< 2 Wakorintho 11 >
1 Nahisi kwamba mngevumiliana na mimi katika baadhi ya upumbavu. Lakini kwa kweli mnavumiliana na mimi.
ⲁ̅ⲛⲁⲛⲟⲩⲥ ⲉⲛⲉⲧⲉⲧⲛⲁⲁⲛⲉⲭⲉ ⲙ̅ⲙⲟⲓ̈ ⲛ̅ⲟⲩⲕⲟⲩⲓ̈ ⲙ̅ⲙⲛ̅ⲧⲁⲑⲏⲧ. ⲁⲗⲗⲁ ⲧⲉⲧⲛ̅ⲁⲛⲉⲭⲉ.
2 Kwa kuwa ni mwenye wivu kuhusu ninyi. Nina wivu wa Mungu kwa ajili yenu, tangu nilipowaahidi ninyi kwenye ndoa ya mume mmoja. Niliahidi kuwaleta ninyi kwa Kristo kama bikra safi.
ⲃ̅ϯⲕⲱϩ ⲅⲁⲣ ⲉⲣⲱⲧⲛ̅ ⲛ̅ⲟⲩⲕⲱϩ ⲛ̅ⲧⲉⲡⲛⲟⲩⲧⲉ. ⲁⲓ̈ⲥⲃ̅ⲧⲱⲧ ⲅⲁⲣ ⲉⲡⲁⲣϩⲓⲥⲧⲁ ⲙ̅ⲙⲱⲧⲛ̅ ⲛ̅ⲟⲩⲡⲁⲣⲑⲉⲛⲟⲥ ⲉⲥⲟⲩⲁⲁⲃ. ⲛ̅ⲟⲩϩⲁⲓ̈ ⲛ̅ⲟⲩⲱⲧ ⲡⲉⲭ̅ⲥ̅.
3 Lakini ninaogopa kwamba kwa namna fulani, kama nyoka alivyomdanganya Eva kwa hila yake, mawazo yenu yanaweza kupotoshwa mbali kutoka kwenye ibada halisi na safi kwa Kristo.
ⲅ̅ϯⲣ̅ϩⲟⲧⲉ ⲇⲉ ϫⲉ ⲙⲏⲡⲟⲧⲉ ⲛ̅ⲑⲉ ⲛ̅ⲧⲁⲡϩⲟϥ ⲉⲝⲁⲡⲁⲧⲁ ⲛ̅ⲉⲩϩⲁ ϩⲛ̅ⲧⲉϥⲡⲁⲛⲟⲩⲣⲅⲓⲁ ⲛ̅ⲥⲉⲧⲁⲕⲟ ⲛ̅ϭⲓⲛⲉⲧⲛ̅ϩⲏⲧ ⲉⲃⲟⲗ ϩⲛ̅ⲧⲙⲛ̅ⲧϩⲁⲡⲗⲟⲩⲥ ⲙⲛ̅ⲡⲧⲃ̅ⲃⲟ ⲉⲧϫⲓ ⲉϩⲟⲩⲛ ⲉⲡⲉⲭ̅ⲥ̅.
4 Kwa kuwa kwa mfano kwamba mtu fulani akaja na kutangaza Yesu mwingine tofauti na yule tuliyewahubiri. Au kwa mfano kwamba mkapokea roho mwingine tofauti na yule mliyempokea. Au kwa mfano kwamba mkapokea injili nyingine tofauti na ile mliyoipokea. Mkavumilia mambo haya vema inatosha!
