< 2 Nyakati 33 >

1 Manase alikuwa na umri wa miaka kumi na mbili alipoanza kutawala, alitawala miaka hamsini na tano katika Yerusalemu.
Manasseh was 12 years old when he became the king [of Judah], and he ruled from Jerusalem for 55 years.
2 Akafanya yalikuwa uovu katika macho ya Yahwe, kama yalivyo mambo ya machukizo ya mataifa ambao Yahwe alikuwa amewafukuza mbele ya watu wa Israeli.
He did many things that Yahweh considered to be evil. He imitated the disgusting things that were formerly done by the people-groups that Yahweh had expelled from Israel as his people advanced [though the land].
3 Kwa maana alizijenga tena sehemu za juu ambazo baba yake Hezekia alikuwa amezibomoa, na akajenga madhabahu kwa ajili ya mabaali, akatengeneza sanaamu za Maashera, na akaziinamia chini nyota zote za mbinguni na kuziabudu.
He commanded his workers to rebuild the shrines [for worshiping idols] that his father Hezekiah had destroyed. He told them to set up altars to [honor] the statues of Baal, and to make altars to [honor the goddess] Asherah. He bowed down to [worship] all the stars.
4 Manase akajenga madhbahu za kipagani katika nyumba ya Yahwe, ingawa Yahwe alikuwa amemwamuru, “Ni katika Yerusalemu ambamo jina langu litawekwa milele”.
He directed his workers to build altars [for foreign gods] in the temple, about which Yahweh had said, “It is here in Jerusalem that I want people to worship me, forever.”
5 Alijenga madhabahu kwa ajili ya nyota zote za mbinguni katika vile viwanja viwili vya nyumba ya Yahwe.
He directed that altars for [worshiping] all the stars be built in both of the courtyards outside the temple.
6 Katika bonde la Beni Hinomu akawaweka wanaye katika moto. Akafanya misemo ya ubashiri, na uchawi, akassoma utabiri; akashauriana na wale waliozungumza na wafu na wale waliozungumza na na roho. Akafanaya maaovu mengi katika mcho ya Yahwe na alimfanya Mungu akasirike.
He even sacrificed [some of] his own sons and burned them in a fire in Hinnom Valley. He performed rituals to practice sorcery. He asked fortune-tellers for advice. He performed witchcraft. He talked to people who consulted the spirits of people who had died to find out what would happen in the future. He did many things that Yahweh considered o be very evil, things that caused Yahweh to become very angry.
7 Ile sanamu ya Maashera aliyokuwa amefanya, akaipeleka katika nyumba ya Mungu. Ni kuhusu nyumba hii ambayo Mungu alikuwa amesema kwa Daudi na Selemani mwanaye; alikuwa amesema, “Ni katika nyumba hii na katika Yerusalemu, ambao nimeuchangua kutoka makabila yote ya Israeli, kwamba nitaliweka jina langu milele.
Manasseh took a carved idol [that his workers had made] and put it in the temple. That is the temple concerning which God had said to David and to his son Solomon, “My temple will be here in Jerusalem, the city that I have chosen [where I want people to] worship me, forever.
8 Sitawaondoa tena watu wa Israeli katina nchi hii ambayo niliitoa kwa babu zao, ikiwa tu watakuwa makini katika kuyashika yote niliyowaamuru, kuzishika sheria zangu, amri zangu, na sheria zangu nilizowapa kupitia Musa.”
If they will obey all the laws and decrees and regulations that I told Moses to give to them, I will not again force the Israeli people to leave this land that I gave to their ancestors.”
9 Manase akawaongoza Yuda na wakaaji wa Yerusalemu hata kufanya uovu zaidi kuliko hata watu wa mataifa ambao Yahwe alikuwa amewateketeza mbele za Israeli.
But Manasseh led the people of Jerusalem and other places in Judah to do things that are wrong, with the result that they did more evil than was done by the people in the people-groups that Yahweh had expelled as the Israeli people advanced [through the land].
10 Yahwe akasema kwa Manase, na kwa watu wake wote, lakini hawakumsikiliza.
Yahweh spoke to Manasseh and the people of Judah, but they paid no attention.
11 Kwa hiyo Yahwe akaleta juu yao maamri jeshsi wa jeshi la Ashuru, ambao walimchukua Manase katika minyonyoro, wakamfunga kwa pingu, na wakampeleka Babeli.
So Yahweh caused the army commanders of Assyria [and their soldiers] to [come to Jerusalem, and they] captured Manasseh. They put a hook in his nose and put bronze chains on his [feet] and took him to Babylon.
12 Manase alipokuwa katika dhika, alimuomba Yahwe, Mungu wake, na akajinyenyekesha sana mbele za Mungu wa babu zake.
There, while he was suffering, he humbled himself greatly in the presence of Yahweh, the God whom his ancestors [worshiped], and pleaded with Yahweh to help him.
13 Akaomba kwake; na Mungu akamsikiliza, na Mungu akasikia kuomba kwake na akamrudisha Yerusalemu, katika ufalme wake. Kisha Manase akafahamu kwamba Yahwe alikuwa Mungu.
