< 2 Nyakati 3 >

1 Kisha Selemani akaanza kuijenga nyumba ya Yahwe katika Yerusalemu juu ya Mlima Moria, ambako Yahwe alimtokea Daudi baba yake. Aliandaa sehemu ambayo Daudi aliikusudia, katika sakafu ya kupuria ya Arauna Myebusi.
[興工建殿]撒羅滿在耶路撒冷,即在他父親達味看見異像的摩黎雅山上,在耶步斯人敖爾難的禾場上,達味所準備的地方,興工建造上主的聖殿。
2 Alianza kujenga siku ya pili ya mwezi wa pili, katika mwaka wa nne wa utawala wake.
撒羅滿在即位後第四年二月興工建造。
3 Sasa hivi ndinyo vipimo vya ule msingi ambao Selemani alijenga kwa ajili ya nyumba ya Mungu. Akitumia mtindo wa vipimo vya zamani, urefu ulikuwa mikono sitini, na upana ulikuwa mikono ishirini.
撒羅滿為建造天主聖殿的基地,按照古尺度計算:長六十肘,寬爾十肘。
4 Urefu wa ukumbi mbele ya nyumba ulikuwa mikono ishirini, ukilingana na upana wa nyumba, urefu wake kwenda juu pia ulikuwa mikono ishirini, na Selemani akaifunika sehemu ya ndani kwa dhahabu halisi.
門廊的長度與聖殿的寬度相等,即二十肘,高二十肘,裏面全貼上純金。
5 Akailitengeneza paa la ukumbi mkuu kwa miti ya miberoshi, ambayo aliifunika kwa dhahabu halisi, na ambayo aliifunika kwa miti ya mitende na minyororo.
大殿裏面先蓋上一層木板,再貼上純金,上面雕刻上棕樹和花環;
6 Akaipamba nyumba kwa vito vya thamani; dhahabu ilikuwa dhahabu kutoka Parvaimu.
又以寶石點綴聖殿,甚是華麗;金子都是帕爾瓦因金。
7 Pia akazifunika boriti zake, vizingiti, kuta, na milango kwa dhahabu; akachonga makerubi juu ya kuta zake.
正殿、棟樑、門限、牆壁,以及門扇,都貼上金子,牆上刻有革魯賓。[至聖所]
8 Akaijenga sehemu ya patakatifu pa patakatifu. Urefu wake ulilingana na upana wa nyumba, mikono ishirini, na upana wake pia ulikuwa mikono ishirini. Aliifunika kwa dhahabu halisi, thamani yake ilikuwa talanta mia sita.
以後,建造了至聖所,長度與聖殿的寬度相等,即二十肘,寬度也是二十肘;內部貼了六百「塔冷通」純金。
9 Uzito wa misumari ulikuwa shekeli hamsini za dhahabu. Alizifunika sehemu za juu kwa dhahabu.
釘子重五十「協刻耳」金子;連樓閣也貼上了金子。
10 Akachonga makerubi wawili kwa ajili ya sehemu za patakatifu pa patakatifu, wahunzi wakayafunika kwa dhahabu. (Maandishi ya kale yanasema: makerubi wawili waliochongwa kwenye mbao).
在至聖所內,以刻工刻了兩個革魯賓,外面包上了黃金;
11 Mabawa ya makerubi yalikuwa na urefu wa mikono ishirini yote kwa pamoja; bawa la kerubi mmoja lilikuwa na urefu wa mikono mitano, lilifikia kwenye ukuta wa chumba; bawa jingine lilikuwa na urefu wa mikono mitano pia.
革魯賓的翅膀,共長二十肘:這邊革魯賓的一個翅膀長五肘,伸至這邊殿牆;另一個翅膀也長五肘,與另一個革魯賓的翅膀相接連。
12 Bawa la kerubi mwingine lilikuwa mikono mitano, likifikia kwenye ukuta wa chumba; bawa lake jingine lilikuwa mikono mitano pia, likigusana na bawa la kerubi wa kwanza.
這一個革魯賓的一個翅膀,也長五肘,伸至那邊殿牆;另一個翅膀也長五肘,與前一個革魯賓的翅膀相接連。
13 Mabawa ya makerubi hawa yalienea jumla ya mikono mitano. Makerubi yalisimama kwa miguu yake, na nyuso zake zikiuelekea ukumbi mkuu.
兩個革魯賓的翅膀都伸開,共長二十肘;他們雙足站立,面向聖殿。
14 Akatengeneza pazia la samawati, dhambarau, na sufu nyekundu, na kitani safi, na akachora makerubi juu yake.
又用藍線、紫線、朱紅線和細麻,作了一帳幔,上面繡上革魯賓。[圓柱]
15 Selemani pia akatengeneza nguzo mbili, kila moja ikiwa na urefu wa mikono thelathini na tano kwenda juu, kwa maana mbele ya nyumba; taji ambazo zilikuwa juu ya nguzo zilikuwa na urefu wa mikono mitano kwenda juu.
他又在殿前造了兩根柱子,共長三十肘;每根柱子頂上有柱帽,高五肘。
16 Akatengeneza minyororo kwa ajili ya nguzo na akaiweka juu yake, pia akatengeneza maakomamanga mia moja na akayaunganisha kwenye minyororo.
又做了類似項鍊的花環,置於柱頭上;又作了一百個石榴,懸在花環上。
17 Akazisimamisha nguzo mbele ya hekalu, mkono wa kulia, na nyingine mkono wa kushoto; akaiita nguzo ya kulia Yakini, na nguzo ya kushoto akaiita Boazi.
把兩根柱子立在殿前,一左一右:右邊的叫雅津,左邊的叫波阿次。

< 2 Nyakati 3 >