ⲇ̅ⲉϣϫⲉⲡⲉⲧⲛⲏⲩ ⲅⲁⲣ ⲛⲁⲧⲁϣⲉⲟⲉⲓϣ ⲛⲏⲧⲛ̅ ⲛ̅ⲕⲉⲓ̅ⲥ̅ ⲉⲙⲡⲉⲛⲧⲁϣⲉⲟⲉⲓϣ ⲙ̅ⲙⲟϥ. ⲏ̅ ⲧⲉⲧⲛⲁϫⲓⲕⲉⲡ̅ⲛ̅ⲁ̅ ⲉⲙⲡⲉⲧⲛ̅ϫⲓⲧϥ̅ ⲏ̅ ⲕⲉⲉⲩⲁⲅⲅⲉⲗⲓⲟⲛ ⲉⲙⲡⲉⲧⲛ̅ϣⲟⲡϥ̅ ⲉⲣⲱⲧⲛ̅. ⲉⲓ̈ⲉ ⲕⲁⲗⲱⲥ ⲧⲉⲧⲛ̅ⲁⲛⲉⲭⲉ.
5 Kwa kuwa nadhani kwamba mimi si miongoni mwa walio duni kwa hao wanaoitwa mitume-bora.
ⲉ̅ϯⲙⲉⲉⲩⲉ ⲅⲁⲣ ϫⲉ ⲙ̅ⲡⲓϣⲱⲱⲧ ⲛ̅ⲗⲁⲁⲩ ⲡⲁⲣⲁⲛ̅ⲛⲟϭ ⲛ̅ⲁⲡⲟⲥⲧⲟⲗⲟⲥ.
6 Lakini hata kama mimi sijafundishwa katika kutoa hotuba, siko hivyo katika maarifa. Kwa kila namna na katika mambo yote tumelifanya hili kujulikana kwenu.
ⲋ̅ⲉϣϫⲉⲁⲛⲅ̅ⲟⲩϩⲓⲇⲓⲱⲧⲏⲥ ⲇⲉ ϩⲙ̅ⲡϣⲁϫⲉ. ⲁⲗⲗⲁ ϩⲙ̅ⲡⲥⲟⲟⲩⲛ ⲁⲛ. ⲁⲗⲗⲁ ϩⲛ̅ⲟⲩⲟⲉⲓϣ ⲛⲓⲙ ⲁⲛⲟⲩⲟⲛϩⲛ̅ ⲉⲣⲱⲧⲛ̅ ϩⲛ̅ϩⲱⲃ ⲛⲓⲙ.
7 Je, nilifanya dhambi kwa kujinyenyekeza mwenyewe ili ninyi muweze kuinuliwa? Kwa kuwa nilihubiri kwa uhuru injili ya Mungu kwenu.
ⲍ̅ⲙⲏ ⲟⲩⲛⲟⲃⲉ ⲡⲉⲛⲧⲁⲓ̈ⲁⲁϥ ⲉⲁⲓ̈ⲑⲃ̅ⲃⲓⲟⲓ̈ ϫⲉⲕⲁⲁⲥ ⲛ̅ⲧⲱⲧⲛ̅ ⲉⲧⲉⲧⲛⲉϫⲓⲥⲉ. ϫⲉ ⲁⲓ̈ⲉⲩⲁⲅⲅⲉⲗⲓⲍⲉ ⲛⲏⲧⲛ̅ ⲙ̅ⲡⲉⲩⲁⲅⲅⲉⲗⲓⲟⲛ ⲙ̅ⲡⲛⲟⲩⲧⲉ ⲛ̅ϫⲓⲛϫⲏ.
8 Nilinyang'anya makanisa mengine kwa kupokea msaada kutoka kwao ili kwamba ningeweza kuwahudumia ninyi.
ⲏ̅ⲁⲓ̈ⲥⲩⲗⲁ ⲛ̅ϩⲉⲛⲕⲉⲉⲕⲕⲗⲏⲥⲓⲁ. ⲁⲓ̈ϫⲓ ⲙ̅ⲡⲁⲟⲯⲱⲛⲓⲟⲛ ⲉⲉⲓⲇⲓⲁⲕⲟⲛⲓ ⲛⲏⲧⲛ̅.
