< 2 Nyakati 30 >

1 Hzekia akatuma wajumbe kwa Israeli wote na Yuda, na pia akawaandikia barua Efraimu na Manase, kwamba waje kwenye nyumba ya Yahwe katika Yerusalemu, kusherekea Pasaka ya Yahwe, Mungu wa Israeli.
And Ezechias sent to all Israel and Juda: and he wrote letters to Ephraim and Manasses, that they should come to the house of the Lord in Jerusalem, and keep the phase to the Lord the God of Israel.
2 Kwa maana mfalme, viongozi wake, na kusanyiko lote katika Yerusalemu walikuwa wameshauriana pamoja, wakakubaliana kusherekea Pasaka katika mwezi wa pili.
For the king, taking counsel, and the princes, and all the assembly of Jerusalem, decreed to keep the phase the second month.
3 Hawakuweza kuisherekea mapema kabla ya hapo, kwa sababu hapakuwa na makuhani wa kutosha waliojitakasa wenyewe, wala watu hawakuwa wamekusanyika pamoja Yerusalemu.
For they could not keep it in its time; because there were not priests enough sanctified, and the people was not as yet gathered together to Jerusalem.
4 Pendekezo hili likaonekana sahihi katika macho ya mfalme na ya kusanyiko lote.
And the thing pleased the king, and all the people.
5 Kwa hiyo wakakubaliana kufanya tangazo katika Israeli yote, kuanzia Beer-sheba hadi Dani, kwamba watu lazima waje kusherehekea Paska ya Yahwe, Mungu wa Israeli, huko Yerusalemu. Kwa maana walikuwa hawakuwa wameisherehekea kwa hesabu kubwa ya watu, kwa mujibu wa jinsi ilivyokuwa imeandikwa.
And they decreed to send messengers to all Israel from Bersabee even to Dan, that they should come, and keep the phase to the Lord the God of Israel in Jerusalem: for many had not kept it as it is prescribed by the law.
6 Hivyo matarishi wakaenda na barua kutoka kwa mfalme na viongozi wake katika Israeli na Yuda yote, kwa agizo la mfalme. wakasema, “Ninyi watu wa Israeli, rudini kwa Yahwe, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Israeli, ili kwamba aweze kuwarudia masalia wenu ninyi mlipona kutoka kwenye mkono wa wafalme wa Ashuru.
And the posts went with letters by commandment of the king, and his princes, to all Israel and Juda, proclaiming according to the king’s orders: Ye children of Israel, turn again to the Lord the God of Abraham, and of Isaac, and of Israel: and he will return to the remnant of you that have escaped the hand of the king of the Assyrians.
7 Msiwe kama babu zenu au ndugu zenu, ambao walimuasi Yahwe, Mungu wa mababu zao, hivyo akawaweka katika kuangamia, kama mnavyoona.
Be not like your fathers, and brethren, who departed from the Lord the God of their fathers, and he hath given them up to destruction, as you see.
8 Sasa msiwe wasumbufu, kama babu zenu walivyokuwa; badala yake, jitoeni wenyewe kwa Yahwe na njoeni kwenye sehemu yake takatifu, ambayo ameitakasa milele, na mwabuduni Yahwe Mungu wenu, ili kwamba uso wake wenye hasira uwageukie mbali.
Harden not your necks, as your fathers did: yield yourselves to the Lord, and come to his sanctuary, which he hath sanctified for ever: serve the Lord the God of your fathers, and the wrath of his indignation shall be turned away from you.
9 Kwa maana ikiwa mtageuka nyuma kwa Yahwe, ndugu zenu na watoto wenu watapata huruma mbele ya hao wanaowaongoza kama wafungwa, na watarudi katika nchi hii. Kwa maana Yahwe Mungu wenu, ni mkarimu na mwenye huruma, na hatawageuzia mbali uso wake, kama mtarudi kwake.”
For if you turn again to the Lord: your brethren, and children shall find mercy before their masters, that have led them away captive, and they shall return into this land: for the Lord your God is merciful, and will not turn away his face from you, if you return to him.
10 Kwa hiyo matarishi wakapita mji kwa mji katika majimbo ya Efraimu na Manase, njia yote hadi Zabuloni, lakini watu waliwacheka na kuwazomea.
So the posts went speedily from city to city, through the land of Ephraim, and of Manasses, even to Zabulon, whilst they laughed at them and mocked them.
11 Lakini, watu wengine wa Asheri na Manase na Zabuloni walijinyenyekesha wenyewe na wakaja Yerusalemu.
Nevertheless some men of Aser, and of Manasses, and of Zabulon, yielding to the counsel, came to Jerusalem.
12 Mkono wa Mungu pia ukaja juu ya Yuda, kuwapa moyo mmmoja, ili kulikubali agizo la mfalme na viongozi kwa neno la Yahwe.
But the hand of God was in Juda, to give them one heart to do the word of the Lord, according to the commandment of the king, and of the princes.
13 Watu wengi, kusanyiko kubwa, likakusanyika Yerusalemu kusherehekea Sikukuu ya Mikate Isiyochacha katika mwezi wa pili.
And much people were assembled to Jerusalem to celebrate the solemnity of the unleavened bread in the second month:
14 Waliinuka na kuchukua madhabahu zizilizokuwa Yerusalemu, madhabahu zote kwa ajili ya sadaka za kufukiza; wakazirusha katika kijito Kidroni.
