< 2 Nyakati 29 >

1 Hezekia alianza kutawala alipokuwa na umri wa miaka ishirini na mitano; alitawala miaka ishini na nane katika Yerusalemu. Jina la mama yake aliitwa Abiya; alikuwa binti wa Zekaria.
Ezéchias avait vingt-cinq ans à son avènement; il régna vingt-neuf ans à Jérusalem; sa mère se nommait Abiyya, fille de Zacharie.
2 Alifanya yaliyoadili katika macho ya Yahwe, kama Daudi baba yake alivyofanya.
Il fit ce qui est droit aux yeux de l’Eternel, absolument comme avait agi David, son aïeul.
3 Katika mwaka wa kwanza wa utawala wake, katika mwezi wa kwanza, Hezekia aliifungua milango ya nyumba ya Yahwe na kuikarabati.
C’Est lui qui, la première année de son règne, le premier mois, rouvrit les portes du temple de l’Eternel et les restaura.
4 Akawaleta ndani makuhani na Walawi, na akawakusanya pamoaja katika uwanda upande wa mashariki.
Il fit venir les prêtres et les Lévites et les réunit à la place orientale.
5 Akawaambia, “Nisikilizeni, ninyi Walawi! Jitakaseni wenyewe, na itakaseni nyumba ya Yahwe, Mungu wa babu zenu, na uondoeni mbali uchafu kutoka kwenye sehemu takatifu.
Puis il leur dit: "Ecoutez-moi, Lévites: à présent, sanctifiez-vous, sanctifiez le temple de l’Eternel, Dieu de vos pères, et faites sortir toute souillure du sanctuaire.
6 Kwa kuwa babu zetu walikosea na kufanya kilichokuwa uovu katika macaho ya Yahwe Mungu wetu; walimsahau, wakageuzia mbali nyuso zao kutoka sehemu ambapo Yahwe anaishi, na kuigeuzia migongo yao.
Car nos pères ont été infidèles et ont fait le mal aux yeux de l’Eternel, notre Dieu; ils l’ont abandonné, ont détourné leur face du sanctuaire de l’Eternel et lui ont tourné le dos.
7 Pia waliifunga milango ya ukumbi nakuziweka nje taa; hawakufukiza uvumba au kutoa sadaka za kuteketezwa katika sehemu takatifu kwa Mungu wa Israeli.
Ils ont même fermé les portes du vestibule, éteint les lampes, n’ont point fait fumer d’encens ni offert d’holocaustes dans le sanctuaire au Dieu d’Israël.
8 Kwa hiyo hasira ya Yahwe ilikuwa imeshuka juu ya Yuda na Yerusalemu, na amewafanya kuwa kitu cha wasiwasi, cha hofu, na cha kudharauriwa, kama mnavyoona kwa macho yenu.
Aussi le courroux de l’Eternel s’est-il abattu sur Juda et Jérusalem, il a fait d’eux un objet d’horreur, de désolation et de raillerie comme vous le constatez de vos yeux.
9 Hii ndiyo maana mababu zetu wameanguka kwa upanga, na wana wetu, binti zetu, na wake zetu wako katika utumwa kwa sababu ya hili.
Et voyez: nos pères sont tombés sous le glaive, nos fils, nos filles et nos femmes ont été emmenés captifs à cause de cela.
10 Sasa ni katika moyo wangu kufanya agano na Yahwe, Mungu wa Israeli, ili kwamba hasira yake kali iweze kugeukia mbali nasi.
Maintenant j’ai à cœur de contracter alliance avec l’Eternel, Dieu d’Israël, pour qu’il détourne de nous la flamme de sa colère.
11 Wanangu, msiwe wavivu sas, kwa kuwa Yahwe amewachagua kwa ajili ya kusimama mbe yake, kwa ajili ya kumwabudu yeye, na kwamba muwe watumishi wake na kufukiza uvumba.”