9 Wakati nilipokuwa nanyi na nilikuwa katika uhitaji, sikumlemea yeyote. Kwa kuwa mahitaji yangu yalitoshelezwa na ndugu waliokuja kutoka Makedonia. Katika kila kitu nimejizuia mwenyewe kutokuwa mzigo kwenu, na nitaendelea kufanya hivyo.
ⲑ̅ⲁⲩⲱ ⲛ̅ⲧⲉⲣⲓϣⲱⲱⲧ ⲉⲉⲓϩⲁⲧⲛ̅ⲧⲏⲩⲧⲛ̅ ⲙ̅ⲡⲓⲟⲩⲉϩϩⲓⲥⲉ ⲉⲗⲁⲁⲩ. ⲡⲁϣⲱⲱⲧ ⲅⲁⲣ ⲁⲛⲉⲥⲛⲏⲩ ϫⲟⲕϥ̅ ⲉⲃⲟⲗ ⲛ̅ⲧⲉⲣⲟⲩⲉⲓ ⲉⲃⲟⲗ ϩⲛ̅ⲧⲙⲁⲕⲉⲇⲟⲛⲓⲁ. ⲁⲩⲱ ϩⲛ̅ϩⲱⲃ ⲛⲓⲙ ⲁⲓ̈ϩⲁⲣⲉϩ ⲉⲣⲟⲓ̈ ⲉⲧⲙ̅ϩⲣⲟϣ ⲉⲣⲱⲧⲛ̅. ⲁⲩⲱ ⲟⲛ ϯⲛⲁϩⲁⲣⲉϩ.
10 Kama kweli ya Kristo ilivyo ndani yangu, huku kujisifu kwangu, hakutanyamazishwa katika sehemu za Akaya.
ⲓ̅ⲟⲩⲛ̅ⲟⲩⲙⲉ ⲛ̅ⲧⲉⲡⲉⲭ̅ⲥ̅ ⲛ̅ϩⲏⲧ. ϫⲉ ⲙ̅ⲡⲉⲓ̈ϣⲟⲩϣⲟⲩ ⲛⲁⲱϫⲛ̅ ⲁⲛ ⲉϩⲟⲩⲛ ⲉⲣⲟⲓ̈ ϩⲛ̅ⲛⲉⲕⲗⲓⲙⲁ ⲛ̅ⲧⲁⲭⲁⲓⲁ.
11 Kwa nini? Kwa sababu siwapendi? Mungu anajua nawapenda.
ⲓ̅ⲁ̅ⲉⲧⲃⲉⲟⲩ ϫⲉ ϯⲙⲉ ⲙ̅ⲙⲱⲧⲛ̅ ⲁⲛ. ⲡⲛⲟⲩⲧⲉ ⲡⲉⲧⲥⲟⲟⲩⲛ.
12 Lakini kile ninachokifanya, nitakifanya pia. Nitakifanya ili kwamba niweze kuzuia nafasi ya wale wanaotamani nafasi ya kuwa kama tulivyo katika kile kile wanachojivunia.
ⲓ̅ⲃ̅ⲡⲉϯⲉⲓⲣⲉ ⲇⲉ ⲙ̅ⲙⲟϥ ϯⲛⲁⲁⲁϥ ⲟⲛ. ϫⲉⲕⲁⲥ ⲉⲓ̈ⲉϭⲱϫⲉ ⲉⲃⲟⲗ ⲛ̅ⲧⲁⲫⲟⲣⲙⲏ ⲛ̅ⲛⲉⲧⲟⲩⲉϣⲁⲫⲟⲣⲙⲏ. ϫⲉ ⲉⲩⲉϩⲉ ⲉⲣⲟⲟⲩ ϩⲙ̅ⲡⲉⲧⲟⲩϣⲟⲩϣⲟⲩ ⲙ̅ⲙⲟⲟⲩ ⲛ̅ϩⲏⲧϥ̅ ⲛ̅ⲧⲉⲛϩⲉ ϩⲱⲱⲛ.
