< 2 Nyakati 6 >
1 Kisha Selemani akasema, “Yahwe alisema kwamba ataishi katika giza nene,
Then said Solomon, “The Lord said that he would dwell in the thick darkness.
2 lakini nimekujengea makao makuu, sehemu kwa ajili yako ya kuishi milele.”
And I have indeed built a dwelling-house for thee, and have settled a place for thy abode for ever.”
3 Kisha mfaalme akageuka nyuma na kuwabariki kusanyiko lote la Israeli, wakati kusanyiko lote la Israeli walikuwa wamesimama.
And the king turned his face, and blessed the whole congregation of Israel, and all the congregation of Israel was standing.
4 Akasema, “Yahwe, Mungu wa Israeli, usifiwe, uliyesema na Daudi baba yangu, na ametimiza kwa mikono yake mwenyewe, akisema.
And he said, Blessed be the Lord, the God of Israel, who spoke with his mouth unto David my father, and hath with his hands fulfilled it, when he said,
5 'Tangu siku nilipowaleta watu wanagu nje ya nchi ya Misiri, sikuchaagua mji wowote nje ya makabaila yote ya Israeli ambamo nyumba ingejengwa, ili jina lanagu liwe humo. Wala sikuchagua mtu yeyote kuwa mfalme juu ya watu wangu Israeli.
Since the day that I brought forth my people out of the land of Egypt, I did not make choice of any city out of all the tribes of Israel to build a house, that my name might be therein; nor did I make choice of any man to be a ruler over my people of Israel;
6 Aidha, nimechagua Yeruselemu, ili kwamba jina langu liwe humo, na nimemchagua Daudi kuwa juu ya watu wanagu Israeli. '
But I have made choice of Jerusalem, that my name might be there; and I have made choice of David to be over my people Israel,
7 Sasa ilikuwa ndani ya moyo wa Daudi baba yangu, kujenga nyumba kwa ajili ya jina la Yahwe, Mungu wa Israeli.
And it was in the heart of David my father to build a house for the name of the Lord the God of Israel.
8 Lakini Yahwe alisema kwa Daudi Baba yanagu. 'Kwmba ilikuwa ndani ya moyo wako kujenga nyumba kwa ajili ya jina langu, ulifanya vizuri kwa hili kuliweka moyono mwako.
But the Lord said unto David my father, Whereas it was in thy heart to build a house unto my name, thou didst well in that it was in thy heart:
9 Aidha, hutaijenga ile nyumba, badala yake, mwanao, mmoja atakayetoka kwenye viuno vyako, ataijenga nyumba kwa ajili ya jina langu.'
Nevertheless thou shalt not thyself build the house; but thy son that shall come forth out of thy loins, he shall build the house unto my name.
10 Yahwe ameyatimiza maneno aliyokuwa amesema, kwa maana nimeiinua sehemu ya Daudi baba yangu, na ninkaa juu ya kiti cha enzi cha Israeli, kama alivyoahidi Yahwe. Nimeijenga nyumba kwa ajii ya jina la Yahwe, Mungu wa Israeli.
And the Lord hath fulfilled his word that he hath spoken; and I am risen up in the stead of David my father, and I sit on the throne of Israel, as the Lord hath spoken, and I have built the house unto the name of the Lord the God of Israel.
11 Nimeliweka humo sanduku, amabamo kuna agano la Yahwe, alilofanya na watu wa Israeli.”
And I have placed there the ark, wherein is the covenant of the Lord which he hath made with the children of Israel.
12 Selemani akasimama mbele ya madhabahu ya Yahwe mbele za kusanyiko lote la Israeli, na akanyosha mikono yake.
And he now placed himself before the altar of the Lord in the presence of all the congregation of Israel, and spread forth his hands;
13 Kwa mana alikuwa ametengeneza jukwaa la shaba, lenye urefu wa mikono mitano, upana wa mikono mitano, urefu wake kwenda juu mikono mitatu. Alikuwa ameliweka katika ya uwanja. Akasimama juu yake na kupiga magoti mbele ya kusanyiko la Israeli, kisha akanyosha mikono yake kuzielekea mbingu.