O mes fils, à présent point de négligence, car c’est de vous que l’Eternel a fait choix pour vous tenir prêts devant lui à le servir, pour être ses ministres et lui offrir l’encens."
12 Basi Walawi wakainuka; Mahathi mwana wa Amasai, na Yoeli mwana wa Azaria, wa watu wa Kohathi; na wa watu wa Merari, Kishi mwana wa Abdi, na Azaria mwana wa Yehaleleli; na wa Wargeshoni, Yoa mwana wa Zimna, na Edeni mwana wa Yoa;
Alors se levèrent les Lévites, Mahat, fils d’Amachaï, Joël, fils d’Azariahou, des enfants de Kehat; des enfants de Merari, Kich, fils d’Abdi, et Azariahou, fils de Yehallélel; des Gersonites, Yoah, fils de Zimma, et Eden, fils de Yoah;
13 wa wana wa Elisafani, Shimri na Yeueli; wa wana wa Asafu, Zekaria na Matania;
des enfants d’Eliçafan, Chimri et Yeïêl; des enfants d’Assaph, Zacharie et Mattanyahou;
14 wa wana wa Hemani, Yehueli na Shimei; na wa wana Yeduthuni, Shemaya na Uzieli.
des enfants de Hêman, Yehïêl et Chimeï, et des enfants de Yedoutoun, Chemaya et Ouzziêl.
15 Wakawakusanya ndugu zao, wakajitakasa wenyewe, na wakaenda ndani, kama alivyoamru mfalme, wakifuata maneno ya Yahwe, kwa ajili ya kuisafisha nyumba ya Yahwe.
Ils rassemblèrent leurs frères, se sanctifièrent et vinrent selon l’ordre du roi, conforme aux prescriptions de l’Eternel, pour purifier le temple de l’Eternel.
16 Makuhani wakaenda kwenye sehemu za ndani ya nyumba ya Yahwe kwa ajili ya kuisafisha; wakaleta nje uchafu wote walioukuta ndani ya hekalu la Yahwe katika uwanja wa nyumba. Walawi wakauchukua kuubeba nje ya hadi kwnye kijito cha Kidroni.
Les prêtres pénétrèrent à l’intérieur du temple de l’Eternel pour le purifier; ils rejetèrent dans le parvis du temple de l’Eternel toutes les impuretés qu’ils trouvèrent dans le sanctuaire de l’Eternel, et les Lévites les reçurent pour les transporter dehors au ravin du Cédron.
17 Sasa wakaanza utakaso katika siku ya kwanza ya mwezi. Katika siku ya nane ya mwezi wakaufikia ukumbi wa Yahwe. Kisha siku nane zaidi wakaitakasa nyumba ya Yahwe. Katika siku ya kumi na sita ya mwezi wa kwanza wakamaliza.
Ils commencèrent cette sanctification le premier du premier mois, et le huitième jour du mois ils vinrent dans le vestibule de l’Eternel et sanctifièrent le temple de l’Eternel en huit jours; ce fut le seizième jour du premier mois qu’ils terminèrent.
18 Kisha wakaenda kwa Hezekia, mfalme, ndani ya ikulu na kusema, “Tumeisafisha nyumba yote ya Yahwe, madhabahu kwa ajili ya kutolea sadaka za kuteketezwa pamoja na vifaa vyake vyote, na meza ya mkate wa uwepo, pamoja na vifaa vyake vyote.
Puis, ils vinrent à l’intérieur auprès du roi Ezéchias et lui dirent: "Nous avons purifié tout le temple de l’Eternel, l’autel des holocaustes avec tous ses ustensiles, et la table de proposition avec tous ses ustensiles.
19 Kwa hiyo tumejiandaa na tumevitakasa vitu vyote ambavyo Mfalme Ahazi aliviondoa wakati alipoenda kwa ukengeufu katika kipindi cha utawala wake, ona, viko mbele ya madhabahu ya Yahwe.”