13 Kwa kuwa watu wale ni mitume wa uongo na watendakazi wadanganyifu. Wanajigeuza wenyewe kama mitume wa Kristo.
ⲓ̅ⲅ̅ⲛⲁⲓ̈ ⲅⲁⲣ ⲛ̅ⲧⲉⲉⲓⲙⲓⲛⲉ ϩⲉⲛⲁⲡⲟⲥⲧⲟⲗⲟⲥ ⲛ̅ⲛⲟⲩϫ ⲛⲉ. ϩⲉⲛⲉⲣⲅⲁⲧⲏⲥ ⲛ̅ⲕⲣⲟϥ ⲛⲉ. ⲉⲩϫⲓϩⲣⲃ̅ ϩⲱⲥ ⲁⲡⲟⲥⲧⲟⲗⲟⲥ ⲙ̅ⲡⲉⲭ̅ⲥ̅.
14 Na hii haishangazi, kwa kuwa hata Shetani hujigeuza mwenyewe kama malaika wa nuru.
ⲓ̅ⲇ̅ⲁⲩⲱ ⲛ̅ⲟⲩϣⲡⲏⲣⲉ ⲁⲛ ⲧⲉ. ⲛ̅ⲧⲟϥ ⲅⲁⲣ ⲡⲥⲁⲧⲁⲛⲁⲥ ϣⲁϥϫⲓϩⲣⲃ̅ ϩⲱⲥ ⲁⲅⲅⲉⲗⲟⲥ ⲛ̅ⲧⲉⲡⲟⲩⲟⲉⲓⲛ.
15 Hii haina mshangao mkubwa kama watumishi wake pia kujigeuza wenyewe kama watumishi wa haki. Hatma yao itakuwa kama matendo yao yastahilivyo.
ⲓ̅ⲉ̅ⲛ̅ⲟⲩⲛⲟϭ ⲁⲛ ϭⲉ ⲡⲉ. ⲉϣϫⲉⲛⲉϥⲕⲉⲇⲓⲁⲕⲟⲛⲟⲥ ϫⲓϩⲣⲃ̅ ϩⲱⲥ ⲇⲓⲁⲕⲟⲛⲟⲥ ⲛ̅ⲧⲉⲧⲇⲓⲕⲁⲓⲟⲥⲩⲛⲏ. ⲛⲁⲓ̈ ⲉⲣⲉⲧⲉⲩϩⲁⲏ ⲛⲁϣⲱⲡⲉ ⲕⲁⲧⲁⲛⲉⲩϩⲃⲏⲩⲉ.
16 Nasema tena: Basi na asiwepo mtu yeyote anayefikiri mimi ni mpumbavu. Lakini kama mkifanya, nipokeeni mimi kama mpumbavu ili niweze kujisifu kidogo.
ⲓ̅ⲋ̅ϯⲛⲁϫⲟⲟⲥ ⲟⲛ ⲙ̅ⲡⲣ̅ⲧⲣⲉⲟⲩⲁ ⲙⲉⲉⲩⲉ ⲉⲣⲟⲓ̈ ϫⲉ ⲁⲛⲅ̅ⲟⲩⲁⲑⲏⲧ. ⲉϣϫⲉⲙ̅ⲙⲟⲛ ⲕⲁⲛ ϣⲟⲡⲧ̅ ⲉⲣⲱⲧⲛ̅ ϩⲱⲥ ⲁⲑⲏⲧ. ϫⲉⲕⲁⲁⲥ ⲉⲓ̈ⲉϣⲟⲩϣⲟⲩ ⲙ̅ⲙⲟⲓ̈ ⲛ̅ⲟⲩϣⲏⲙ.