When he prayed, Yahweh heard him and pitied him. So he [allowed him to] return to Jerusalem and [to] rule his kingdom again. Then Manasseh realized that Yahweh is [an all-powerful] God.
14 Baada ya hayo, manase akajenga ukuta wa nje ya mji wa Daudi, upande wa magharibi wa Gihoni, katika bonde, hadi kwenye lango la Samaki. Akauzungushia mlima wa Ofeli na akaupandisha ukuta hadi usawa mrefu sana. Akaweka maamri jeshi jasiri katika ngome zote za miji ya Yuda.
Later, Manasseh’s [workers] rebuilt the eastern section of the outer wall around Jerusalem, and [they] made it higher. That section extended from Gihon Spring [north] to the Fish Gate, and around the part of the city that they called Ophel [Hill]. Manasseh also appointed army officers to guard each of the cities in Judah that had walls around them.
15 Akaipeleka mbali miungu yote ya kigeni, akaondoa sanamu zote kwenye nyumba ya Yahwe, na madhabahu zote ambazo alikuwa amejenga juu ya mlima wa nyumba ya Yahwe na katika Yerusalemu, na kuvitupa nje ya mji.
Manasseh’s [workers] removed from the temple the idols and the stone statues of gods of other nations. Manasseh also [told them to] remove the altars that they had previously built on Zion Hill and in [other places in] Jerusalem. He had all those things thrown out of the city.
16 Akaijenga tena madhabahu ya Yahwe na juu yake akatoa sadaka za amani na sadaka za shukrani; akamwamuru Yuda amtumikie Yahwe, Mungu wa Israeli.
Then he [told them to] repair the altar of Yahweh, and he offered sacrifices to restore fellowship with Yahweh and to thank him. And he told [the people of] Judah that they must worship [only] Yahweh.
17 Hata hivyo watu bado walitoa sadaka mahali pa sehemu za juu, lakini kwa Yahwe, Mungu wao pekee.
The people continued to offer sacrifices on the hilltops, but only to Yahweh their God.
18 Katika mambo mengine kuhusu Manase, maombi yake kwa Mungu wake, na maneno ya waonaji ambao walisema kwake katika jina la Yahwe, Mungu wa Israeli, tazama, yameandikwa miongoni mwa matendo ya wafalme wa Israeli.
The other things that happened while Manasseh was ruling, including his prayer to God and the messages from Yahweh that the prophets gave to him, are written in the scroll called ‘The History of the Kings of Israel’.
19 Katika matukio hayo kuna historia ya maombi yake, na jinsi Mungu alivyoguswa na maomabi hayo. Pia kuna kumbu kumbu ya dhambi zake zote na makosa yake, na sehemu ambako alikuwa amejenga sehemu za juu na kuzisimamisha Maashera na sanamu za kuchonga, kambla ya kujinyenyekesha mwenyewe — na imeandikwa kuhusu hayo katika tarehe ya waonaji. (Maandishi ya kale yanasema hivi, “tarehe ya Hozai,” ambayo ni maandishi ya kifungu asili. Lakini matoleo mengi ya kisasa yamesahihisha na kusomeka “tarehe ya waonaj” Pia, matoleo machache ya kisasa yanasema “tarehe ya waonaji”.).
What Manasseh prayed and how God pitied him because he pleaded to God, and also his sins and ways in which he disobeyed God, and the [list of] places where he built shrines and set up poles to [honor the goddess] Asherah and other idols [before he humbled himself], are written in what the prophets wrote.
20 Kwa hiyo Manase akalala na babu zake, na wakamzika katika nyumba yake mwenyewe. Amoni, mwaye, akawa mfalme katika nafasi yake.
Manasseh died and was buried in his palace. Then his son Amon became the king [of Judah].
21 Amoni alikuwa na umri wa miaka ishirini na mbili alipoanza kutawala; alitawala miaka miwili katika Yerusalemu.
Amon was 22 years old when he became king, and he ruled in Jerusalem for two years.
22 Akafanya yaliyokuwa uovu katika macho ya Yaahwe, kama Manase, baba yake, alivyofanya. Amoni alitoa sadaka katika sanamau zote za kuchonga ambazo alitengeneza Manase baba yake, na aliziabudu.
He did things that Yahweh considered to be evil, like his father Manasseh had done. Amon worshiped all the idols that Manasseh’s [workers] had made.
23 Hakujinyenyekesha mbele za Yahwe, kama baba yake Manase alivyokuwa amefanya. Badala yake, Amoni huyu huyu alifanya makosa zaidi na zaidi.
But he did not humble himself and turn to Yahweh like his father did. So he became more sinful than his father had been.
24 Watumishi wake wakapanga njama wa zidi yake na wakamua katika nyumba yake mwenyewe.
Then Amon’s officials made plans to kill him. They assassinated him in his palace.
25 Lakini watu wa nchi wakawaua wote waliofanya njama zidi ya Mfalme Amoni, na wakamfanya Yosia, mwanaye, mfalme katika nafasi yake.
But then the people of Judah killed all those who had assassinated Amon, and they appointed his son Josiah to be their king.

< 2 Nyakati 33 >