Tous les ustensiles que le roi Achaz avait écartés durant son règne, dans son infidélité, nous les avons réparés et consacrés, et ils se trouvent maintenant devant l’autel du Seigneur."
20 Kisha Hezekia mfalme akaamka mapema asubuhi na kuwakusanya viongozi wa miji; akaenda kwenye nyumba ya Yahwe.
Le roi Ezéchias se leva de bon matin, assembla les chefs de la ville, et monta au temple de l’Eternel.
21 Wakaleta ng'ombe waume saba, kondoo waume saba, wanakondoo saba, mbuzi waume saba kama sadaka ya dhambi kwa ajili ya mfalme, kwa ajili ya patakatifu, kwa ajili ya Yuda. Akawaamuru makuhani, wana wa Haruni, kuwatoa sadaka juu ya madhabahu ya Yahwe.
On amena sept taureaux, sept béliers, sept agneaux et sept boucs expiatoires pour la royauté, pour le sanctuaire et pour Juda, et il prescrivit aux prêtres de la famille d’Aaron de les offrir sur l’autel de l’Eternel.
22 Kwa hiyo wakawachinja ng'ombe, na makuhani wakaipokea damu na kuinyunyiza juu ya madhabahu. Wakawachinja kondoo dume, na kunyunyiza damu juu ya madhabahu; Pia wakawachinja wanakondoo na kuinyunyiza damu juu ya madhabahu.
Alors ils immolèrent les taureaux, et les prêtres reçurent le sang et en aspergèrent l’autel. Ils immolèrent les béliers et lancèrent le sang sur l’autel. Ils immolèrent les agneaux et lancèrent le sang sur l’autel.
23 Wakawaleta mbuzi kwa ajili ya sadka ya dhambi mbele ya mfalme na kusnyiko; wakaweka mikono yao juu ya hao mbuzi.
Puis ils amenèrent les boucs expiatoires devant le roi et le peuple et imposèrent leurs mains sur eux.
24 Makuhani wakawachinja, na wakafanya sadaka ya dhambi kwa damu yao juu ya madhabahu ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Israeli wote, kwa maana mfalme alikuwa ameamuru kuwa sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya dhambi lazima zifanywe kwa ajili ya Israeli wote.
Les prêtres les immolèrent et offrirent leur sang sur l’autel pour faire propitiation sur tout Israël, car c’est pour tout Israël que le roi avait prescrit l’holocauste et l’expiatoire.
25 Hezekia akawaweka Walawi katika nyumba ya Yahwe wakiwa na matoazi, vinanda, na vinubi, akiwapanga kwa amri ya Daaudi, Gadi, mwonaji wa mfalme, na Nathani, nabii, kwa maana amri ilitoka kwa Yahwe kupitia manabii wake.
Il posta les Lévites dans le temple de l’Eternel avec des cymbales, des luths et des harpes, selon l’ordonnance de David, de Gad, Voyant du roi, et du prophète Nathan, car l’ordre en avait été donné par Dieu, par l’entremise de ses prophètes.
26 Walawi wakasimama na vyombo vya Daudi, na makauhani wakasimama na matarumbeta.
Les Lévites se tinrent avec les instruments de David, et les prêtres avec les trompettes.
27 Hezekia akawaamuru kutoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu. Sadaka zilipoanza, wimbo wa Yahwe ukaanza pia, kwa matarumbeta, pamoja na vyombo vya Daudi, mfalme wa Israeli.
Puis, Ezéchias ordonna d’offrir l’holocauste sur l’autel, et en même temps que l’holocauste commencèrent le cantique à l’Eternel et les trompettes, avec accompagnement des instruments de David, roi d’Israël.
28 Kusanyiko lote wakaabudu, waimbaji wakaimba, na wapiga matarumbeta wakapiga; yote hayo yakaendele hadi sadaka za kuteketezwa zilizipokwisha.
