huje huyiyee!
5 Kwa kuwa nadhani kwamba mimi si miongoni mwa walio duni kwa hao wanaoitwa mitume-bora.
Hwa huje anesendingene nabhala awantu bhabhali bila hantu bhala bhabha kwiziwe antumi ahwiza.
6 Lakini hata kama mimi sijafundishwa katika kutoa hotuba, siko hivyo katika maarifa. Kwa kila namna na katika mambo yote tumelifanya hili kujulikana kwenu.
Ane nemwene nomowandogozezye afumwe amazyu, sagaendiesho hunjele hwalyolyoti lila tilibhombile humanyishe hwenyu.
7 Je, nilifanya dhambi kwa kujinyenyekeza mwenyewe ili ninyi muweze kuinuliwa? Kwa kuwa nilihubiri kwa uhuru injili ya Mungu kwenu.
Je nabhombile mbibhi ahwishe nene ilimwe mubhe amwanya? Hwa huje nalumbelele wenee izuu elya Ngolobhe awahulimwi.
8 Nilinyang'anya makanisa mengine kwa kupokea msaada kutoka kwao ili kwamba ningeweza kuwahudumia ninyi.
Nafyulile amabhaza gamwabho naposhele wanavwize afume amwabho huje embweye abhalishe amwe.
9 Wakati nilipokuwa nanyi na nilikuwa katika uhitaji, sikumlemea yeyote. Kwa kuwa mahitaji yangu yalitoshelezwa na ndugu waliokuja kutoka Makedonia. Katika kila kitu nimejizuia mwenyewe kutokuwa mzigo kwenu, na nitaendelea kufanya hivyo.
Panali namwe nalihali eyeupena lakini saganalabhile hohonti, eshida zyane zyanjiye aholo bhahenzele afume hu Makedonia. Kwa kila hantu nahwizijile nene esibhelizigo hulimwi, embawendele abhombe shesho.
10 Kama kweli ya Kristo ilivyo ndani yangu, huku kujisifu kwangu, hakutanyamazishwa katika sehemu za Akaya.
Nashi elyoli sehweli mhati yane, ohu ahwintofye hwane senaipomezewa katika ensi iya Akaya.
11 Kwa nini? Kwa sababu siwapendi? Mungu anajua nawapenda.
Yenu? hahuje sembagene? Ongolobhe amenye huje embagene.
12 Lakini kile ninachokifanya, nitakifanya pia. Nitakifanya ili kwamba niweze kuzuia nafasi ya wale wanaotamani nafasi ya kuwa kama tulivyo katika kile kile wanachojivunia.
Lakini lilalyebhomba, embalibhombe na engalibhomba huje ehwiziye omwoyo hwabhala bhabhaziliha umwoyo nashi satihweli galagala gabha sobhela.
13 Kwa kuwa watu wale ni mitume wa uongo na watendakazi wadanganyifu. Wanajigeuza wenyewe kama mitume wa Kristo.
Hwa huje bhala bhatumwa bhilenka bhabhomba mbombo abhilenga bhahwigaluzya huuje bhatumwa bha Kristi.
14 Na hii haishangazi, kwa kuwa hata Shetani hujigeuza mwenyewe kama malaika wa nuru.
Neeli sagaliswijisha hwa huje uSetano ahwigaluzanya yuyo nashi ohala uzelu nu bhozyo.
15 Hii haina mshangao mkubwa kama watumishi wake pia kujigeuza wenyewe kama watumishi wa haki. Hatma yao itakuwa kama matendo yao yastahilivyo.
Eli sagalitisha hwaa bhabhomba mbombo bhakwe aigaluzanye bhabhe nashi abhomba mbombo bhelyoli omwisho gwabho gwaibha nashi amatendo gabho gawaziwa.
16 Nasema tena: Basi na asiwepo mtu yeyote anayefikiri mimi ni mpumbavu. Lakini kama mkifanya, nipokeeni mimi kama mpumbavu ili niweze kujisifu kidogo.
Eyanga nantele agaje abhe omtu wowoti wasebha huje ane sagaendini njele. Lakini kambhombe, nejeleli ane nashi olema nane ahwintuntumule hashee.
17 Kile ninachosema kuhusu huku kujiamini kwa kujivuna hakuhukumiwi na Bwana, lakini nazungumza kama mpumbavu.
Lila lyeyayanga ahwintuntumile naajivune hagale gwa nu gosi, lakini eyanga nashi ulemaa.
18 Kwa vile watu wengi hujivuna kwa jinsi ya mwili, nitajivuna pia.
Hwa huje abhantu abhinji bhahwilola hubele, embahwintutumle nane.
19 Kwa kuwa mlichukuliana kwa furaha na wapumbavu, ninyi wenyewe mna busara!
Hwa huje mwakhatene huhwinza nuubhibhi, amwee namwee muhwisizye!
20 Kwa kuwa mnachukuliana na mtu kama akikutia utumwani, kama husababisha mgawanyiko kati yenu, kama akiwatumia ninyi kwa faida yake, kama akijiweka juu hewani, au kama akiwapiga usoni.
