< 2 Nyakati 32 >
1 Baada ya mambo haya na matendo haya ya uaminifu, Senakeribu, mfalme wa Ashuru, akaja na kuingia Yuda. Alipiga kambi kwa ajili ya kuivamia miji yenye ngome, ambayo alikusudia kuiteka kwa ajili yake.
Or, après ces choses faites avec sincérité, Sennachérib, roi des Assyriens, vint envahir Juda, et campa devant les villes fortes pour s'en emparer.
2 Sedekia alipoona kwamba Senakeribu amekuja na kwamba amedhamiria kupigana zidi ya Yerusalemu,
Et Ezéchias vit que Sennachérib s'avançait et menaçait Jérusalem.
3 aliwashirikisha viongozi wake na watu wake wenye nguvu kuyazuia maji ya chemichemi yaliyokuwa nje ya mji; waalimsaidia kufanya hivyo.
Et il tint conseil avec ses anciens et ses vaillants, leur proposant de clore les fontaines hors de la ville; et ils l'appuyèrent de toute leur force.
4 Kwa hiyo watu wengi wakakusanyika na kuyazuia maji ya chemichemi zote na mikondo yote amabayo ilikuwa inatiririka katikati ya nchi. wakasema, “Kwa nini mfalme wa Ashuru aje na kupata maji mengi?”
Il assembla donc beaucoup de monde, et il renferma en des murs les eaux des fontaines, ainsi que le ruisseau qui traverse la ville, disant: C'est de peur que le roi d'Assyrie, venant, ne trouve une abondance d'eau qui le fortifierait.
5 Hezekia akijipa ujasiri na kuujeenga ukuta wote uliokuwa umeangushwa chini. Akaijenga minara mirefu, na pia ukuta mwingine nje. Pia akaiimarisha Milo katika mji wa Dudi, na akafanya kiasi kikubwa cha silaha na ngao. (Maanshi ya kale yanasema hivi: “Badala ya, “akajenga minara amirefu”, baadhi ya matoleo ya zamani na kisasa yanasema, “akajenga minara mirefu juu yake”, Hii ni juu ya ukuta).
Et Ezéchias augmenta ses défenses; il rétablit toutes les parties des remparts qui s'étaient écroulées et les tours; il bâtit en dehors une seconde enceinte, il releva les fortifications de la ville de David; enfin, il fit faire beaucoup d'armes.
6 Akaweka maamri jeshi juu wa watu. Akawakusanya pamoja kwake katika sehemu pana kwenye lango la mji na akasema kwao kwa ujasiri. Akasema,
Ensuite, il mit des chefs de guerre à la tête du peuple qui s'assembla devant lui sur l'esplanade, vers la porte de la Vallée, et il lui parla au cœur, disant:
7 “Muwe imara na wenye ujasiri mzuri. Msiogope wala kukata tamaa kwa sababu ya mfalme wa Ashuru na jeshi lote ambalo liko naye, kwa maana kuna mtu yuko pamoja nasi ambaye ni mkuu kuliko
Soyez forts, agissez en hommes, n'ayez ni crainte ni faiblesse devant le roi d'Assyrie, et devant les peuples qui le suivent; car il y a plus d'auxiliaires avec nous qu'avec lui.
8 walio naye mfalme wa Ashuru. walionaye ni jeshi la mwili tu, lakini aliye nasi ni Yahwe, Mungu wetu, kwa ajili ya kutusaidia, na kupiagana vita vyetu.” Kisha watu wakajifariji wenyewe kwa maneno ya Hezekia, mfalme wa Yuda.
Il a pour lui des bras de chair; nous, nous avons le Seigneur notre Dieu, qui combattra pour nous et nous sauvera. Et le peuple fut encouragé par le discours d'Ezéchias, roi de Juda.
