< 2 Nyakati 30 >
1 Hzekia akatuma wajumbe kwa Israeli wote na Yuda, na pia akawaandikia barua Efraimu na Manase, kwamba waje kwenye nyumba ya Yahwe katika Yerusalemu, kusherekea Pasaka ya Yahwe, Mungu wa Israeli.
Hezekiah in Israel leh Judah te jouse chu thu athotnin chuleh Ephraim leh Manasseh tejong lekha athotnin Jerusalem ma Pakai houin na hung na dingleh Israel te Pakai kalchuh kut mang dingin akouvin ahi
2 Kwa maana mfalme, viongozi wake, na kusanyiko lote katika Yerusalemu walikuwa wameshauriana pamoja, wakakubaliana kusherekea Pasaka katika mwezi wa pili.
Ajeh chu lengpaleh alamkai ho jouse chuleh Jerusalem ma khop pi – a mipiho jouse chu lhani channa tengleh kalchuh kut manding in akinop to taovin ahi
3 Hawakuweza kuisherekea mapema kabla ya hapo, kwa sababu hapakuwa na makuhani wa kutosha waliojitakasa wenyewe, wala watu hawakuwa wamekusanyika pamoja Yerusalemu.
Amahon ahi ding bangin anamang thei pouvin ahi, chuleh thempu hojong amale ama kithenso na – a ana lhing jou pouvin ahi. Chuleh mipijong Jerusalem mah ana kikhom kim thei pouvin ahi
4 Pendekezo hili likaonekana sahihi katika macho ya mfalme na ya kusanyiko lote.
Hiche thuhin lengpa leh khoppi chu akipa sah lheh jengun ahi
5 Kwa hiyo wakakubaliana kufanya tangazo katika Israeli yote, kuanzia Beer-sheba hadi Dani, kwamba watu lazima waje kusherehekea Paska ya Yahwe, Mungu wa Israeli, huko Yerusalemu. Kwa maana walikuwa hawakuwa wameisherehekea kwa hesabu kubwa ya watu, kwa mujibu wa jinsi ilivyokuwa imeandikwa.
Hitichun amahon Bersheba a patna Dan geija Israel pumpi Jerusalem ma ahung kikhopmu va Israel Pakai Pathen anga sottah ahi ding banga ana manjou tah louvu kalchuh kut man nadingin aphongdoh taovin ahi
6 Hivyo matarishi wakaenda na barua kutoka kwa mfalme na viongozi wake katika Israeli na Yuda yote, kwa agizo la mfalme. wakasema, “Ninyi watu wa Israeli, rudini kwa Yahwe, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Israeli, ili kwamba aweze kuwarudia masalia wenu ninyi mlipona kutoka kwenye mkono wa wafalme wa Ashuru.
Hijou chun Judah leh Israel gampumpi a mikouding asollun leng pa le lamkai ho a kon in lekhathot achoijun lengpa thupeh chu asimphongun “Israel chateho Abraham Isaac le Israel Pakai Pathen na hung kile kittaovin chuteng leh Assyria lenghoa konna hungjamdoh amohcheng nangho komma Pakai jong hung kile kit ding ahi
7 Msiwe kama babu zenu au ndugu zenu, ambao walimuasi Yahwe, Mungu wa mababu zao, hivyo akawaweka katika kuangamia, kama mnavyoona.
Pakai Pathen doumah a chon napu napateo bangin chon hih un nanghon nahet bangun Pathen nin ama ho chu nasahtah in a engbollun ahi
8 Sasa msiwe wasumbufu, kama babu zenu walivyokuwa; badala yake, jitoeni wenyewe kwa Yahwe na njoeni kwenye sehemu yake takatifu, ambayo ameitakasa milele, na mwabuduni Yahwe Mungu wenu, ili kwamba uso wake wenye hasira uwageukie mbali.
Amaho bangin louchal hih un, Pakai thuchu nitjouvin. Jerusalem ma Pakai houinna hungun, hichu na Pakai na Pathennun a imatih channa dinga asuhtheng ahi, hungunlang chibai hungboh un chutileh nachunguvah lung hang taponte
9 Kwa maana ikiwa mtageuka nyuma kwa Yahwe, ndugu zenu na watoto wenu watapata huruma mbele ya hao wanaowaongoza kama wafungwa, na watarudi katika nchi hii. Kwa maana Yahwe Mungu wenu, ni mkarimu na mwenye huruma, na hatawageuzia mbali uso wake, kama mtarudi kwake.”
