< 2 Nyakati 29 >
1 Hezekia alianza kutawala alipokuwa na umri wa miaka ishirini na mitano; alitawala miaka ishini na nane katika Yerusalemu. Jina la mama yake aliitwa Abiya; alikuwa binti wa Zekaria.
Hezekiah he became king a son of twenty and five year[s] and twenty and nine year[s] he reigned in Jerusalem and [the] name of mother his [was] Abijah [the] daughter of Zechariah.
2 Alifanya yaliyoadili katika macho ya Yahwe, kama Daudi baba yake alivyofanya.
And he did the right in [the] eyes of Yahweh according to all that he had done David ancestor his.
3 Katika mwaka wa kwanza wa utawala wake, katika mwezi wa kwanza, Hezekia aliifungua milango ya nyumba ya Yahwe na kuikarabati.
He in the year first of reigning his in the month first he opened [the] doors of [the] house of Yahweh and he repaired them.
4 Akawaleta ndani makuhani na Walawi, na akawakusanya pamoaja katika uwanda upande wa mashariki.
And he brought the priests and the Levites and he gathered them to [the] open place of the east.
5 Akawaambia, “Nisikilizeni, ninyi Walawi! Jitakaseni wenyewe, na itakaseni nyumba ya Yahwe, Mungu wa babu zenu, na uondoeni mbali uchafu kutoka kwenye sehemu takatifu.
And he said to them listen to me O Levites now consecrate yourselves and consecrate [the] house of Yahweh [the] God of ancestors your and bring out the impurity from the holy place.
6 Kwa kuwa babu zetu walikosea na kufanya kilichokuwa uovu katika macaho ya Yahwe Mungu wetu; walimsahau, wakageuzia mbali nyuso zao kutoka sehemu ambapo Yahwe anaishi, na kuigeuzia migongo yao.
For they acted unfaithfully fathers our and they did the evil in [the] eyes of Yahweh God our and they forsook him and they turned faces their away from [the] tabernacle of Yahweh and they gave a back.
7 Pia waliifunga milango ya ukumbi nakuziweka nje taa; hawakufukiza uvumba au kutoa sadaka za kuteketezwa katika sehemu takatifu kwa Mungu wa Israeli.
Also they shut [the] doors of the porch and they extinguished the lamps and incense not they made smoke and burnt offering[s] not they offered up in the holy place to [the] God of Israel.
8 Kwa hiyo hasira ya Yahwe ilikuwa imeshuka juu ya Yuda na Yerusalemu, na amewafanya kuwa kitu cha wasiwasi, cha hofu, na cha kudharauriwa, kama mnavyoona kwa macho yenu.
And it was [the] wrath of Yahweh towards Judah and Jerusalem and he has made them (into a terror *Q(K)*) into a horror and into a hissing just as you [are] seeing with own eyes your.
9 Hii ndiyo maana mababu zetu wameanguka kwa upanga, na wana wetu, binti zetu, na wake zetu wako katika utumwa kwa sababu ya hili.
And there! they have fallen fathers our by the sword and sons our and daughters our and wives our [are] in captivity on this.
10 Sasa ni katika moyo wangu kufanya agano na Yahwe, Mungu wa Israeli, ili kwamba hasira yake kali iweze kugeukia mbali nasi.
Now [is] with heart my to make a covenant to Yahweh [the] God of Israel and it may turn back from us [the] burning of anger his.
11 Wanangu, msiwe wavivu sas, kwa kuwa Yahwe amewachagua kwa ajili ya kusimama mbe yake, kwa ajili ya kumwabudu yeye, na kwamba muwe watumishi wake na kufukiza uvumba.”
O sons my now may not you be negligent for you he has chosen Yahweh to stand before him to serve him and to be of him servants and makers of smoke.
12 Basi Walawi wakainuka; Mahathi mwana wa Amasai, na Yoeli mwana wa Azaria, wa watu wa Kohathi; na wa watu wa Merari, Kishi mwana wa Abdi, na Azaria mwana wa Yehaleleli; na wa Wargeshoni, Yoa mwana wa Zimna, na Edeni mwana wa Yoa;
And they arose the Levites Mahath [the] son of Amasai and Joel [the] son of Azariah of [the] descendants of the Kohathite[s] and of [the] descendants of Merari Kish [the] son of Abdi and Azariah [the] son of Jehallelel and of the Gershonite[s] Joah [the] son of Zimmah and Eden [the] son of Joah.
13 wa wana wa Elisafani, Shimri na Yeueli; wa wana wa Asafu, Zekaria na Matania;
And of [the] descendants of Elizaphan Shimri (and Jeiel *Q(K)*) and of [the] descendants of Asaph Zechariah and Mattaniah.
14 wa wana wa Hemani, Yehueli na Shimei; na wa wana Yeduthuni, Shemaya na Uzieli.