17 Kile ninachosema kuhusu huku kujiamini kwa kujivuna hakuhukumiwi na Bwana, lakini nazungumza kama mpumbavu.
ⲓ̅ⲍ̅ⲡⲉϯϫⲱ ⲙ̅ⲙⲟϥ ⲛⲉⲓ̈ϫⲱ ⲙ̅ⲙⲟϥ ⲁⲛ ⲕⲁⲧⲁⲡϫⲟⲉⲓⲥ. ⲁⲗⲗⲁ ϩⲱⲥ ϩⲛ̅ⲟⲩⲙⲛ̅ⲧⲁⲑⲏⲧ ϩⲙ̅ⲡⲧⲁϫⲣⲟ ⲙ̅ⲡϣⲟⲩϣⲟⲩ.
18 Kwa vile watu wengi hujivuna kwa jinsi ya mwili, nitajivuna pia.
ⲓ̅ⲏ̅ⲉⲃⲟⲗ ϫⲉ ⲟⲩⲛ̅ϩⲁϩ ϣⲟⲩϣⲟⲩ ⲙ̅ⲙⲟⲟⲩ ⲕⲁⲧⲁⲥⲁⲣⲝ̅. ϯⲛⲁϣⲟⲩϣⲟⲩ ϩⲱ ⲙ̅ⲙⲟⲓ̈.
19 Kwa kuwa mlichukuliana kwa furaha na wapumbavu, ninyi wenyewe mna busara!
ⲓ̅ⲑ̅ⲧⲉⲧⲛ̅ⲁⲛⲉⲭⲉ ⲅⲁⲣ ⲉϩⲛⲏⲧⲛ̅ ⲛ̅ⲛⲓⲁⲑⲏⲧ ⲛ̅ⲧⲉⲧⲛ̅ϩⲉⲛⲥⲁⲃⲉⲉⲩ.
20 Kwa kuwa mnachukuliana na mtu kama akikutia utumwani, kama husababisha mgawanyiko kati yenu, kama akiwatumia ninyi kwa faida yake, kama akijiweka juu hewani, au kama akiwapiga usoni.
ⲕ̅ⲧⲉⲧⲛ̅ⲁⲛⲉⲭⲉ ⲅⲁⲣ ⲙ̅ⲡⲉⲧⲉⲝⲁⲡⲁⲧⲁ ⲙ̅ⲙⲱⲧⲛ̅. ⲙ̅ⲡⲉⲧⲕ̅ⲕⲧⲟ ⲉⲃⲟⲗ. ⲙ̅ⲡⲉⲧⲉⲓⲣⲉ ⲙ̅ⲙⲱⲧⲛ̅ ⲛ̅ϩⲙ̅ϩⲁⲗ. ⲙ̅ⲡⲉⲧⲟⲩⲱⲙ. ⲙ̅ⲡⲉⲧϫⲓ. ⲙ̅ⲡⲉⲧϫⲓⲥⲉ ⲙ̅ⲙⲟϥ. ⲙ̅ⲡⲉⲧϩⲓⲟⲩⲉ ⲉϩⲟⲩⲛ ⲉⲡⲉⲧⲛ̅ϩⲟ.
21 Nitasema kwa aibu yetu kwamba sisi tukuwa dhaifu sana kufanya hivyo. Na bado kama yeyote akijivuna— nazungumza kama mpumbavu— mimi pia nitajivuna.
ⲕ̅ⲁ̅ⲉⲓ̈ϫⲱ ⲙ̅ⲙⲟⲥ ⲕⲁⲧⲁⲟⲩⲥⲱϣ. ϩⲱⲥ ϩⲟⲧⲓ ϫⲉ ⲁⲛⲟⲛ ⲁⲛϭⲃ̅ⲃⲉ. ϩⲙ̅ⲡⲉⲧⲉⲣⲉⲟⲩⲁ ⲇⲉ ⲛⲁⲧⲟⲗⲙⲁ ⲛ̅ϩⲏⲧϥ̅ ϩⲛ̅ⲟⲩⲙⲛ̅ⲧⲁⲑⲏⲧ ⲉⲉⲓϫⲱ ⲙ̅ⲙⲟⲥ ϯⲛⲁⲧⲟⲗⲙⲁ ϩⲱ.