Pakai komma nahung kileova ahileh na sopite hou galhinga man hochun lungset nale khotona hinnei juntin a in lang uva ahin kile sah diu ahi. Pakai na Pathennu hi mikhoto them ahi nahung kinung leoleh aman nahinsah diu ahi
10 Kwa hiyo matarishi wakapita mji kwa mji katika majimbo ya Efraimu na Manase, njia yote hadi Zabuloni, lakini watu waliwacheka na kuwazomea.
Hiche thupo poleho chu Ephraim leh Manasseh phungho chen na gamhoa acheovin chuleh sahlang Zebulun phungho chenna gamgeijin acheovin ahin la amahon ana nuisatnun ana houseovin ahi
11 Lakini, watu wengine wa Asheri na Manase na Zabuloni walijinyenyekesha wenyewe na wakaja Yerusalemu.
Ahijeng vang'in Asher, Manasseh le Zebulun phunghoa kon in mi phabep Jerusalem mah ahungun ahi
12 Mkono wa Mungu pia ukaja juu ya Yuda, kuwapa moyo mmmoja, ili kulikubali agizo la mfalme na viongozi kwa neno la Yahwe.
Pathenin Judah mite lah a na anatongin ana kipumkhat sahun ahi. Ajeh chu amahon lengpe leh anoija lamkaiho thu angaijun Pathen lungdei boldingin lunggel dettah in aneiyun ahi
13 Watu wengi, kusanyiko kubwa, likakusanyika Yerusalemu kusherehekea Sikukuu ya Mikate Isiyochacha katika mwezi wa pili.
Lhani chan na in mitamtah Jerusalem mah ahung kikhom mun cholsolou changlhah kutchu amangun ahi
14 Waliinuka na kuchukua madhabahu zizilizokuwa Yerusalemu, madhabahu zote kwa ajili ya sadaka za kufukiza; wakazirusha katika kijito Kidroni.
Amahon Jerusalem pumgo thiltona le gimnamtwi lhutnam – a ana kimang maicham ho chu aladoh un Kidron phaicham mah aga lehmangun ahi
15 Kisha wakamuua mwanakondoo wa Paska katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili. Makuhani na Walawi wakaona aibu, kwa hiyo wakajitakasa wenyewe na kuleta sadaka za kuteketezwa katika nyumba ya Yahwe.
Hijouchun lhani channa a ni 14 nikhochun kalchuh kut na dingin kelngoi athatnun ahi. Thempu holeh Levi techu daan dung jui'a ana kisuhtheng lou jeh'un ajahchao vin hijeh chun Pakai jah amaho le amaho aga kisutheng un ahileh houinna pumgo thilto kibolna – a akimangcha thei taovin ahi
16 Wakasimama katika sehemu zao katika makaundi yao, wakifuata maelekezo yaliyotolewa na sheria ya Musa, mtu wa Mungu. Makuhani wakainyunyiza damu waliyoipokea kutoka kwenye mikono ya Walawi.
Aman Pathen mipa Mose daan thupeh dung juiyin ama ama panmuncheh akilo taovin ahi. Levi ten gancha kitohdoh thisan chu thempuho khutna apeovin amahon hichu maicham chungah atheovin ahi
17 Kwa maana walikuwepo wengi katika kusanyikao amaabao hawakuwa wamejitakasa wenyewe. Kwa hiyo Makuhani wakamchinja mwanakondoo wa Pasaka kwa ajili ya kila mmoja ambaye hakuwa amejisafisha na hakuweza kuzitakasa sadaka zake kwa Yahwe.