For Solomon had made a laver of copper, and had placed it in the midst of the out-court, five cubits being its length, five cubits its breadth, and three cubits its height; and he placed himself upon it, and kneeled down upon his knees in the presence of all the congregation of Israel, and spread forth his hands toward heaven;
14 Akasema, “Yahwe, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe katika mbingu, au juu ya dunia, ambaye anatunza agano na upendo imara na watumishi wako ambao hutembea mbele zako kwa moyo wao wote;
And he said, O Lord God of Israel, there is no god like thee in the heavens, or on the earth, thou who keepest the covenant, and the kindness for thy servants that walk before thee with all their heart;
15 wewe uliyetimtimizia Daudi baba yanagu, uliyokuwa umemwahidi. Ndiyo, ulisema kwa kinywa chako na umetimiza kwa mkono wako, kama ilivyo leo.
Who has kept for thy servant David my father that which thou hadst promised him; and thou spokest with thy mouth, and hast fulfilled it with thy hand, as it is this day.
16 Sasa, Yahwe, Mungu wa Israeli, tunza ahadi uliyoahidi kwa mtumishi wako Daudi baba yangu, uliposema, 'Hautashindwa kupata mtu mbele yangu wa kukaa juu ya kiti cha enzi cha Israeli, ikiwa tu uzao wako ni waangalifu kutembea katika sheria yangu, kama wewe ulivyotembea mbele zangu.
And now, O Lord, God of Israel, keep for thy servant David my father that which thou hast spoken concerning him, saying, There shall never fail thee a man in my sight who sitteth on the throne of Israel, if thy children but take heed to their way to walk in my law, as thou hast walked before me.
17 Sasa, Mungu wa Israeli, ninaomba kwamba ahadi uliyofanya kwa mtumishi wako Daudi itakuwa kweli.
And now, O Lord, the God of Israel, let thy word be verified, which thou hast spoken unto thy servant, unto David.
18 Lakini kweli Mungu ataishi na wanadamu juu ya dunia? Angalia, dunia yoye na mbugu yenyewe haviwezi kukubeba -sembuse na hekalu hili nililojenga!
For, in truth, will God then dwell with men on the earth? behold, the heavens and the heavens of heavens cannot contain thee: how much less then this house that I have built!
19 Nakusihi yaheshimu maombi haya ya mtumishi wako na ombi lake. Yahwe Mungu wangu; sikia kilio na amaombi ambayo mtumishi wako anaomba mbele zako.
Yet wilt thou turn thy regard unto the prayer of thy servant, and to his supplication, O Lord my God, to listen unto the entreaty and the prayer which thy servant prayeth before thee:
20 Fumbua macho yako kuelekea hekaalu hili usiku na mchana, sehemu aambaayo uliahidi kuliweka jina lako. Nakuomba usikie maombi atakayoomba mtumishi wako kuelekea sehemu hii.
That thy eyes may be open toward this house day and night, toward the place of which thou hast said that thou wouldst put thy name there; that thou mayest listen unto the prayer which thy servant will pray at this place.
21 Hivyo sikia maombi ya mtumishi na ya watu wako Israeli tunapoomba kuelekea sehemu hii. Ndiyo, sikia kutoka mahali unapoishi, kutoka mbinguni; na unaposikia, samehe.
And listen thou to the supplications of thy servant, and of thy people Israel, which they will pray at this place: and oh, do thou hear from thy dwelling-place, from heaven; and hear, and forgive.
22 Kama mtu atamtenda dhambi jirani yake na ikampasa kuapa kiapo, na ikiwa atakuja na kuapa kiapo mbele ya madhabahu yako katika nyumba hii,
If any man trespass against his neighbor, and an oath be laid upon him to cause him to swear, and the oath come before thy altar in this house:
23 basi sikia kutoka mbinguni na kutend na ukawahukumu watumishi wako, ukamlipizie mwovu, ili kuyaleta matendo yake juu ya kichwa chake. Ukamtangaze mwenye haki kuwa hana hatia, ili kumlipa thawabu kwa ajili ya uaminifu wake.