Toute l’assemblée se prosternait, les chants s’élevaient, et les trompettes sonnaient, tout cela jusqu’à l’achèvement de l’holocauste.
29 Walipomaliza kutoa sadaka, mfalme na watu waliokuwepo pamoja naye wakainama, na kusujudu.
Dès que fut terminé l’holocauste; le roi et tous ceux qui étaient avec lui fléchirent les genoux et se prosternèrent.
30 Vile vile, Hezekia, mfalme, na viongozi wakawaamuru Walawi kuimba ili kumsifu Yahwe kwa maneno ya Daudi na ya Asafu, mwonaji. Wakaimba sifa kwa furaha, wakainama chini wakasujudu.
Alors le roi Ezéchias et les chefs ordonnèrent aux Lévites de louer le Seigneur sur les paroles de David et d’Assaph, le Voyant, et ils chantèrent avec allégresse, s’inclinèrent et se prosternèrent.
31 Kisha Hezekia akasema, “Sasa mmejiweka wakfu wenyewe kwa Yahwe. Njoni hapa na mlete sadaka na dhabihu za shukrani katika nyumba ya Yahwe.” Kusanyiko wakaleta sadka na dhabihu za shukrani, na wote waliaokuwa na moyo wa kuhiyalika wakaleta sadka za kuteketezwa.
Puis Ezéchias prit la parole et dit: "Maintenant, vous vous êtes consacrés à l’Eternel, approchez et offrez des victimes et des sacrifices d’actions de grâces dans le temple de l’Eternel", et l’assemblée offrit des victimes et des sacrifices d’actions de grâces, et, selon les libéralités, des holocaustes.
32 Hesabu ya sadaka za kuteketezwa ambazo kusanyiko walileta ilikuwa ng'ombe sabini, kondoo waume mia moja, na wanakondo waume mia mbili. Wote hao walikuwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa Yahwe.
Le nombre des holocaustes qu’offrit l’assemblée fut de soixante-dix têtes de gros bétail, cent béliers, deux cents agneaux; tout cela fut offert en holocauste à l’Eternel.
33 Sadaka za kuwekwa wakfu zilikuwa ng'ome mia sita na kondoo elfu tatu.
Les autres sacrifices furent de six cents têtes de gros et de trois mille têtes de menu bétail.
34 Lakini makuhani walikuwa wachache sana kuchuna sadaka zote za kuteketezwa, kwa hiyo ndgugu zao, Walawi, wakawasaidia hadi kazi ilipoisha, na hadi makuhani walipoweza kujitakasa wenyewe, kwa maana Walawi walikuwa makaini sana kujitaksa wenyewe kuliko makuhani.
Seulement les prêtres furent en trop petit nombre et ils ne purent dépouiller tous les holocaustes; ils furent secondés par leurs frères, les Lévites, jusqu’à ce que fût achevée la besogne et que les prêtres se fussent purifiés, car les Lévites étaient plus consciencieux pour se sanctifier que les prêtres.
35 Zaidi ya hayo, palikuwa na sadaka za kuteketezwa nyingi sana; zilitolewa pamoja na sadaka za mafauta za amani, na kulikuwa na sadaka za vinywaji kwa kila sadaka ya kuteketezwa. Kwa hiyo huduma ya nyumba ya Yahwe ikawekwa katika utaratibu.
Il y eut aussi quantité d’holocaustes avec les graisses des sacrifices rémunératoires et avec les libations des holocaustes. Ainsi fut rétabli le service du temple de l’Eternel.
36 Hezekia akafurahia, na watu pia, kwa sababu ya kile ambacho Mungu alikuwa ameandaa kwa ajili ya watu, kwa maana kazi ilikuwa imekamilika haraka.
Ezéchias et tout le peuple se réjouirent de ce que Dieu eût agi en faveur du peuple, car la chose se fit rapidement.

< 2 Nyakati 29 >