And of [the] descendants of Heman (Jehiel *Q(K)*) and Shimei. And of [the] descendants of Jeduthun Shemaiah and Uzziel.
15 Wakawakusanya ndugu zao, wakajitakasa wenyewe, na wakaenda ndani, kama alivyoamru mfalme, wakifuata maneno ya Yahwe, kwa ajili ya kuisafisha nyumba ya Yahwe.
And they gathered relatives their and they consecrated themselves and they went according to [the] command of the king by [the] words of Yahweh to cleanse [the] house of Yahweh.
16 Makuhani wakaenda kwenye sehemu za ndani ya nyumba ya Yahwe kwa ajili ya kuisafisha; wakaleta nje uchafu wote walioukuta ndani ya hekalu la Yahwe katika uwanja wa nyumba. Walawi wakauchukua kuubeba nje ya hadi kwnye kijito cha Kidroni.
And they went the priests to within [the] house of Yahweh to cleanse [it] and they brought out all the uncleanness which they found in [the] temple of Yahweh to [the] court of [the] house of Yahweh and they received [it] the Levites to bring [it] out to [the] wadi of Kidron [the] outside towards.
17 Sasa wakaanza utakaso katika siku ya kwanza ya mwezi. Katika siku ya nane ya mwezi wakaufikia ukumbi wa Yahwe. Kisha siku nane zaidi wakaitakasa nyumba ya Yahwe. Katika siku ya kumi na sita ya mwezi wa kwanza wakamaliza.
And they began on [day] one of the month first to consecrate and on day eight of the month they came to [the] porch of Yahweh and they consecrated [the] house of Yahweh for days eight and on day six-teen of the month first they finished.
18 Kisha wakaenda kwa Hezekia, mfalme, ndani ya ikulu na kusema, “Tumeisafisha nyumba yote ya Yahwe, madhabahu kwa ajili ya kutolea sadaka za kuteketezwa pamoja na vifaa vyake vyote, na meza ya mkate wa uwepo, pamoja na vifaa vyake vyote.
And they went within to Hezekiah the king and they said we have cleansed all [the] house of Yahweh [the] altar of the burnt offering and all utensils its and [the] table of the row and all utensils its.
19 Kwa hiyo tumejiandaa na tumevitakasa vitu vyote ambavyo Mfalme Ahazi aliviondoa wakati alipoenda kwa ukengeufu katika kipindi cha utawala wake, ona, viko mbele ya madhabahu ya Yahwe.”
And all the utensils which he had rejected the king Ahaz in reign his in unfaithfulness his we have prepared and we have consecrated and there they [are] before [the] altar of Yahweh.
20 Kisha Hezekia mfalme akaamka mapema asubuhi na kuwakusanya viongozi wa miji; akaenda kwenye nyumba ya Yahwe.
And he rose early Hezekiah the king and he gathered [the] officials of the city and he went up [the] house of Yahweh.
21 Wakaleta ng'ombe waume saba, kondoo waume saba, wanakondoo saba, mbuzi waume saba kama sadaka ya dhambi kwa ajili ya mfalme, kwa ajili ya patakatifu, kwa ajili ya Yuda. Akawaamuru makuhani, wana wa Haruni, kuwatoa sadaka juu ya madhabahu ya Yahwe.
And they brought young bulls seven and rams seven and lambs seven and he-goats of goats seven to a sin offering on the kingdom and on the sanctuary and on Judah and he said to [the] descendants of Aaron the priests to offer up on [the] altar of Yahweh.
22 Kwa hiyo wakawachinja ng'ombe, na makuhani wakaipokea damu na kuinyunyiza juu ya madhabahu. Wakawachinja kondoo dume, na kunyunyiza damu juu ya madhabahu; Pia wakawachinja wanakondoo na kuinyunyiza damu juu ya madhabahu.
And they slaughtered the cattle and they took the priests the blood and they sprinkled [it] the altar towards and they slaughtered the rams and they sprinkled the blood the altar towards and they slaughtered the lambs and they sprinkled the blood the altar towards.
23 Wakawaleta mbuzi kwa ajili ya sadka ya dhambi mbele ya mfalme na kusnyiko; wakaweka mikono yao juu ya hao mbuzi.
And they brought near [the] goats of the sin offering before the king and the assembly and they laid hands their on them.
24 Makuhani wakawachinja, na wakafanya sadaka ya dhambi kwa damu yao juu ya madhabahu ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Israeli wote, kwa maana mfalme alikuwa ameamuru kuwa sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya dhambi lazima zifanywe kwa ajili ya Israeli wote.
And they slaughtered them the priests and they made a sin offering blood their the altar towards to make atonement on all Israel for for all Israel he had said the king the burnt offering and the sin offering.
