< 2 Wakorintho 1 >
1 Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu, kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, na kwa waumini wote walioko katika mkoa wote wa Akaya.
IshvarasyechChayA yIshukhrIShTasya preritaH paulastimathirbhrAtA cha dvAvetau karinthanagarasthAyai IshvarIyasamitaya AkhAyAdeshasthebhyaH sarvvebhyaH pavitralokebhyashcha patraM likhataH|
2 Neema na iwe kwenu na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.
asmAkaM tAtasyeshvarasya prabhoryIshukhrIShTasya chAnugrahaH shAntishcha yuShmAsu varttatAM|
3 Na asifiwe Mungu na Baba wa Bwana Yesu Kristo. Yeye ni Baba wa rehema na Mungu wa faraja yote.
kR^ipAluH pitA sarvvasAntvanAkArIshvarashcha yo. asmatprabhoryIshukhrIShTasya tAta IshvaraH sa dhanyo bhavatu|
4 Mungu hutufariji sisi katika mateso yetu yote, ili kwamba tuweze kuwafariji wale walio katika mateso. Tunawafariji wengine kwa faraja ileile ambayo Mungu alitumia kutufariji sisi.
yato vayam IshvarAt sAntvanAM prApya tayA sAntvanayA yat sarvvavidhakliShTAn lokAn sAntvayituM shaknuyAma tadarthaM so. asmAkaM sarvvakleshasamaye. asmAn sAntvayati|
5 Kwa kuwa kama vile mateso ya Kristo huongezeka kwa ajili yetu, vile vile faraja yetu huongezeka kupitia Kristo.
yataH khrIShTasya kleshA yadvad bAhulyenAsmAsu varttante tadvad vayaM khrIShTena bahusAntvanADhyA api bhavAmaH|
6 Lakini kama tunataabishwa, ni kwa ajili ya faraja yenu na wokovu wenu. Na kama tunafarijiwa, ni kwa ajili ya faraja yenu. Faraja yenu inafanya kazi kikamilifu mnaposhiriki mateso kwa uvumilivu kama sisi pia tunavyoteseka.
vayaM yadi klishyAmahe tarhi yuShmAkaM sAntvanAparitrANayoH kR^ite klishyAmahe yato. asmAbhi ryAdR^ishAni duHkhAni sahyante yuShmAkaM tAdR^ishaduHkhAnAM sahanena tau sAdhayiShyete ityasmin yuShmAnadhi mama dR^iDhA pratyAshA bhavati|
7 Na ujasiri wetu juu yenu ni thabiti. Tunajua kwamba kama vile ambavyo mnashiriki mateso, vile vile mnashiriki faraja.
yadi vA vayaM sAntvanAM labhAmahe tarhi yuShmAkaM sAntvanAparitrANayoH kR^ite tAmapi labhAmahe| yato yUyaM yAdR^ig duHkhAnAM bhAgino. abhavata tAdR^ik sAntvanAyA api bhAgino bhaviShyatheti vayaM jAnImaH|
8 Kwa kuwa hatutaki ninyi muwe wajinga, ndugu, kuhusu matatizo tuliyokuwa nayo huko Asia. Tulionewa zaidi ya vile tuwezavyo kubeba, kana kwamba hatukuwa hata na tumaini la kuishi tena.
he bhrAtaraH, AshiyAdeshe yaH klesho. asmAn AkrAmyat taM yUyaM yad anavagatAstiShThata tanmayA bhadraM na manyate| tenAtishaktikleshena vayamatIva pIDitAstasmAt jIvanarakShaNe nirupAyA jAtAshcha,
9 Kweli, tulikuwa na hukumu ya kifo juu yetu. Lakini hiyo ilikuwa ni kutufanya sisi tusiweke tumaini juu yetu wenyewe, badala yake tuweke tumaini katika Mungu, afufuaye wafu.
ato vayaM sveShu na vishvasya mR^italokAnAm utthApayitarIshvare yad vishvAsaM kurmmastadartham asmAbhiH prANadaNDo bhoktavya iti svamanasi nishchitaM|
10 Alituokoa sisi kutoka hayo maafa ya mauti, na atatuokoa tena. Tumeweka ujasiri wetu katika yeye ya kwamba atatuokoa tena.
etAdR^ishabhaya NkarAt mR^ityo ryo. asmAn atrAyatedAnImapi trAyate sa itaH paramapyasmAn trAsyate. asmAkam etAdR^ishI pratyAshA vidyate|
11 Atafanya hivi kama vile ninyi pia mtusaidiavyo kwa maombi yenu. Hivyo wengi watatoa shukurani kwa niaba yetu kwa ajili ya upendeleo wa neema tuliyopewa sisi kupitia maombi ya wengi.
etadarthamasmatkR^ite prArthanayA vayaM yuShmAbhirupakarttavyAstathA kR^ite bahubhi ryAchito yo. anugraho. asmAsu varttiShyate tatkR^ite bahubhirIshvarasya dhanyavAdo. api kAriShyate|
12 Tunajivunia hili: ushuhuda wa dhamiri yetu. Kwa kuwa ni katika nia safi na usafi wa Mungu kwamba tulienenda wenyewe katika dunia. Tumefanya hivi hasa na ninyi, na sio katika hekima ya ulimwengu, lakini badala yake ni katika neema ya Mungu.