Yenu mkhatana numuntu kabheshe mmateso nashi samnyapana kati yenyu, nashi abhabheshe bhabhomba mbombo amwe hufaida yakwe, nashi ahwibheshe humwanya mhala, au kashile abhabhome humaso.
21 Nitasema kwa aibu yetu kwamba sisi tukuwa dhaifu sana kufanya hivyo. Na bado kama yeyote akijivuna— nazungumza kama mpumbavu— mimi pia nitajivuna.
Embayanje nesoni huje talibhahwinu sana abhombe eshoo. Nabadonkashile aweli wahwilola— eyanga nashi olema— nane embahwilole.
22 Je, wao ni Wayahudi? Na mimi ni hivyo. Je, wao ni Waisraeli? Na mimi ni hivyo. Je, wao ni uzao wa Abrahamu? Na mimi ni hivyo.
Je, abhene Bhayahudi? Nane endishesho. Je abhene Bhaisraeli? Nane shesho. Je, abhene bhahwa Iblahimu? Nane shesho.
23 Je, wao ni watumishi wa Kristo? (Nanena kama nilirukwa na akili zangu. ) Mimi ni zaidi. Nimekuwa hata katika kazi ngumu zaidi, mbali zaidi ya kuwa vifungoni, katika kupigwa kupita vipimo, katika kukabili hatari nyingi za kifo.
Je, abhene bhatumwa bha Kristi? (Eyanga nashi umuntu wezyepile enjele zyane.) Ane sananyene. Endinashi pambombo ehome sana uhutali sana ugaga endimchabho, ashilile ahomwe naashilile ahomwe, apalamile ehatali enyinji hata afwe.
24 Kutoka kwa Wayahudi nimepokea mara tano “mapigo arobaini kutoa moja.”
Afume hwa Bhayahudi eposheye malahasanu, abhomwe mala alobaini afume limo.”
25 Mara tatu nilipigwa kwa fimbo. Mara moja nilipigwa mawe. Mara tatu nilinusurika melini. Nimetumia usiku na mchana katika bahari wazi.
Mala hatatu nabhomwilwe nendesa. Mala limo nabhomwilwa amawe. Mala hantatu nanusulishe mumeli enjendile nusiku na pasanya mbahali wazi.
26 Nimekuwa katika safari za mara kwa mara, katika hatari za mito, katika hatari za majambazi, katika hatari kutoka kwa watu wangu mwenyewe, katika hatari kutoka kwa watu wa mataifa, katika hatari ya mji, katika hatari ya jangwa, katika hatari ya bahari, katika hatari kutoka kwa ndugu waongo.
Naliinee safali izye wilawila, nehatali ezya mmeze, nehatali ezya ambuda, nehali ezyafume hwabhantu bhanenene, nehatali zya bhantu hwimataifa, nehatali iyammeze, nehatali iyamwipoli, nehatali iya mwiwaa, nehatali iyafume waholo bhane adodo.
27 Nimekuwa katika kazi ngumu na katika maisha magumu, katika usiku mwingi wa kutolala, katika njaa na kiu, mara nyingi katika kufunga, katika baridi na uchi.
Endi mbombo ehome namaisha amakhome lumo lumo etoloha nu siku sagagona nashi ezala nahomelwe, mala nyinji afunje, lumo embe welele nisasa.
28 Mbali na kila kitu kingine, kuna msukumo wa kila siku juu yangu wa wasiwasi wangu kwa ajili ya makanisa.
Hutali na hantu hohoti, naliwahitume kila lisiku naline wasiwasi namabhaza. Yonanu obhinu nanene saga endibhinu?
29 Nani ni dhaifu, na mimi siyo dhaifu? Nani amesababisha mwingine kuanguka dhambini, na mimi siungui ndani?
Yonanu wasababisizye omo agwe mbiwi, nane sembile mhati?
30 Kama ni lazima nijivune, nitajivunia kuhusu kile kinachoonyesha udhaifu wangu.
Hwahuje nane ehwivuna, na embahwivune ahusu nahabhonesha ubhinu wane.
31 Mungu na Baba wa Bwana Yesu, yeye ambaye anatukuzwa milele, anajua kwamba mimi sidanganyi. (aiōn g165)
Ongolobhe nu Daada owa Gosi uYesu, oyo umene atufiwa wenee, amenye huje ane sekhopela. (aiōn g165)
32 Kule Dameski, mkuu wa mkoa chini ya mfalme Areta alikuwa akiulinda mji wa Dameski ili kunikamata.
Hula hu Dameski, ugosi uwe mkoa pasi ya mwene aleta aliagudima omji gwa Dameski huje ahante.
33 Lakini niliwekwa kikapuni, kupitia dirishani katika ukuta, na nikanusurika kutoka mikononi mwake.
Lakini abhehwele mshikapo, ashilile mwidirisha na mlubhomba, nanusulishe akhatwe mmabhona gakwe.

< 2 Wakorintho 11 >