22 Je, wao ni Wayahudi? Na mimi ni hivyo. Je, wao ni Waisraeli? Na mimi ni hivyo. Je, wao ni uzao wa Abrahamu? Na mimi ni hivyo.
ⲕ̅ⲃ̅ϩⲉⲛϩⲉⲃⲣⲁⲓⲟⲥ ⲛⲉ ⲁⲛⲅ̅ⲟⲩⲁ ϩⲱ. ϩⲉⲛⲓ̈ⲥⲣⲁⲏⲗⲓⲧⲏⲥ ⲛⲉ ⲁⲛⲅ̅ⲟⲩⲁ ϩⲱ. ⲡⲉⲥⲡⲉⲣⲙⲁ ⲛ̅ⲁⲃⲣⲁϩⲁⲙ ⲛⲉ ⲁⲛⲟⲕ ϩⲱ.
23 Je, wao ni watumishi wa Kristo? (Nanena kama nilirukwa na akili zangu. ) Mimi ni zaidi. Nimekuwa hata katika kazi ngumu zaidi, mbali zaidi ya kuwa vifungoni, katika kupigwa kupita vipimo, katika kukabili hatari nyingi za kifo.
ⲕ̅ⲅ̅ϩⲉⲛⲇⲓⲁⲕⲟⲛⲟⲥ ⲙ̅ⲡⲉⲭ̅ⲥ̅ ⲛⲉ. ⲉⲉⲓϫⲱ ⲙ̅ⲙⲟⲥ ϩⲛ̅ⲟⲩⲙⲛ̅ⲧⲁⲑⲏⲧ ⲁⲛⲅ̅ⲟⲩⲁ ⲉϩⲟⲩⲉⲣⲟⲟⲩ. ϩⲛ̅ϩⲉⲛϩⲓⲥⲉ ⲉϩⲟⲩⲉⲣⲟⲟⲩ. ϩⲛ̅ϩⲉⲛϣⲧⲉⲕⲱⲟⲩ ⲉϩⲟⲩⲉⲣⲟⲟⲩ. ϩⲛ̅ϩⲉⲛⲥⲏϣⲉ ⲉⲛⲁϣⲱⲟⲩ. ϩⲛ̅ϩⲉⲛⲙⲟⲩ ⲛ̅ϩⲁϩ ⲛ̅ⲥⲟⲡ.
24 Kutoka kwa Wayahudi nimepokea mara tano “mapigo arobaini kutoa moja.”
ⲕ̅ⲇ̅ⲉⲃⲟⲗ ϩⲓⲧⲟⲟⲧⲟⲩ ⲛ̅ⲛ̅ⲓ̈ⲟⲩⲇⲁⲓ̈ ⲁⲓ̈ϫⲓϩⲙⲉ ⲛ̅ⲥⲁϣ ϣⲁⲧⲛ̅ⲟⲩⲁ ⲛ̅ϯⲟⲩ ⲛ̅ⲥⲟⲡ.
25 Mara tatu nilipigwa kwa fimbo. Mara moja nilipigwa mawe. Mara tatu nilinusurika melini. Nimetumia usiku na mchana katika bahari wazi.
ⲕ̅ⲉ̅ⲁⲩϩⲓⲟⲩⲉ ⲉⲣⲟⲓ̈ ⲛ̅ⲛ̅ϭⲉⲣⲟⲟⲃ ⲛ̅ϣⲙ̅ⲧⲥⲱⲱⲡ. ⲁⲩϩⲓⲱⲛⲉ ⲉⲣⲟⲓ̈ ⲛⲟⲩⲥⲟⲡ. ⲁⲡϫⲟⲓ̈ ⲃⲱⲕ ϩⲁⲣⲟⲓ̈ ⲛ̅ϣⲙ̅ⲧⲥⲱⲱⲡ. ⲁⲓ̈ⲣ̅ⲟⲩϩⲟⲟⲩ ⲙⲛ̅ⲟⲩⲟⲩϣⲏ ϩⲙ̅ⲡⲛⲟⲩⲛ.