9 Baada ya hayo, Senakeribu, mfalme wa Ashuru, aliwatuma watumishi wake kwenda Yetusalemu (sasa alikuwa mbe ya Lakishi, na jeshi lake lote lilikuwa pamoja naye), kwa Hezekia, mfaalme wa Yuda, na watu wote wa Yuda walikuwa Yerusalemu. Akasema,
Après cela, Sennachérib, roi des Assyriens, envoya ses serviteurs à Jérusalem, et lui-même, avec toute son armée, était autour de Lachis, et il envoya ses serviteurs au roi Ezéchias et à tout le peuple de Juda renfermé dans Jérusalem, disant:
10 “Hivi ndivyo Senakeribu, mfalme wa Ashuru, anasema: Ni kitu gani mnategemea kwa ajili ya kuhimili uvamizi katika Yerusalemu?
Voici ce que dit Sennachérib, roi des Assyriens: Sur quoi vous appuyez- vous pour rester immobiles dans l'enceinte de Jérusalem?
11 Je, Hezekia hawapotoshi ninyi, ili kwamba awatoe kufa kwa njaa na kiu, anapowaambia, “Yahwe Mungu wetu atatuokoa na mkono wa mfalme wa Ashuru?
Ezéchias ne vous a-t-il pas trompés, pour vous livrer à la faim, à la soif, à la mort, quand il vous a dit: Le Seigneur notre Dieu nous sauvera des mains du roi d'Assyrie?
12 Je, siyo Hezekia yule yule ambaye amezipeleka juu sehemu zake na madhabahu zake na kuwaamuru Yuda na Yerusalemu, juu ya madhabahu moja lazima muabudu, na juu yake lazima mchome sadaka zenu?
N'est-ce point cet Ezéchias qui a détruit ses autels et ses hauts lieux, et qui a dit à Juda et à Jérusalem: Vous adorerez sur cet autel, et, sur cet autel, vous offrirez de l'encens?
13 Je, hamjui mimi na babu zangu tulifanya nini kwa makundi ya wote wa inchi zingine? Je, miungu ya watu wa hizo nchi iliweza kwa njia yoyote kuziokoa nchi zao zidi ya nguvu zangu?
Ignorez-vous ce que moi et mes pères avons fait aux peuples de toute la terre? Parmi les dieux des nations de la terre, en est-il un seul qui ait pu sauver son peuple de mes mains?
14 Miongoni mwa miungu yote ya mataifa hayo amabayo babu zangu waliwatekeza, je, kulikuwa na muungu yeyote aliyeweza kuwaokoa watu wake kutoka kwenye mkono wangu? Itakuwaje Mungu wenu aweze kuwakoa ninyi zidi ya nguvu zangu?
Qui l'a fait, parmi les dieux des nations que nos pères ont exterminées? Si nul d'eux n'a pu sauver son peuple de nos mains, votre Dieu pourra t-il le faire?
15 Sasa msimuruhusu Hezekia awadanganye au kuwashawishi katika njia hii. Msimwamini, kwa maana hakuna muungu wa taifa lolote au ufalme amewahi kuwaokoa watu wake nje ya mkono wangu, au nje ya mkono wa babu zangu. Sembuse na Mungu wenu kwa namna gani atawaokoa na mkono wangu?
Qu'Ezéchias cesse donc de vous tromper, qu'il ne vous inspire pas une folle confiance, ne le croyez pas; car nul, des dieux des nations et des royaumes, n'a pu sauver son peuple de mes mains et des mains de nos pères, et votre Dieu ne vous sauvera pas non plus.
16 Watumishi wa Senakeribu hata walinena mabaya zaidi juu ya Yahwe Mungu na juu ya mtumishi wake Hezekia.
Or, les serviteurs de Sennachérib continuèrent de parler contre le Seigneur Dieu et contre son serviteur Ezéchias.
17 Senakeribu pia akandika barua ili kumdhihaki Yahwe, Mungu wa Israeli, na kunena kinyume naye. Alisema, “Kama ambavyo miungu ya mataifa haikuwaokoa watu wake kutoka kwenye mkono wangu, hivyo hivyo na Mungu wa Hezekia hatawaokoa watu wake kutoka kwenye mkono wangu.”