apara ncha saMsAramadhye visheShato yuShmanmadhye vayaM sAMsArikyA dhiyA nahi kintvIshvarasyAnugraheNAkuTilatAm IshvarIyasAralya nchAcharitavanto. atrAsmAkaM mano yat pramANaM dadAti tena vayaM shlAghAmahe|
13 Hatuwaandikii chochote ambacho hamwezi kukisoma au kuelewa. Ninaujasiri
yuShmAbhi ryad yat paThyate gR^ihyate cha tadanyat kimapi yuShmabhyam asmAbhi rna likhyate tachchAntaM yAvad yuShmAbhi rgrahIShyata ityasmAkam AshA|
14 kwamba kwa sehemu mumekwisha kutuelewa. Na ninaujasiri kwamba katika siku ya Bwana Yesu tutakuwa sababu yenu kwa ajili ya kiburi chenu, kama vile mtakavyokuwa kwetu.
yUyamitaH pUrvvamapyasmAn aMshato gR^ihItavantaH, yataH prabho ryIshukhrIShTasya dine yadvad yuShmAsvasmAkaM shlAghA tadvad asmAsu yuShmAkamapi shlAghA bhaviShyati|
15 Kwa sababu nilikuwa na ujasiri kuhusu hili, nilitaka kuja kwenu kwanza, ili kwamba muweze kupokea faida ya kutembelewa mara mbili.
aparaM yUyaM yad dvitIyaM varaM labhadhve tadarthamitaH pUrvvaM tayA pratyAshayA yuShmatsamIpaM gamiShyAmi
16 Nilikuwa napanga kuwatembelea wakati nikielekea Makedonia. Tena nilitaka kuwatembelea tena wakati nikirudi kutoka Makedonia, na kisha ninyi kunituma mimi wakati nikielekea Uyahudi.
yuShmaddeshena mAkidaniyAdeshaM vrajitvA punastasmAt mAkidaniyAdeshAt yuShmatsamIpam etya yuShmAbhi ryihUdAdeshaM preShayiShye cheti mama vA nChAsIt|
17 Nilipokuwa nafikiria namna hii, je, nilikuwa nasitasita? Je ninapanga mambo kulingana na viwango vya kibinadamu, ili kwamba niseme “Ndiyo, ndiyo” na “Hapana, hapana” kwa wakati mmoja?
etAdR^ishI mantraNA mayA kiM chA nchalyena kR^itA? yad yad ahaM mantraye tat kiM viShayilokaiva mantrayANa Adau svIkR^itya pashchAd asvIkurvve?
18 Lakini kama vile Mungu alivyo mwaminifu, hatusemi vyote “Ndiyo” na “Hapana.”
yuShmAn prati mayA kathitAni vAkyAnyagre svIkR^itAni sheShe. asvIkR^itAni nAbhavan eteneshvarasya vishvastatA prakAshate|
19 Kwa kuwa mwana wa Mungu, Yesu Kristo, ambaye Silvano, Timotheo na mimi tulimtangaza miongoni mwenu, siyo “Ndiyo” na “Hapana.” Badala yake, yeye wakati wote ni “Ndiyo.”
mayA silvAnena timathinA cheshvarasya putro yo yIshukhrIShTo yuShmanmadhye ghoShitaH sa tena svIkR^itaH punarasvIkR^itashcha tannahi kintu sa tasya svIkArasvarUpaeva|
20 Kwa kuwa ahadi zote za Mungu ni “Ndiyo” katika yeye. Hivyo pia kupitia yeye tunasema “Amina” kwa utukufu wa Mungu.
Ishvarasya mahimA yad asmAbhiH prakAsheta tadartham IshvareNa yad yat pratij nAtaM tatsarvvaM khrIShTena svIkR^itaM satyIbhUta ncha|
21 Sasa ni Mungu ambaye hututhibitisha sisi pamoja nanyi katika Kristo, na alitutuma sisi.
yuShmAn asmAMshchAbhiShichya yaH khrIShTe sthAsnUn karoti sa Ishvara eva|
22 Aliweka muhuri juu yetu na alitupa Roho katika mioyo yetu kama dhamana ya kile ambacho angetupatia baadaye.
sa chAsmAn mudrA NkitAn akArShIt satyA NkArasya paNakharUpam AtmAnaM asmAkam antaHkaraNeShu nirakShipachcha|
23 Badala yake, namsihi Mungu kunishuhudia mimi kwamba sababu iliyonifanya nisije Korintho ni kwamba nisiwalemee ninyi.
aparaM yuShmAsu karuNAM kurvvan aham etAvatkAlaM yAvat karinthanagaraM na gatavAn iti satyametasmin IshvaraM sAkShiNaM kR^itvA mayA svaprANAnAM shapathaH kriyate|
24 Hii sio kwa sababu tunajaribu kudhibiti jinsi imani yenu inavyotakiwa kuwa. Badala yake, tunafanya pamoja nanyi kwa ajili ya furaha yenu, kama mnavyosimama katika imani yenu.
vayaM yuShmAkaM vishvAsasya niyantAro na bhavAmaH kintu yuShmAkam Anandasya sahAyA bhavAmaH, yasmAd vishvAse yuShmAkaM sthiti rbhavati|