26 Nimekuwa katika safari za mara kwa mara, katika hatari za mito, katika hatari za majambazi, katika hatari kutoka kwa watu wangu mwenyewe, katika hatari kutoka kwa watu wa mataifa, katika hatari ya mji, katika hatari ya jangwa, katika hatari ya bahari, katika hatari kutoka kwa ndugu waongo.
ⲕ̅ⲋ̅ϩⲛ̅ϩⲉⲛϩⲓⲏ ⲙ̅ⲙⲟⲟϣⲉ ⲛ̅ϩⲁϩ ⲛ̅ⲥⲟⲡ. ϩⲛ̅ⲛ̅ⲕⲓⲛⲇⲩⲛⲟⲥ ⲛ̅ⲉⲓⲉⲣⲱⲟⲩ. ϩⲛ̅ⲛ̅ⲕⲓⲛⲇⲩⲛⲟⲥ ⲛ̅ⲛ̅ⲥⲟⲟⲛⲉ· ϩⲛ̅ⲛ̅ⲕⲓⲛⲇⲩⲛⲟⲥ ⲉⲃⲟⲗ ϩⲙ̅ⲡⲁⲅⲉⲛⲟⲥ. ϩⲛ̅ⲛ̅ⲕⲓⲛⲇⲩⲛⲟⲥ ⲉⲃⲟⲗ ϩⲛ̅ⲛ̅ϩⲉⲑⲛⲟⲥ. ϩⲛ̅ⲛ̅ⲕⲓⲛⲇⲩⲛⲟⲥ ⲛⲧⲡⲟⲗⲓⲥ. ϩⲛ̅ⲛ̅ⲕⲓⲛⲇⲩⲛⲟⲥ ⲙ̅ⲡϫⲁⲉⲓⲉ. ϩⲛ̅ⲛ̅ⲕⲓⲛⲇⲩⲛⲟⲥ ⲛ̅ⲑⲁⲗⲁⲥⲥⲁ. ϩⲛ̅ⲛ̅ⲕⲓⲛⲇⲩⲛⲟⲥ ϩⲛ̅ϩⲉⲛⲥⲛⲏⲩ ⲛ̅ⲛⲟⲩϫ.
27 Nimekuwa katika kazi ngumu na katika maisha magumu, katika usiku mwingi wa kutolala, katika njaa na kiu, mara nyingi katika kufunga, katika baridi na uchi.
ⲕ̅ⲍ̅ϩⲛ̅ⲟⲩϩⲓⲥⲉ. ⲙⲛ̅ⲟⲩⲙ̅ⲕⲁϩ. ϩⲛ̅ϩⲉⲛⲟⲩϣⲏ ⲛ̅ⲣⲟⲉⲓⲥ ⲛ̅ϩⲁϩ ⲛ̅ⲥⲟⲡ. ϩⲛ̅ⲟⲩϩⲕⲟ ⲙⲛ̅ⲟⲩⲉⲓⲃⲉ. ϩⲛ̅ϩⲉⲛⲛⲏⲥⲧⲓⲁ ⲉⲛⲁϣⲱⲟⲩ. ϩⲛ̅ⲟⲩϫⲁϥ ⲙⲛ̅ⲟⲩⲕⲱⲕⲁϩⲏⲩ.
