< 2 Nyakati 3 >

1 Kisha Selemani akaanza kuijenga nyumba ya Yahwe katika Yerusalemu juu ya Mlima Moria, ambako Yahwe alimtokea Daudi baba yake. Aliandaa sehemu ambayo Daudi aliikusudia, katika sakafu ya kupuria ya Arauna Myebusi.
Ainsi Salomon commença à bâtir la maison du Seigneur à Jérusalem, sur la montagne de Moria, qui avait été montrée à David, son père, au lieu qu’avait préparé David dans l’aire d’Ornan, le Jébuséen.
2 Alianza kujenga siku ya pili ya mwezi wa pili, katika mwaka wa nne wa utawala wake.
Or il commença à bâtir au second mois, à la quatrième année de son règne.
3 Sasa hivi ndinyo vipimo vya ule msingi ambao Selemani alijenga kwa ajili ya nyumba ya Mungu. Akitumia mtindo wa vipimo vya zamani, urefu ulikuwa mikono sitini, na upana ulikuwa mikono ishirini.
Et voici les fondements que jeta Salomon pour bâtir la maison du Seigneur: il lui donna soixante coudées de longueur, suivant la première mesure, et vingt coudées de largeur.
4 Urefu wa ukumbi mbele ya nyumba ulikuwa mikono ishirini, ukilingana na upana wa nyumba, urefu wake kwenda juu pia ulikuwa mikono ishirini, na Selemani akaifunika sehemu ya ndani kwa dhahabu halisi.
De plus, il bâtit, devant la façade, le portique qui s’étendait selon la mesure de la largeur de la maison, à la longueur de vingt coudées; mais sa hauteur était de cent vingt coudées; et Salomon le fit dorer en dedans d’un or très pur.
5 Akailitengeneza paa la ukumbi mkuu kwa miti ya miberoshi, ambayo aliifunika kwa dhahabu halisi, na ambayo aliifunika kwa miti ya mitende na minyororo.
Il lambrissa aussi la partie de la maison la plus grande d’ais de bois de sapin, et il attacha sur le tout des lames de l’or le plus fin; et il y grava des palmes et comme de petites chaînes entrelacées les unes dans les autres.
6 Akaipamba nyumba kwa vito vya thamani; dhahabu ilikuwa dhahabu kutoka Parvaimu.
Il fit aussi le pavé du temple d’un marbre très précieux, avec beaucoup de décorations,
7 Pia akazifunika boriti zake, vizingiti, kuta, na milango kwa dhahabu; akachonga makerubi juu ya kuta zake.
L’or des lames dont il couvrit la maison, les poutres, les poteaux, les murailles et les portes, était très fin; et il grava des chérubins sur les murailles.
8 Akaijenga sehemu ya patakatifu pa patakatifu. Urefu wake ulilingana na upana wa nyumba, mikono ishirini, na upana wake pia ulikuwa mikono ishirini. Aliifunika kwa dhahabu halisi, thamani yake ilikuwa talanta mia sita.
Il fit aussi la maison du Saint des saints, lui donnant une longueur selon la largeur de la maison, de vingt coudées, et une largeur également de vingt coudées; et il la couvrit de lames d’or, d’environ six cents talents.
9 Uzito wa misumari ulikuwa shekeli hamsini za dhahabu. Alizifunika sehemu za juu kwa dhahabu.
Il fit de plus des clous d’or, de manière que chaque clou pesait cinquante sicles; les chambres d’en haut aussi, il les couvrit d’or.
10 Akachonga makerubi wawili kwa ajili ya sehemu za patakatifu pa patakatifu, wahunzi wakayafunika kwa dhahabu. (Maandishi ya kale yanasema: makerubi wawili waliochongwa kwenye mbao).
Il fit encore dans la maison du Saint des saints deux chérubins, d’un travail de statuaire; et il les couvrit d’or.
11 Mabawa ya makerubi yalikuwa na urefu wa mikono ishirini yote kwa pamoja; bawa la kerubi mmoja lilikuwa na urefu wa mikono mitano, lilifikia kwenye ukuta wa chumba; bawa jingine lilikuwa na urefu wa mikono mitano pia.
Les ailes des chérubins avaient vingt coudées d’étendue, en sorte qu’une aile avait cinq coudées et touchait la muraille de la maison, et que l’autre, qui avait cinq coudées, touchait l’aile de l’autre chérubin.
12 Bawa la kerubi mwingine lilikuwa mikono mitano, likifikia kwenye ukuta wa chumba; bawa lake jingine lilikuwa mikono mitano pia, likigusana na bawa la kerubi wa kwanza.
De même une aile de cet autre chérubin avait cinq coudées, et touchait la muraille; et son autre aile, de cinq coudées, touchait l’aile de l’autre chérubin.
13 Mabawa ya makerubi hawa yalienea jumla ya mikono mitano. Makerubi yalisimama kwa miguu yake, na nyuso zake zikiuelekea ukumbi mkuu.
Ainsi les ailes des deux chérubins étaient déployées, et avaient vingt coudées d’étendue; et ils étaient eux-mêmes droits sur leurs pieds, et leurs faces étaient tournées vers la maison extérieure.
14 Akatengeneza pazia la samawati, dhambarau, na sufu nyekundu, na kitani safi, na akachora makerubi juu yake.
Il fit aussi le voile d’hyacinthe, de pourpre, d’écarlate et de lin fin, et il y tissa des chérubins:
15 Selemani pia akatengeneza nguzo mbili, kila moja ikiwa na urefu wa mikono thelathini na tano kwenda juu, kwa maana mbele ya nyumba; taji ambazo zilikuwa juu ya nguzo zilikuwa na urefu wa mikono mitano kwenda juu.
Et de plus, devant la porte du temple, deux colonnes qui avaient trente-cinq coudées de hauteur; et leurs chapiteaux étaient de cinq coudées.
16 Akatengeneza minyororo kwa ajili ya nguzo na akaiweka juu yake, pia akatengeneza maakomamanga mia moja na akayaunganisha kwenye minyororo.
Il fit de même comme de petites chaînes dans l’oracle, et il les mit sur les chapiteaux des colonnes, ainsi que cent grenades qu’il entrelaça dans les chaînes.
17 Akazisimamisha nguzo mbele ya hekalu, mkono wa kulia, na nyingine mkono wa kushoto; akaiita nguzo ya kulia Yakini, na nguzo ya kushoto akaiita Boazi.
Et les colonnes elles-mêmes, il les mit dans le vestibule du temple, l’une à droite, l’autre à gauche: il appela celle qui était à droite, Jachin, et celle qui était à gauche, Booz.

< 2 Nyakati 3 >