Then do thou hear from heaven, and act, and judge thy servants, by requiting the wicked, to bring his way upon his own head; and by justifying the righteous, to give him according to his righteousness.
24 Watu wako watakaposhindwa na adui kwa sababu wamekutenda dhambi, kama watageuka nyuma kwako, wakilikili jina lako, wakisali na kuomba msamaha mbele zako hekaluni—
And if thy people Israel be struck down before the enemy, because they have sinned against thee, and they return and confess thy name, and pray, and make supplication before thee in this house:
25 basi tafadhali sikia mbinguni na usamehe dhambi za watu wako Isaraeli; uwarudishe katika nchi uliyoitoa kwa ajili yao na baba zao.
Then do thou hear from heaven, and forgive the sin of thy people Israel, and cause them to return unto the land which thou hast given to them and to their fathers.
26 Wakati mbingu zimefungwa na hakuna mvua kwa sababu watu wamekutenda dhambi—ikiwa wataomba kuelekea sehemu hii, wakilikili jina lako, na kuziacha dhambi zao utakapokuwa umewaadhibu—
When the heavens be shut up, and there he no rain, because they have sinned against thee, and they pray toward this place, and confess thy name, and turn from their sin, because thou hast afflicted them:
27 basi sikia mbinguni na usamehe dhambi za watumishi wako na watu wako Israeli, utakapowaelekeza kwenye njia njema iwapasayo kutembea. Tuma mvua juu ya nchi yako, ambayo umewapa watu wako kama urithi.
Then do thou hear in heaven, and forgive the sin of thy servants, and of thy people Israel; for thou wilt direct them unto the good way, wherein they should walk; and give then rain upon thy land, which thou hast given unto thy people for an inheritance.
28 Kama kuna njaa katika nchi, au kama kuna ugonjwa, tauni au ukungu, nzige au viwavijeshi, au kama adui wake wameyavamia malango ya mji katika nchi yao, au kwamba kuna pigo lolote au ugonjwa—
If there be famine in the land, if there be pestilence, blasting, or mildew, if there be locusts, or caterpillars; if their enemies besiege them in their land, in their gates at whatsoever plague, and at whatsoever sickness;
29 na ikiwa sala na maombi yamefanywa na mtu au watu wako wote Israel—kila mmoja akilijua pigo na huzuni katika moyo wake akinyosha mikono yake kuelekea hekalu hili.
What prayer and what supplication soever be made by any man, or by all thy people Israel, when they shall be conscious every man of his plague and his pain, and he then spread forth his hands toward this house:
30 Basi sikiliza mbinguni, sehemu ambayo unaishi; samehe, na umlipe kila mtu kwa njia zake zote; uhaujua moyo wake, kwa sababu wewe na ni wewe pekee unaijua mioyo ya wanadamu.
Then do thou hear from heaven the place of thy dwelling, and forgive, and give to every man in accordance with all his ways, as thou mayest know his heart; for thou, thyself alone, knowest the heart of the children of men;
31 Fanya hivyo ili kwamba wakuogope wewe, ili waweze kutembea katika katika njia zako siku zote ambazo wataishi katika nchi uliyowapa baba zetu.
In order that they may fear thee, to walk in thy ways, all the days that they live on the face of the land which thou hast given unto our fathers.
32 Kwa mgeni ambaye siyo sehemu ya watu wako Israeli, lakini ambaye- kwa sababu ya ukuu wa jina lako, mkono wako wenye nguvu, na mkono wako ulionyoshwa- akija na kuomba kuelekea sehemu nyumba hii,
But also to the stranger, who is not of thy people Israel, but cometh out of a far-off country for the sake of thy great name, and of thy mighty hand, and of thy outstretched arm, — if they come and pray in this house, —
33 basi sikiliza mbinguni, sehemu ambayo unaishi, na fanya yote ambayo mgeni atakuomba, ili kwamba watu wote wa dunia walijue jina lako na kukuogopa wewe, kama wafanyavyo watu wako Israeli, na kwamba waweze kujua kwamba nyumba hii niliyoijenga inaitwa kwa jina lako.
