< 2 Nyakati 32 >
1 Baada ya mambo haya na matendo haya ya uaminifu, Senakeribu, mfalme wa Ashuru, akaja na kuingia Yuda. Alipiga kambi kwa ajili ya kuivamia miji yenye ngome, ambayo alikusudia kuiteka kwa ajili yake.
After these things faithfully described, Saneherib King of Asshur came and entred into Iudah, and besieged the strong cities, and thought to winne them for him selfe.
2 Sedekia alipoona kwamba Senakeribu amekuja na kwamba amedhamiria kupigana zidi ya Yerusalemu,
When Hezekiah sawe that Saneherib was come, and that his purpose was to fight against Ierusalem,
3 aliwashirikisha viongozi wake na watu wake wenye nguvu kuyazuia maji ya chemichemi yaliyokuwa nje ya mji; waalimsaidia kufanya hivyo.
Then he tooke counsell with his princes and his nobles, to stoppe the water of the fountaines without the citie: and they did helpe him.
4 Kwa hiyo watu wengi wakakusanyika na kuyazuia maji ya chemichemi zote na mikondo yote amabayo ilikuwa inatiririka katikati ya nchi. wakasema, “Kwa nini mfalme wa Ashuru aje na kupata maji mengi?”
So many of the people assembled themselues, and stopt all the fountaines, and the riuer that ranne through the middes of the countrey, saying, Why should the Kings of Asshur come, and finde much water?
5 Hezekia akijipa ujasiri na kuujeenga ukuta wote uliokuwa umeangushwa chini. Akaijenga minara mirefu, na pia ukuta mwingine nje. Pia akaiimarisha Milo katika mji wa Dudi, na akafanya kiasi kikubwa cha silaha na ngao. (Maanshi ya kale yanasema hivi: “Badala ya, “akajenga minara amirefu”, baadhi ya matoleo ya zamani na kisasa yanasema, “akajenga minara mirefu juu yake”, Hii ni juu ya ukuta).
And he tooke courage, and built all the broken wall, and made vp the towers, and another wall without, and repayred Millo in the citie of Dauid, and made many dartes and shields.
6 Akaweka maamri jeshi juu wa watu. Akawakusanya pamoja kwake katika sehemu pana kwenye lango la mji na akasema kwao kwa ujasiri. Akasema,
And he set captaines of warre ouer the people, and assembled them to him in the broade place of the gate of the citie, and spake comfortably vnto them, saying,
7 “Muwe imara na wenye ujasiri mzuri. Msiogope wala kukata tamaa kwa sababu ya mfalme wa Ashuru na jeshi lote ambalo liko naye, kwa maana kuna mtu yuko pamoja nasi ambaye ni mkuu kuliko
Be strong and couragious: feare not, neither be afraide for the King of Asshur, neither for all the multitude that is with him: for there be more with vs, then is with him.
8 walio naye mfalme wa Ashuru. walionaye ni jeshi la mwili tu, lakini aliye nasi ni Yahwe, Mungu wetu, kwa ajili ya kutusaidia, na kupiagana vita vyetu.” Kisha watu wakajifariji wenyewe kwa maneno ya Hezekia, mfalme wa Yuda.
With him is an arme of flesh, but with vs is the Lord our God for to helpe vs, and to fight our battels. Then the people were confirmed by the wordes of Hezekiah King of Iudah.
9 Baada ya hayo, Senakeribu, mfalme wa Ashuru, aliwatuma watumishi wake kwenda Yetusalemu (sasa alikuwa mbe ya Lakishi, na jeshi lake lote lilikuwa pamoja naye), kwa Hezekia, mfaalme wa Yuda, na watu wote wa Yuda walikuwa Yerusalemu. Akasema,
After this, did Saneherib King of Asshur send his seruants to Ierusalem (while he was against Lachish, and all his dominion with him) vnto Hezekiah King of Iudah and vnto all Iudah that were at Ierusalem, saying,
10 “Hivi ndivyo Senakeribu, mfalme wa Ashuru, anasema: Ni kitu gani mnategemea kwa ajili ya kuhimili uvamizi katika Yerusalemu?
Thus saith Saneherib the King of Asshur, Wherein doe ye trust, that ye will remaine in Ierusalem, during the siege?
11 Je, Hezekia hawapotoshi ninyi, ili kwamba awatoe kufa kwa njaa na kiu, anapowaambia, “Yahwe Mungu wetu atatuokoa na mkono wa mfalme wa Ashuru?
Doeth not Hezekiah entice you to giue ouer your selues vnto death by famine and by thirst, saying, The Lord our God shall deliuer vs out of the hande of the King of Asshur?
12 Je, siyo Hezekia yule yule ambaye amezipeleka juu sehemu zake na madhabahu zake na kuwaamuru Yuda na Yerusalemu, juu ya madhabahu moja lazima muabudu, na juu yake lazima mchome sadaka zenu?
