< 2 Nyakati 5 >

1 Wakati ilipomalizika kazi aliyofanya Selemani kwa ajili ya Yahwe, Selemani akapeleka vitu ndani, ambavyo Daudi, baba yake, aliviweka wakifu kwa kusudi hilo, pamoja na zile fedha, dhahabu, na vyombo vyote akavileta ndani ya hazina ya nyumba ya Mungu.
And all the work that Solomon made for the house of YHWH is finished, and Solomon brings in the sanctified things of his father David, and the silver, and the gold, and all the vessels he has put among the treasures of the house of God.
2 Kisha Selemanai akawakusanya wazee wa Israeli, wakuu wa makabila yote, na viongozi wa familia za watu wa Israeli, katika Yerusalemu, ili walilete sanduku la agano la Yahwe kutoka mji wa Daudi, ambao ni Sayuni.
Then Solomon assembles the elderly of Israel, and all the heads of the tribes, princes of the fathers of the sons of Israel, to Jerusalem, to bring up the Ark of the Covenant of YHWH from the City of David—it [is] Zion.
3 Wanaume wote wa Israeli wakakusanyika mbele za mfalme katika sikukuu, ambayo ilikuwa katika mwezi wa saba.
And all the men of Israel are assembled to the king in the celebration—it [is] the seventh month;
4 Wazee wote wa Israeli wakaja, na Walawi wakalichukua sanduku.
and all [the] elderly of Israel come in, and the Levites lift up the Ark,
5 Wakalileta sanduku, hema ya kukutania, na vyombo vitakatifu vyote ambavyo vilikuwa ndani ya hema. Makuhani waliokuwa wa kabila la Lawi wakavileta vtu hivyo.
and they bring up the Ark, and the Tent of Meeting, and all the holy vessels that [are] in the tent; the priests, the Levites, have brought them up;
6 Mfalme Selemanai na kusanyiko lote la Israeli wakaja pamoja, mbele ya sanduku, wakitoa sadaka za kondoo na maksai ambao hawakuweza kuhesabika.
and King Solomon and all the congregation of Israel who are convened to him before the Ark are sacrificing sheep and oxen that are not counted nor numbered from multitude.
7 Makuhani wakalileta sanduku la anago la Yahwe ndani mahali pake, katika chumba cha ndani cha nyumba, kwenye patakatifu pa patakatifu, chini ya mabawa ya makerubi.
And the priests bring in the Ark of the Covenant of YHWH to its place, to the oracle of the house, to the Holy of Holies, to the place of the wings of the cherubim;
8 Kwa kuwa makerubi walitandaza mabawa yao juu ya mahali pa sanduku, na walilifunika sanduku na na miti yake ya kulibebea.
and the cherubim are spreading out wings over the place of the Ark, and the cherubim cover over the Ark, and over its poles, from above;
9 Miti ilikuwa mirefu sana kwamba ncha zake zlionekana kutoka ile sehemu takatifu mbele ya chumba cha andani, lakini hazikuweza kuonekana kutoka nje. Zipo hapo hadi leo.
and they lengthen the poles, and the heads of the poles are seen out of the Ark on the front of the oracle, and they are not seen outside; and it is there to this day.
10 Hapakuwa na kitu katika sanaduku isipokuwa zile meza mbili ambazo Musa aliziweka humo huko Horebu, wakati Mungu alipofanya agano na watu wa Israeli, walipotoka nje ya Misri.
There is nothing in the Ark but the two tablets that Moses gave in Horeb, where YHWH covenanted with the sons of Israel, in their going out from Egypt.
11 Ilikuwa makuhani walipotoka nje ya sehemu takatifu. Makuhanai wote wliokuwepo wakajiweka wakifu wenyewe kwa Yahwe, bila kujiamuru wenyewe kulingana na sehemu zao.
And it comes to pass, in the going out of the priests from the holy place—for all the priests who are present have sanctified themselves, there is none to watch by divisions,
12 Pia makuhani waliokuwa waimbaji, wote kwa ujumla wao, pamoja na Asafu, Hemani, Yeduthuni, na wana wao na ndugu zao, wakiwa wamevalia kitani safi na wakipiga matoazi, vinanda, na vinubi, wakaasimama upande wa mashariki wa mwisho wa madhabahu. Pamoja nao palikuwa na makuhuni 120 wakipuliza tarumbeta.
and the Levites, the singers, to all of them, to Asaph, to Heman, to Jeduthun, and to their sons, and to their brothers, clothed in white linen, with cymbals, and with psalteries, and harps, are standing on the east of the altar, and with them one hundred and twenty priests blowing with trumpets—
13 Ikawa kwamba wapuruza tarumbeta na waimbaji wakafanya mziki pamoja, wakifanya sauti moja isikike kwa ajili ya kumsifu na kumshukuru Yahwe. Walipaza sauti zao kwa tarumbeta, toazi na vyombo vingine, na wakamsifu Yahwe. Wakaimba, “Kwa maana Yeye ni mwema, kwa kuwa uaminifu wa agano lake wadumu milele.” Kisha nyumba, ile nyumba ya Yahwe, ikajawa na wingu.
indeed, it comes to pass, trumpeters and singers [are] as one, to sound [with] one voice—to praise and to give thanks to YHWH, and at the lifting up of the sound with trumpets, and with cymbals, and with instruments of song, and at giving praise to YHWH, [saying], “For [He is] good, for His kindness [is] for all time,” that the house is filled with a cloud—the house of YHWH,
14 Makuhani hawakuweza kusimama ili wahudumu kwa sababu ya lile wingu, kwa maana utukufu wa Yahwe uliijaza nyumba yake.
and the priests have not been able to stand to minister from the presence of the cloud, for the glory of YHWH has filled the house of God.

< 2 Nyakati 5 >