< 2 Nyakati 3 >

1 Kisha Selemani akaanza kuijenga nyumba ya Yahwe katika Yerusalemu juu ya Mlima Moria, ambako Yahwe alimtokea Daudi baba yake. Aliandaa sehemu ambayo Daudi aliikusudia, katika sakafu ya kupuria ya Arauna Myebusi.
Salomon commença à bâtir la maison du Seigneur à Jérusalem, sur le mont Moria; là, le Seigneur était apparu à son père David, qui avait fixé son choix sur l’emplacement lui appartenant dans l’aire d’Ornan, le Jébuséen.
2 Alianza kujenga siku ya pili ya mwezi wa pili, katika mwaka wa nne wa utawala wake.
Il commença la construction le deuxième jour du deuxième mois, dans la quatrième année de son règne.
3 Sasa hivi ndinyo vipimo vya ule msingi ambao Selemani alijenga kwa ajili ya nyumba ya Mungu. Akitumia mtindo wa vipimo vya zamani, urefu ulikuwa mikono sitini, na upana ulikuwa mikono ishirini.
Voici les dimensions adoptées par Salomon comme base de la construction de la maison de Dieu: la longueur, en coudées de l’ancienne mesure, était de soixante coudées, la largeur de vingt coudées.
4 Urefu wa ukumbi mbele ya nyumba ulikuwa mikono ishirini, ukilingana na upana wa nyumba, urefu wake kwenda juu pia ulikuwa mikono ishirini, na Selemani akaifunika sehemu ya ndani kwa dhahabu halisi.
Le portique (qui s’étendait dans le sens de la longueur) avait vingt coudées dans le sens de la largeur de l’édifice; la hauteur en était de cent vingt. Salomon en revêtit l’intérieur d’or pur.
5 Akailitengeneza paa la ukumbi mkuu kwa miti ya miberoshi, ambayo aliifunika kwa dhahabu halisi, na ambayo aliifunika kwa miti ya mitende na minyororo.
La grande enceinte, il la recouvrit de bois de cyprès, auxquels il ajouta un revêtement d’or fin; et il y sculpta des palmes et des festons.
6 Akaipamba nyumba kwa vito vya thamani; dhahabu ilikuwa dhahabu kutoka Parvaimu.
Il garnit l’intérieur de l’édifice de pierres précieuses comme ornement; l’or employé était de l’or de Parvaïm.
7 Pia akazifunika boriti zake, vizingiti, kuta, na milango kwa dhahabu; akachonga makerubi juu ya kuta zake.
Il recouvrit d’or l’édifice, poutres, seuils, parois et battants des portes, et il tailla dans les murs des figures de chérubins.
8 Akaijenga sehemu ya patakatifu pa patakatifu. Urefu wake ulilingana na upana wa nyumba, mikono ishirini, na upana wake pia ulikuwa mikono ishirini. Aliifunika kwa dhahabu halisi, thamani yake ilikuwa talanta mia sita.
Il fit l’enceinte du Saint des Saints, dont la longueur, prise dans le sens de la largeur de l’édifice, était de vingt coudées, la largeur également de vingt coudées. Il la revêtit d’or fin, équivalant à six cents kikkar.
9 Uzito wa misumari ulikuwa shekeli hamsini za dhahabu. Alizifunika sehemu za juu kwa dhahabu.
Le poids de l’or pour les clous fut de cinquante sicles. Il revêtit aussi d’or les chambres hautes.
10 Akachonga makerubi wawili kwa ajili ya sehemu za patakatifu pa patakatifu, wahunzi wakayafunika kwa dhahabu. (Maandishi ya kale yanasema: makerubi wawili waliochongwa kwenye mbao).
Il fit dans l’enceinte du Saint des Saints deux chérubins, artistement sculptés, qu’on recouvrit d’or.
11 Mabawa ya makerubi yalikuwa na urefu wa mikono ishirini yote kwa pamoja; bawa la kerubi mmoja lilikuwa na urefu wa mikono mitano, lilifikia kwenye ukuta wa chumba; bawa jingine lilikuwa na urefu wa mikono mitano pia.
Les ailes des chérubins avaient une longueur (totale) de vingt coudées; l’aile d’un chérubin, longue de cinq coudées, touchait le mur de l’enceinte, et sa seconde aile, longue de cinq coudées, touchait l’aile de l’autre chérubin;
12 Bawa la kerubi mwingine lilikuwa mikono mitano, likifikia kwenye ukuta wa chumba; bawa lake jingine lilikuwa mikono mitano pia, likigusana na bawa la kerubi wa kwanza.
de même, l’aile de l’autre chérubin; longue de cinq coudées, touchait le mur de l’enceinte, et sa seconde aile, longue de cinq coudées, rejoignait l’aile du chérubin correspondant.
13 Mabawa ya makerubi hawa yalienea jumla ya mikono mitano. Makerubi yalisimama kwa miguu yake, na nyuso zake zikiuelekea ukumbi mkuu.
Les ailes de ces chérubins avaient donc une envergure de vingt coudées; quant à eux-mêmes, ils se tenaient debout sur leurs pieds, la face tournée vers l’édifice.
14 Akatengeneza pazia la samawati, dhambarau, na sufu nyekundu, na kitani safi, na akachora makerubi juu yake.
Il fit le voile en étoffes d’azur, de pourpre, de cramoisi et de byssus, et y broda des chérubins.
15 Selemani pia akatengeneza nguzo mbili, kila moja ikiwa na urefu wa mikono thelathini na tano kwenda juu, kwa maana mbele ya nyumba; taji ambazo zilikuwa juu ya nguzo zilikuwa na urefu wa mikono mitano kwenda juu.
Il disposa, en avant du temple, deux colonnes longues de trente-cinq coudées et surmontées d’un chapiteau de cinq coudées.
16 Akatengeneza minyororo kwa ajili ya nguzo na akaiweka juu yake, pia akatengeneza maakomamanga mia moja na akayaunganisha kwenye minyororo.
Il fit des festons en forme de chaînes et les posa sur le sommet des colonnes; il fit cent grenades et les entrelaça dans les festons.
17 Akazisimamisha nguzo mbele ya hekalu, mkono wa kulia, na nyingine mkono wa kushoto; akaiita nguzo ya kulia Yakini, na nguzo ya kushoto akaiita Boazi.
Puis il dressa les colonnes devant le hêkhal, l’une à droite et l’autre à gauche, donna à celle de droite le nom de Yakhin, et à celle de gauche le nom de Boaz.

< 2 Nyakati 3 >