< 2 Nyakati 8 >
1 Ikawa karibu ya mwisho wa miaka ishirini, kipindi ambacho Selemani alikuwa ameijenga nyumba ya Yahwe na ya kwake mwenye,
Le roi Salomon avait mis vingt ans à construire ces deux édifices: le temple du Seigneur et son propre palais.
2 kwamba Selemani akaiajenga miji ambayo Hiramu alikuwa amempa, na ndani yake akawaweka watu wa Israeli.
Et il rebâtit les villes qu'Hiram lui avait données, et il y établit des fils d'Israël.
3 Selemani akauavamia Hamathzoba, akaushinda.
Puis, il se rendit à Bésoba, qu'il entoura de remparts.
4 Akaijenga Tadmori katika nyika, na miji yote ya hazina, ambayo aliijenga katika Hamathi.
Et il bâtit Thœdnior (Palmyre) dans le désert, ainsi que toutes les places fortes du pays d'Emath.
5 Pia akaujenga Beth-horoni wa juu, na Beth-horoni wa chini, miji iliyozungushiwa kwa ukuta, malango, na makomeo.
Et il fit de Béthoron-la-Haute et de Béthoron-la-Basse deux forteresses, avec murailles, portes et verrous.
6 Akaujenga Baalathi na miji yote ya hazina aliyoimiliki, na miji yote kwa ajili ya magari yake na miji kwa ajili ya wapanda farasi wake, na chochote alichotamani kujenga kwa ajili ya starehe zake katika Yerusalemu, katika Lebanoni, na katika nchi zote zilizokuwa chini ya utawala wake.
Et il bâtit Balaath, ainsi que toutes les places fortes qui lui appartenaient, toutes les villes des chars, les villes des cavaliers, enfin tout ce qu'il lui plut de bâtir tant à Jérusalem que dans le Liban, et dans tout son royaume.
7 Kuhusu watu wengine wote ambao walikuwa wamesalia wa Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi, Wayebusi, ambao hawakuwa wa Israeli,
Tout ce qui restait de l'Hettéen, de l'Amorrhéen, de l'Evéen, du Jébuséen; tout ce qui n'était point d'Israël,
8 watoto wao ambao waliachwa baada yao katika nchi, ambaoa watu wa Israeli hawakuwaangamiza—Selemani akawafanyisha kazi kwa nguvu, ndivyo walivyo hata leo.
Mais qui descendait de ceux que les fils d'Israël n'avaient point exterminés, et qui étaient restés avec eux en la terre promise, furent obligés de payer à Salomon un tribut qu'ils paient encore de nos jours.
9 Vile vile, Selemani hakuwafanyisha kazi kwa nguvu watu wa Israeli. Badala yake, wakawa wanajeshsi wake, maakida wake, wakuu wake, na maakida wa magari ya majeshi yake na wapanda farasi wake.
Et Salomon ne permit point qu'il y eût en son royaume de serviteurs nés des fils d'Israël; car ceux-ci étaient des guerriers, des chefs, des vaillants, qui commandaient les chars et les cavaliers.
10 Pia hawa walikuwa wakuu wa wakuu wakisimamia wasimamizi waliokuwa wa mfalme Selemani, walikuwa 250, waliowasimamia watu walioifanya kazi.
Il y en avait à la tête des intendants du roi Salomon; on en comptait deux cent cinquante dirigeant les travaux du peuple.
11 Selemani akamleta binti Farao nje ya mji wa Daudi kwenye nyumba aaliyokuwa amemjengea, kwa maana alisema, “Mke wangu lazima asiishi kataika nyumba ya Daudi mfalme wa Israeli, kwa sababu kila linapokuja sanduku la Yahwe ni takatifu”.
Et Salomon conduisit la fille du Pharaon de la ville de David, au palais qu'il avait bâti pour elle, car il avait dit: Ma femme ne doit pas demeurer en la ville de David, roi d'Israël, parce qu'une ville où est entrée l'arche du Seigneur est sainte.
12 Kisha Selemani akatoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu yake ambayo alikuwa ametengeza mbele ya ukumbi.
Alors, Salomon offrit des holocaustes au Seigneur sur l'autel qu'il avait élevé au Seigneur devant le temple,
13 Akatoa sadaka kama ilivyohitaka katika ratiba ya kila siku; akazitoa, kwa kufuata maelekezo yaliyokuwa katika amari ya Musa, katika siku za Sabato, miezi mipya, na katika siku zilizopangwa mara tatu kila mwaka: Sikukuu ya mikate isiyochachwa, sikukuu ya majuma, na sikuku ya vibanda.
Selon la règle de chaque jour; il les offrit conformément aux commandements de Moïse sur les sabbats, les lunes et les fêtes des trois époques de l'année: fête des azymes, fête des semaines, fête des tabernacles.
14 Katika kuyatunza maagizo ya baba yake Daudi, Selemani akayapanga makundi ya makuhani kwenye kazi yao, na Walawi kwenye nafasi zao, ili kumsisfu Mungu na kuhudumu mbele za makuhani, kama ilivyotakiwa katika ratiba ya kila siku. Pia akawateua walinda lango kwa zamu zao kwa kila lango, kwa maana Daudi, mtu wa Mungu, alikuwa ameagiza hivyo pia.
Ensuite, conformément à l'ordre établi par David, son père, il régla les fonctions des prêtres et celles des lévites, qui devaient servir et chanter journellement devant les prêtres; il désigna aussi les portiers; car, ainsi l'avait prescrit David, homme de Dieu.
15 Watu hawa hawakupotea kutoka kwenye amri ya mfalme kwa makuhani na Walawi kuhusu jambo lolote, au kuhusu vyumba vya hazina.
Et on ne s'écarta point des commandements du roi, concernant les prêtres et les lévites, en aucune chose, notamment en ce qui regardait les trésors.
16 Kazi yote aliyoagizwa na Selemani ikakamilika, kutoka siku msingi wa nyumba ya Yahwe ulipowekwa hadi ilipokamilika. Nyumba ya Yahwe ikamalizika.
Tous les travaux avaient été préparés à partir du jour où Salomon avait jeté les fondations du temple, jusqu'à celui où la construction fut achevée.
17 Kisha Selemani akaenda Esion geberi, na Elothi, juu ya pwani katika nchi ya Edomu.
Alors, Salomon alla à Asiongaber et à Ailath, en la terre d'Idumée, près du rivage de la mer.
18 Hiramu akatuma meli zake kupitia watumishi wake ambao walikuwa wana maji wenye uzoefu. Wakasafiri na Selemani na watumishi wa Semani hadi Ofiri. Wakachukua kutoka huko talanta 450 za dhahabu ambazo walimletea Selemani.
Là, Hiram lui envoya des vaisseaux et des serviteurs habitués à la mer; ceux-ci naviguèrent, avec les serviteurs de Salomon, jusqu'à Ophir; ils rapportèrent de là trois cent cinquante talents d'or, et ils revinrent auprès du roi Salomon.