And they arose and destroyed the altars that were in Jerusalem, and took sway all things in which incense was burnt to idols, and cast them into the torrent Cedron.
15 Kisha wakamuua mwanakondoo wa Paska katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili. Makuhani na Walawi wakaona aibu, kwa hiyo wakajitakasa wenyewe na kuleta sadaka za kuteketezwa katika nyumba ya Yahwe.
And they immolated the phase on the fourteenth day of the second month. And the priests and the Levites being at length sanctified offered holocausts in the house of the Lord.
16 Wakasimama katika sehemu zao katika makaundi yao, wakifuata maelekezo yaliyotolewa na sheria ya Musa, mtu wa Mungu. Makuhani wakainyunyiza damu waliyoipokea kutoka kwenye mikono ya Walawi.
And they stood in their order according to the disposition, and law of Moses the man of God: but the priests received the blood which was to be poured out, from the hands of the Levites,
17 Kwa maana walikuwepo wengi katika kusanyikao amaabao hawakuwa wamejitakasa wenyewe. Kwa hiyo Makuhani wakamchinja mwanakondoo wa Pasaka kwa ajili ya kila mmoja ambaye hakuwa amejisafisha na hakuweza kuzitakasa sadaka zake kwa Yahwe.
Because a great number was not sanctified: and therefore the Levites immolated the phase for them that came not in time to be sanctified to the Lord.
18 Kwa kuwa wingi wa watu, wengi wao kutoka Efraimu na Manase, Asakari na Zabuloni, hawakuwa wamejitakasa wenyewe, bado waliula mlo wa Paska, kinyume na maelekezo yaliyoandikwa. Kwa kuwa Hezekia alikuwa amewaombea, akisema, “Mungu Yahwe amsamehe kila mmoja
For a great part of the people from Ephraim, and Manasses, and Issachar, and Zabulon, that had not been sanctified, ate the phase otherwise than it is written: and Ezechias prayed for them, saying: The Lord who is good will shew mercy,
19 ambaye anaulekeza moyo wake kumtafuta Mungu, Yahwe, Mungu wa babu zake, hata kama hajasafiswa kwa utakaso wa viwango vya patakatifu.”
To all them, who with their whole heart, seek the Lord the God of their fathers: and will not impute it to them that they are not sanctified.
20 Kwa hiyo Yahwe akamsikiliza Hezekia na akawaponya watu.
And the Lord heard him, and was merciful to the people.
21 Watu wa Israeli waliokuwepo Yerusalemu wakaitunza Sikukuu ya Mikaate Isiyochachwa na furaha kubwa kwa siku saba. Walawi na makuhani wakamsifu Yahwe siku baada ya siku, wakiimwimbia Yahwe kwa vyombo vya sauti kuu.
And the children of Israel, that were found at Jerusalem, kept the feast of unleavened bread seven days with great joy, praising the Lord every day: the Levites also, and the priests, with instruments that agreed to their office.
22 Hezekia akazungumza kwa kuwatia moyo Walawi wote walioilewa ibada ya Yahwe, Kwa hiyo wakala kwa kipindi cha siku saba, wakitoa sadaka za amani, na kufanya toba kwa Yahwe, Mungu wa babu zao.
And Ezechias spoke to the heart of all the Levites, that had good understanding concerning the Lord: and they ate during the seven days of the solemnity, immolating victims of peace offerings, and praising the Lord the God of their fathers.
23 Kusanyiko lote kisha likaamua kusherehekea kwa siku zingine saba, na wakafanya hivyo kwa furaha.
And it pleased the whole multitude to keep other seven days: which they did with great joy.
24 Kwa kuwa Hezekia mfalme wa Yuda aliwapa kusanyiko ng'ombe dume elf moja, na kondoo elfu saba kama sadaka; na viongozi wakawapa kusanyiko ng'ombe dume elfu moja na kondoo na mbuzi elfu kumi. Idadi kubwa ya makuhani wakajitakasa wenyewe.
For Ezechias the king of Juda had given to the multitude a thousand bullocks, and seven thousand sheep: and the princes had given the people a thousand bullocks, and ten thousand sheep: and a great number of priests was sanctified.
25 Kusanyiko lote la Yuda, pamoja na makuhani na Walawi na watu wote walikuja pamoja kutoka nchi ya Israeli na wale walioishi Yuda—wote wakafurahia.
And all the multitude of Juda with the priests and Levites, and all the assembly, that came out of Israel; and the proselytes of the land of Israel, and that dwelt in Juda were full of joy.
26 Hivyo kulikuwa na furaha kuu katika Yerusalemu, kwa kuwa tangu wakati wa Solomoni mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli, hapakuwa na kitu kama hicho katika Yerusalemu.
And there was a great solemnity in Jerusalem, such as had not been in that city since the time of Solomon the son of David king of Israel.
27 Kisha makuhani, Walawi, wakainuka na kuwabariki watu. Sauti zao zilisikika na maombi yao yakaenda juu mbinguni, sehemu takatifu ambapo Mungu anaishi.
And the priests and the Levites rose up and blessed the people: and their voice was heard: and their prayer came to the holy dwelling place of heaven.

< 2 Nyakati 30 >