Lui-même écrivit une lettre pour outrager le Seigneur Dieu d'Israël, et il dit: De même que les dieux des nations de la terre n'ont pu délivrer leurs peuples de mes mains, le Dieu d'Ezéchias ne pourra en aucune manière sauver son peuple.
18 Wakawalilia kwa lugha ya Wayahudi watu wa Yerusalemu waliokuwa juu ya ukuta, ili kuwaogopesha na kuwasumbua, ili kwamba waweze kuuteka mji.
Et l'un des serviteurs cria, en langue judaïque, au peuple de Jérusalem qui se tenait sur les remparts, l'invitant à haute voix à les seconder à démolir les murailles, à leur livrer la ville.
19 Wakamnenea Mungu wa Yerusalemu kama walivyowanenea miungu wa Dunia, ambao ni kazi ya mikono ya wanadamu tu.
Il parla aussi contre le Seigneur Dieu d'Israël, de la même manière que contre les dieux des nations de la terre, œuvres des mains des hommes.
20 Hezekia, mfalme, na Isaya mwana wa Amozi, nabii, wakaomba kwa sababu ya jambo hili na wakalia hadi mbinguni.
Et, sur ces paroles, le roi Ezéchias et le prophète Isaïe, fils d'Amos, prièrent, et crièrent au ciel.
21 Yahwe akatuma malaika, ambaye aliwaua wanaume wa kupigana vita, majemedari, na maakida wa mfalme katika kambi. Kwa hiyo Senakeribu akarudi katika nchi yake akiwa na uso wa aibu. Alipokuwa ameenda katika nyumba ya muungu wake, baadhi ya watoto wake wakamuua huko kwa upanga.
Et le Seigneur envoya un ange, et il extermina dans le camp assyrien tous les combattants, les chefs et les généraux. Et Sennachérib, la honte au front, retourna en son royaume, et il entra dans le temple de son Dieu; et des hommes, issus de son sang, le firent périr par le glaive.
22 Katika namna hii, Yahwe akamwokoa Hezekia na wakazi wa Yerusalemu kutoka kwenye mkono wa Senakeribu, mfalme wa Ashuru, na kutoka kwenye mikono ya wengine, na akawapa pumzika juu ya kila upande. (Maandishi ya kale yanasema hivi: badala ya “akawapa pumziko juu ya kila pande”, baadhi ya matoleo ya zamani na ya kisasa yanasema, “akawaongoza juu ya kila pande”).
Et le Seigneur sauva Ezéchias, ainsi que les habitants de Jérusalem, des mains de Sennachérib, roi d'Assyrie, et des mains de tous les rois, et il leur donna le repos tout alentour.
23 Wengi walikuwa wakileta sadaka kwa Yahwe katika Yarusalemu, na zawadi za thamani kwa Hezekia mfalme wa Yuda, kwa hiyo aliinuliwa mbele za macho ya mataifa yote toka wakati huo na kuendelea.
Et nombre de gens apportèrent à Jérusalem des présents pour le Seigneur et pour Ezéchias, roi de Juda, et, après cela, il fut glorifié aux yeux de toutes les nations.
24 Katika siku hizo Hezekia akaugua hadi hatua ya kufa. Akaomba kwa Yahwe, ambaye alisema kwake na kumpa ishara kwamba angeponywa.
En ces jours-là, Ezéchias tomba malade à en mourir, et il pria le Seigneur, et le Seigneur l'exauça, et il lui donna un signe.
25 Lakini Hezekia hakumlipa Yahwe kwa ajili ya msaada uliotolewa kwake, kwa maana moyo wake uliinuliwa juu.
Mais Ezéchias ne lui rendit pas selon ce qu'il en avait reçu; son cœur s'enorgueillit, et la colère du Seigneur éclata contre le roi, contre Juda, contre Jérusalem.