Mi atamjo chu daan jungjui ja athen lou jeh un kalchuh kutna chun kelngoi athat thei pouvin ahi. Hijeh chun Levi ten amaho khellin athapeh un kelngoi ho chu Pakai jah akatdoh un ahi
18 Kwa kuwa wingi wa watu, wengi wao kutoka Efraimu na Manase, Asakari na Zabuloni, hawakuwa wamejitakasa wenyewe, bado waliula mlo wa Paska, kinyume na maelekezo yaliyoandikwa. Kwa kuwa Hezekia alikuwa amewaombea, akisema, “Mungu Yahwe amsamehe kila mmoja
Hiche chung chonchun Ephraim Manasseh, Issachar leh Zebulun phunghoa konna hungho chun daan dungjuija kisuhtheng nachu abolpouvin hijeh chun amahon kalchuh kutchu kiphalam tah in amangun ahi. Hezekiah lengpan amaho ding chun taona amanpeh in ahi
19 ambaye anaulekeza moyo wake kumtafuta Mungu, Yahwe, Mungu wa babu zake, hata kama hajasafiswa kwa utakaso wa viwango vya patakatifu.”
“Vo Pakai kapu kapateo Pathen naphatna jal in alung thimpum pia nakomma taohohi, daandungjuijin thengjou hih jong leo ataonao sanpeh in” ati
20 Kwa hiyo Yahwe akamsikiliza Hezekia na akawaponya watu.
Pakaiyin Hezekiah taona asangin mipi hochu angaidammin achunguva thilse abol tapon ahi
21 Watu wa Israeli waliokuwepo Yerusalemu wakaitunza Sikukuu ya Mikaate Isiyochachwa na furaha kubwa kwa siku saba. Walawi na makuhani wakamsifu Yahwe siku baada ya siku, wakiimwimbia Yahwe kwa vyombo vya sauti kuu.
Nisagi sungin mipi ho chu Jerusalem mah akikhomun cholsolou changlhah kutchu kipahtah le thanom tah in abollun ani anin Levi te le thempu hochun lungnachim tah in Pakai athangvah un ahi
22 Hezekia akazungumza kwa kuwatia moyo Walawi wote walioilewa ibada ya Yahwe, Kwa hiyo wakala kwa kipindi cha siku saba, wakitoa sadaka za amani, na kufanya toba kwa Yahwe, Mungu wa babu zao.
Hezekiah in Levi techu Pakai chibai bohna – a alamkai thepjeh un apahchan ahi. Nisagi sunga apu apateo Pakai Pathen thangvah na kikatdoh na maicham apeovin ahi
23 Kusanyiko lote kisha likaamua kusherehekea kwa siku zingine saba, na wakafanya hivyo kwa furaha.
Amahon abonchaovin ni sagi lopbe kitdingin anomsoh keijun, hitichun kipahtah in alopbe kit nun ahi
24 Kwa kuwa Hezekia mfalme wa Yuda aliwapa kusanyiko ng'ombe dume elf moja, na kondoo elfu saba kama sadaka; na viongozi wakawapa kusanyiko ng'ombe dume elfu moja na kondoo na mbuzi elfu kumi. Idadi kubwa ya makuhani wakajitakasa wenyewe.
Hezekiah lengpan bongchal 1000 (sangkhat) kelngoichal 7000 (Sang sagi) mipihon akithaova anehdiuvin atohdoh in, chuleh lamkai hon bongchal 1000 (sangkhat) leh kelngoichal 10,000 (sang som) mipiho din atohdoh un, hitichun thempuho tamtah'in daan dungjuija kithensona aneiyun ahi
25 Kusanyiko lote la Yuda, pamoja na makuhani na Walawi na watu wote walikuja pamoja kutoka nchi ya Israeli na wale walioishi Yuda—wote wakafurahia.
Hitichun Judah mipite leh thempu ho Levi te leh sahlanga konna hung mipite leh gamdang miho Israel te leh Judah te lah a anacheng denjing ho abonchaovin akipah sohkeijun
26 Hivyo kulikuwa na furaha kuu katika Yerusalemu, kwa kuwa tangu wakati wa Solomoni mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli, hapakuwa na kitu kama hicho katika Yerusalemu.
Jerusalem khopi chu kipana adimset jengin ahi, Ajeh chu David chapa Solomon lengpa nikho apatnin hitobang hi ana shoh khah hih laijin ahi
27 Kisha makuhani, Walawi, wakainuka na kuwabariki watu. Sauti zao zilisikika na maombi yao yakaenda juu mbinguni, sehemu takatifu ambapo Mungu anaishi.
Thempu hole Leve techun mipi phatthei achan na dingun Pakai kommah ataopeh un ahi leh Pathenin atao naochu asanpeh in ahi