25 Hezekia akawaweka Walawi katika nyumba ya Yahwe wakiwa na matoazi, vinanda, na vinubi, akiwapanga kwa amri ya Daaudi, Gadi, mwonaji wa mfalme, na Nathani, nabii, kwa maana amri ilitoka kwa Yahwe kupitia manabii wake.
And he stationed the Levites [the] house of Yahweh with cymbals with lyres and with harps by [the] command of David and Gad [the] seer of the king and Nathan the prophet for [was] by [the] hand of Yahweh the commandment by [the] hand of prophets his.
26 Walawi wakasimama na vyombo vya Daudi, na makauhani wakasimama na matarumbeta.
And they stood the Levites with [the] instruments of David and the priests with trumpets.
27 Hezekia akawaamuru kutoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu. Sadaka zilipoanza, wimbo wa Yahwe ukaanza pia, kwa matarumbeta, pamoja na vyombo vya Daudi, mfalme wa Israeli.
And he said Hezekiah to offer up the burnt offering to the altar and at [the] time [when] it began the burnt offering it began [the] song of Yahweh and the trumpets and on [the] hands of [the] instruments of David [the] king of Israel.
28 Kusanyiko lote wakaabudu, waimbaji wakaimba, na wapiga matarumbeta wakapiga; yote hayo yakaendele hadi sadaka za kuteketezwa zilizipokwisha.
And all the assembly [were] bowing down and the song [was] singing and the trumpets ([were] blowing a trumpet *Q(k)*) everything until was complete the burnt offering.
29 Walipomaliza kutoa sadaka, mfalme na watu waliokuwepo pamoja naye wakainama, na kusujudu.
And just as finished to offer up they bowed down the king and all those [who] were found with him and they bowed down.
30 Vile vile, Hezekia, mfalme, na viongozi wakawaamuru Walawi kuimba ili kumsifu Yahwe kwa maneno ya Daudi na ya Asafu, mwonaji. Wakaimba sifa kwa furaha, wakainama chini wakasujudu.
And he said Hezekiah the king and the officials to the Levites to praise Yahweh with [the] words of David and Asaph the seer and they praised to to joy and they bowed low and they bowed down.
31 Kisha Hezekia akasema, “Sasa mmejiweka wakfu wenyewe kwa Yahwe. Njoni hapa na mlete sadaka na dhabihu za shukrani katika nyumba ya Yahwe.” Kusanyiko wakaleta sadka na dhabihu za shukrani, na wote waliaokuwa na moyo wa kuhiyalika wakaleta sadka za kuteketezwa.
And he answered Hezekiah and he said now you have filled hand your to Yahweh draw near and bring sacrifices and thank-offerings to [the] house of Yahweh and they brought the assembly sacrifices and thank-offerings and every [person] willing of heart burnt offerings.
32 Hesabu ya sadaka za kuteketezwa ambazo kusanyiko walileta ilikuwa ng'ombe sabini, kondoo waume mia moja, na wanakondo waume mia mbili. Wote hao walikuwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa Yahwe.
And it was [the] number of the burnt offering[s] which they brought the assembly cattle seventy rams one hundred lambs two hundred [were] for a burnt offering to Yahweh all these.
33 Sadaka za kuwekwa wakfu zilikuwa ng'ome mia sita na kondoo elfu tatu.
And the holy offerings [were] cattle six hundred and sheep three thousand.
34 Lakini makuhani walikuwa wachache sana kuchuna sadaka zote za kuteketezwa, kwa hiyo ndgugu zao, Walawi, wakawasaidia hadi kazi ilipoisha, na hadi makuhani walipoweza kujitakasa wenyewe, kwa maana Walawi walikuwa makaini sana kujitaksa wenyewe kuliko makuhani.
Only the priests they were to fewness and not they were able to skin all the burnt offerings and they helped them relatives their the Levites until was complete the work and until they had consecrated themselves the priests for the Levites [were] upright of heart to consecrate themselves more than the priests.
35 Zaidi ya hayo, palikuwa na sadaka za kuteketezwa nyingi sana; zilitolewa pamoja na sadaka za mafauta za amani, na kulikuwa na sadaka za vinywaji kwa kila sadaka ya kuteketezwa. Kwa hiyo huduma ya nyumba ya Yahwe ikawekwa katika utaratibu.
And also burnt offering[s] to abundance with [the] fat of the peace offerings and with the drink offerings of the burnt offering and it was arranged [the] service of [the] house of Yahweh.
36 Hezekia akafurahia, na watu pia, kwa sababu ya kile ambacho Mungu alikuwa ameandaa kwa ajili ya watu, kwa maana kazi ilikuwa imekamilika haraka.
And he rejoiced Hezekiah and all the people on what he had prepared God for the people for in suddenness it had happened the thing.