Mayest thou likewise listen from heaven, from the place of thy dwelling, and do according to all that the stranger will call on thee for: in order that all people of the earth may know thy name, both to fear thee, as do thy people Israel, and to understand that this house, which I have built, is called by thy name.
34 Ikiwa kwamba watu wako wakaenda nje kupigana dhidi ya adui zao, kwa njia yoyote amabayo unaweza kuwatuma, na ikiwa kwamba wakaomba kwako kuelekea mji huu ambao umeuchagua, na kuelekea nyumba ambayo nimeijenga kwa ajili ya jina lako.
If thy people go out to battle against their enemies on the way on which thou mayest send them, and they do pray unto thee in the direction of this city which thou hast chosen, and of the house that I have built unto thy name:
35 Basi sikiliza maombi yao mbinguni, ombi lao, na uwasaidie.
Then hear thou from heaven their prayer and their supplication, and procure them justice.
36 Kama wametenda dhambi dhidi yako—kwa kuwa hakuna asiye tenda dhambi—na ikiwa una hasira nao na kuwakabidhi kwa adui zao, ili kwamba adui wakawabeba na kuwachukua kama mateka kwa ajili ya nchi zao, iwe mbali au karibu.
If they sin against thee—for there is no man that may not sin, —and thou be angry with them, and give them up before the enemy, so that their captors carry them away captive unto a land far off or near;
37 Kisha wakatambua kuwa wako katika nchi ambako wamewekwa utumwani, na ikiwa watatubu na kutafuta msaada kwako katika utumwa wao. ikiwa watasema, 'Tumetenda kinyume na kutenda dhambi. Tumetenda kwa uovu,'
And if they then take it to their heart in the land whither they have been carried captive, and repent and make supplication unto thee in the land of their captivity, saying, We have sinned, we have committed iniquity, and have acted wickedly;
38 ikiwa watarudi kwako kwa mioyo yao yote na kwa nia yao yote katika nchi ya utumwa wao, ambako walichuliwa kama mateka, na ikiwa wataomba kukabili nchi yao, uliyowapa babu zao, na kukabili mji ambao uliuchagua na kukabili nyumba ambayo niliijenga kwa ajili ya jina lako.
And they return unto thee with all their heart and with all their soul in the land of their captivity, whither they have been carried captive, and they pray in the direction of their land, which thou hast given unto their fathers, and of the city which thou hast chosen, and toward the house which I have built unto thy name:
39 Basi sika kutoka mbinguni, mahali unapoishi, sikia kuomba kwao na maombi na wayaombayo, na uwasaidie shida zao. Wasamehe watu wako, ambao wamekutenda dhambi.
Then hear thou from heaven, from the place of thy dwelling, their prayer and their supplications, and procure them justice, and forgive thy people for what they have sinned against thee.
40 Sasa, Mungu wangu, ninakusihi, uyafungue macho yako, na masikio yako yasiskie maombi yatakayofanywa katika sehemu hii.
Now, my God, let I beseech thee, thy eyes be open, and thy ears be attentive unto the prayer on this place.
41 Sasa basi, amka, Yahwe Mungu, kwenye mahali pako pa kupumzikia, Wewe na sanduku la nguvu zako. Makuhani wako, Yahwe Mungu, wavikwe wokovu, na watakatifu wako wafurahi katika wema.
And now arise, O Lord God, unto thy resting-place, thou, and the ark of thy strength: let thy priests, O Lord God, clothe themselves with salvation, and let thy pious servants rejoice in happiness.
42 Yahwe Mungu, usiugeuze nyuma uso wa masihi wako. Yakumbuke matendo yako katika agano lako la ufalme kwa ajili ya Daudi, mtumishi wako.
O Lord God, turn not away the face of thy anointed: remember the pious deeds of David thy servant.