Hath not the same Hezekiah taken away his hie places and his altars, and commanded Iudah and Ierusalem, saying, Ye shall worshippe before one altar, and burne incense vpon it?
13 Je, hamjui mimi na babu zangu tulifanya nini kwa makundi ya wote wa inchi zingine? Je, miungu ya watu wa hizo nchi iliweza kwa njia yoyote kuziokoa nchi zao zidi ya nguvu zangu?
Knowe ye not what I and my fathers haue done vnto all the people of other countreyes? were the gods of the nations of other landes able to deliuer their land out of mine hande?
14 Miongoni mwa miungu yote ya mataifa hayo amabayo babu zangu waliwatekeza, je, kulikuwa na muungu yeyote aliyeweza kuwaokoa watu wake kutoka kwenye mkono wangu? Itakuwaje Mungu wenu aweze kuwakoa ninyi zidi ya nguvu zangu?
Who is he of al the gods of those natios (that my fathers haue destroied) that could deliuer his people out of mine hande? that your God should be able to deliuer you out of mine hand?
15 Sasa msimuruhusu Hezekia awadanganye au kuwashawishi katika njia hii. Msimwamini, kwa maana hakuna muungu wa taifa lolote au ufalme amewahi kuwaokoa watu wake nje ya mkono wangu, au nje ya mkono wa babu zangu. Sembuse na Mungu wenu kwa namna gani atawaokoa na mkono wangu?
Nowe therefore let not Hezekiah deceiue you, nor seduce you after this sort, neither beleeue ye him: for none of all the gods of any nation or kingdome was able to deliuer his people out of mine hande and out of the hande of my fathers: howe much lesse shall your gods deliuer you out of mine hande?
16 Watumishi wa Senakeribu hata walinena mabaya zaidi juu ya Yahwe Mungu na juu ya mtumishi wake Hezekia.
And his seruants spake yet more against the Lord God, and against his seruant Hezekiah.
17 Senakeribu pia akandika barua ili kumdhihaki Yahwe, Mungu wa Israeli, na kunena kinyume naye. Alisema, “Kama ambavyo miungu ya mataifa haikuwaokoa watu wake kutoka kwenye mkono wangu, hivyo hivyo na Mungu wa Hezekia hatawaokoa watu wake kutoka kwenye mkono wangu.”
He wrote also letters, blaspheming the Lord God of Israel and speaking against him, saying, As the gods of the nations of other countreies could not deliuer their people out of mine hand, so shall not the God of Hezekiah deliuer his people out of mine hande.
18 Wakawalilia kwa lugha ya Wayahudi watu wa Yerusalemu waliokuwa juu ya ukuta, ili kuwaogopesha na kuwasumbua, ili kwamba waweze kuuteka mji.
Then they cryed with a loude voyce in the Iewes speach vnto the people of Ierusalem that were on the wall, to feare them and to astonish them, that they might take the citie.
19 Wakamnenea Mungu wa Yerusalemu kama walivyowanenea miungu wa Dunia, ambao ni kazi ya mikono ya wanadamu tu.
Thus they spake against the God of Ierusalem, as against the gods of the people of the earth, euen the workes of mans hands,
20 Hezekia, mfalme, na Isaya mwana wa Amozi, nabii, wakaomba kwa sababu ya jambo hili na wakalia hadi mbinguni.
But Hezekiah the King, and the Prophet Isaiah the sonne of Amoz prayed against this and cryed to heauen.
21 Yahwe akatuma malaika, ambaye aliwaua wanaume wa kupigana vita, majemedari, na maakida wa mfalme katika kambi. Kwa hiyo Senakeribu akarudi katika nchi yake akiwa na uso wa aibu. Alipokuwa ameenda katika nyumba ya muungu wake, baadhi ya watoto wake wakamuua huko kwa upanga.
And the Lord sent an Angel which destroyed all the valiant men, and the princes and captaines of the hoste of the King of Asshur: so he returned with shame to his owne lande. And when he was come into the house of his god, they that came foorth of his owne bowels, slewe him there with the sworde.
22 Katika namna hii, Yahwe akamwokoa Hezekia na wakazi wa Yerusalemu kutoka kwenye mkono wa Senakeribu, mfalme wa Ashuru, na kutoka kwenye mikono ya wengine, na akawapa pumzika juu ya kila upande. (Maandishi ya kale yanasema hivi: badala ya “akawapa pumziko juu ya kila pande”, baadhi ya matoleo ya zamani na ya kisasa yanasema, “akawaongoza juu ya kila pande”).
So the Lord saued Hezekiah and the inhabitants of Ierusalem from the hande of Saneherib King of Asshur, and from the hande of all other, and maintained them on euery side.