26 Kwa hiyo hasira ikaja juu yake, na juu ya Yuda na Yerusalemu. Hata hivyo, baadaye Hezekia alijinyenyekesha mwenyewe kwa jali ya kiburi cha moyo wake, wote Yeye na wakaaji wa Yerusalemu, hivyo hasira ya Yahwe haikuja juu yao wakati wa siku za Hezekia.
Et Ezéchias s'humilia de s'être enorgueilli en son cœur, et, avec lui, tous les habitants de Jérusalem; et la colère du Seigneur ne vint plus sur eux tant que vécut Ezéchias.
27 Hezekia alikuwa na utajiri mwingi sana na heshima kubwa. Alijipatia mwenyewe vyumba vya kuhifadhia kwa ajili ya fedha, dhahabu, vito vya thamani, na kwa ajili ya manukato, na kwa ajili ya ngao na na vyombo vyote vya thamani pia.
Et Ezéchias eut beaucoup de gloire et de richesses; il amassa, en ses trésors, de l'or, de l'argent, des pierreries; il eut des épices, des vases de prix et des arsenaux.
28 Pia alikuwa na nyumba za maghala kwa ajili ya mavuno ya nafaka, divai mpya, na mafuta, na malisho kwa ajili ya aina zote za wanyama.
Il eut des villes où l'on conservait du blé, du vin et de l'huile; il eut des villages et des étables pour toute sorte de bétail, et des bergeries pour les menus troupeaux.
29 Pia alikuwa na makundi katika mazizi. Zaidi ya hayo, alijipatia mwenyewe miji na makundi ya na ng'ombe kwa wingi, kwa maana Mungu alaikuwa amempa afya tele. (Maandishi ya kale yanasema hivi: Badala ya “miji” baadji ya matoleo ya kisasa yanasema “punda”, na baadhi mengine ya kisasa yanaacaha neno nzima)
Il eut des villes, qu'il bâtit pour lui-même, et une grande abondance de bœufs et de brebis; car le Seigneur lui donna d'immenses richesses.
30 Alikuwa ni Hezekia huyu huyu ambaye alisimamisha chemi chemi ya juu ya maji ya Gihoni, na aliye ileta moja kwa moja chini upande wa magharibi mwa mji wa Daudi. Hezekia alifanikiwa katika miradi yake yote.
Ce fut Ezéchias qui fit l'aqueduc qui amena les eaux de la haute fontaine de Gihon en la ville basse de David, au midi. Ezéchias réussit en toutes ses entreprises.
31 Hata hivyo, katika jambo la mabolozi wa wakuu wa Babeli, waliotumwa kwake kuwauliza waliofahamu, kuhusu ishara za miujiza iliyokuwa imefanywa katika nchi, Mungu alimwachia mwenyewe, ili kumjaribu, na kujua yote yaliyokuwa katika moyo wake.
Néanmoins, le Seigneur l'abandonna pour l'éprouver et savoir ce qu'il avait dans le cœur, lorsque les envoyés des chefs de Babylone vinrent le trouver et le questionner sur le prodige qui avait éclaté en la terre promise.
32 Kwa mambo mengine kuhusu Hezekia, pamoja na matendo yake ya uaminifu wa agano, unaweza kuona kwamba yameandikwa katika Maono ya Nabii Isaya Mwana wa Amozi, na katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
Le reste des actes d'Ezéchias et sa miséricorde sont écrits en la prophétie d'Isaïe, fils d'Amos, le prophète, et au livre des Rois de Juda et d'Israël.
33 Hezekia akalala pamaoja na babu zake, na wakamzika katika mlima wa makaburi ya vizazi vya Daudi. Yuda wote na wakaaji wa Yerusalemu wakamheshimu katika kifo chake. Manase mwanaye akawa mfalme katika nafasi yake.
Et Ezéchias s'endormit avec ses pères, et on l'ensevelit au-dessus des sépulcres des fils de David; et tout Juda et les habitants de Jérusalem l'honorèrent et le glorifièrent à sa mort. Et Manassé, son fils, régna à sa place.