28 Mbali na kila kitu kingine, kuna msukumo wa kila siku juu yangu wa wasiwasi wangu kwa ajili ya makanisa.
ⲕ̅ⲏ̅ⲭⲱⲣⲓⲥ ⲛⲉⲧϩⲓⲃⲟⲗ ⲛⲉⲧⲛⲏⲩ ⲉϫⲱⲓ̈ ⲙ̅ⲙⲏⲛⲉ ⲛ̅ⲣⲟⲟⲩϣ ⲛ̅ⲛ̅ⲉⲕⲕⲗⲏⲥⲓⲁ ⲧⲏⲣⲟⲩ.
29 Nani ni dhaifu, na mimi siyo dhaifu? Nani amesababisha mwingine kuanguka dhambini, na mimi siungui ndani?
ⲕ̅ⲑ̅ⲛⲓⲙ ⲡⲉⲧϣⲱⲛⲉ ⲉⲛϯϣⲱⲛⲉ ⲁⲛ ⲛⲙ̅ⲙⲁϥ. ⲛⲓⲙ ⲡⲉϣⲁϥⲥⲕⲁⲛⲇⲁⲗⲓⲍⲉ. ⲁⲩⲱ ⲁⲛⲟⲕ ⲉⲙⲉⲉⲓϫⲉⲣⲟ.
30 Kama ni lazima nijivune, nitajivunia kuhusu kile kinachoonyesha udhaifu wangu.
ⲗ̅ⲉϣϫⲉϣϣⲉ ⲉϣⲟⲩϣⲟⲩ ⲉⲉⲓⲛⲁϣⲟⲩϣⲟⲩ ⲙ̅ⲙⲟⲓ̈ ϩⲛ̅ⲛⲁⲧⲁⲥⲑⲉⲛⲓⲁ·
31 Mungu na Baba wa Bwana Yesu, yeye ambaye anatukuzwa milele, anajua kwamba mimi sidanganyi. (aiōn )
ⲗ̅ⲁ̅ⲡⲛⲟⲩⲧⲉ ⲁⲩⲱ ⲡⲉⲓⲱⲧ ⲙ̅ⲡⲉⲛϫⲟⲉⲓⲥ ⲓ̅ⲥ̅ ⲥⲟⲟⲩⲛ ⲡⲉⲧⲥⲙⲁⲙⲁⲁⲧ ϣⲁⲛⲓⲉⲛⲉϩ ϫⲉ ⲛ̅ϯϫⲓϭⲟⲗ ⲁⲛ. (aiōn )
32 Kule Dameski, mkuu wa mkoa chini ya mfalme Areta alikuwa akiulinda mji wa Dameski ili kunikamata.
ⲗ̅ⲃ̅ϫⲉ ϩⲣⲁⲓ̈ ϩⲛ̅ⲇⲁⲙⲁⲥⲕⲟⲥ ⲁⲡϩⲉⲑⲛⲁⲣⲭⲏⲥ ⲛ̅ⲧⲉⲁⲣⲉⲧⲁ ⲡⲣ̅ⲣⲟ ϩⲁⲣⲉϩ ⲉⲧⲡⲟⲗⲓⲥ ⲛ̅ⲇⲁⲙⲁⲥⲕⲟⲥ ⲉϭⲟⲡⲧ.
33 Lakini niliwekwa kikapuni, kupitia dirishani katika ukuta, na nikanusurika kutoka mikononi mwake.
ⲗ̅ⲅ̅ⲁⲩⲱ ⲉⲃⲟⲗ ϩⲓⲧⲛ̅ⲟⲩϣⲟⲩϣⲧ̅ ϩⲛ̅ⲟⲩⲥⲁⲣⲅⲁⲛⲏ. ⲁⲩⲭⲁⲗⲁ ⲙ̅ⲙⲟⲓ̈ ⲡⲃⲟⲗ ⲙ̅ⲡⲥⲟⲃⲧ̅. ⲁⲓ̈ⲣ̅ⲃⲟⲗ ⲉⲛⲉϥϭⲓϫ.