23 Wengi walikuwa wakileta sadaka kwa Yahwe katika Yarusalemu, na zawadi za thamani kwa Hezekia mfalme wa Yuda, kwa hiyo aliinuliwa mbele za macho ya mataifa yote toka wakati huo na kuendelea.
And many brought offrings vnto the Lord to Ierusalem, and presents to Hezekiah King of Iudah, so that he was magnified in the sight of all nations from thencefoorth.
24 Katika siku hizo Hezekia akaugua hadi hatua ya kufa. Akaomba kwa Yahwe, ambaye alisema kwake na kumpa ishara kwamba angeponywa.
In those dayes Hezekiah was sicke vnto the death, and prayed vnto the Lord, who spake vnto him, and gaue him a signe.
25 Lakini Hezekia hakumlipa Yahwe kwa ajili ya msaada uliotolewa kwake, kwa maana moyo wake uliinuliwa juu.
But Hezekiah did not render according to the rewarde bestowed vpon him: for his heart was lift vp, and wrath came vpon him, and vpon Iudah and Ierusalem.
26 Kwa hiyo hasira ikaja juu yake, na juu ya Yuda na Yerusalemu. Hata hivyo, baadaye Hezekia alijinyenyekesha mwenyewe kwa jali ya kiburi cha moyo wake, wote Yeye na wakaaji wa Yerusalemu, hivyo hasira ya Yahwe haikuja juu yao wakati wa siku za Hezekia.
Notwithstanding Hezekiah humbled him selfe (after that his heart was lifted vp) he and the inhabitants of Ierusalem, and the wrath of the Lord came not vpon them in the dayes of Hezekiah.
27 Hezekia alikuwa na utajiri mwingi sana na heshima kubwa. Alijipatia mwenyewe vyumba vya kuhifadhia kwa ajili ya fedha, dhahabu, vito vya thamani, na kwa ajili ya manukato, na kwa ajili ya ngao na na vyombo vyote vya thamani pia.
Hezekiah also had exceeding much riches and honour, and he gate him treasures of siluer, and of golde, and of precious stones, and of sweete odours, and of shieldes, and of all pleasant vessels:
28 Pia alikuwa na nyumba za maghala kwa ajili ya mavuno ya nafaka, divai mpya, na mafuta, na malisho kwa ajili ya aina zote za wanyama.
And of store houses for the increase of wheat and wine and oyle, and stalles for all beasts, and rowes for the stables.
29 Pia alikuwa na makundi katika mazizi. Zaidi ya hayo, alijipatia mwenyewe miji na makundi ya na ng'ombe kwa wingi, kwa maana Mungu alaikuwa amempa afya tele. (Maandishi ya kale yanasema hivi: Badala ya “miji” baadji ya matoleo ya kisasa yanasema “punda”, na baadhi mengine ya kisasa yanaacaha neno nzima)
And he made him cities, and had possession of sheepe and oxen in abundance: for God had giuen him substance exceeding much.
30 Alikuwa ni Hezekia huyu huyu ambaye alisimamisha chemi chemi ya juu ya maji ya Gihoni, na aliye ileta moja kwa moja chini upande wa magharibi mwa mji wa Daudi. Hezekia alifanikiwa katika miradi yake yote.
This same Hezekiah also stopped the vpper water springs of Gihon, and led them streight vnderneath towarde the citie of Dauid Westwarde. so Hezekiah prospered in all his workes.
31 Hata hivyo, katika jambo la mabolozi wa wakuu wa Babeli, waliotumwa kwake kuwauliza waliofahamu, kuhusu ishara za miujiza iliyokuwa imefanywa katika nchi, Mungu alimwachia mwenyewe, ili kumjaribu, na kujua yote yaliyokuwa katika moyo wake.
But because of the ambassadours of the princes of Babel, which sent vnto him to enquire of the wonder that was done in the lande, God left him to trie him, and to knowe all that was in his heart.
32 Kwa mambo mengine kuhusu Hezekia, pamoja na matendo yake ya uaminifu wa agano, unaweza kuona kwamba yameandikwa katika Maono ya Nabii Isaya Mwana wa Amozi, na katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
Concerning the rest of the actes of Hezekiah, and his goodnesse, beholde, they are written in the vision of Ishiah the Prophet, the sonne of Amoz, in the booke of the Kings of Iudah and Israel.
33 Hezekia akalala pamaoja na babu zake, na wakamzika katika mlima wa makaburi ya vizazi vya Daudi. Yuda wote na wakaaji wa Yerusalemu wakamheshimu katika kifo chake. Manase mwanaye akawa mfalme katika nafasi yake.
So Hezekiah slept with his fathers, and they buryed him in the highest sepulchre of the sonnes of Dauid: and all Iudah and the inhabitants of Ierusalem did him honour at his death: and Manasseh his sonne reigned in his stead.