< 2 Nyakati 28 >

1 Ahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, na akatawala miaka kumi na sita katika Yerusalemu. Hakufanya yaliyoadili katika macho ya Yahwe, kama Daudi babu yake alivyokuwa amefanya.
Ahaz was 20 years old when he became the king [of Judah]. He ruled from Jerusalem for 16 years. His ancestor King David was a good king, but Ahaz was not like David. He constantly disobeyed Yahweh
2 Badala yake, alitembea katika njia za wafalme wa Israeli; pia alitengeneza sanamu za kusubu kwa ajila ya Mabaali.
and was as sinful as the kings of Israel had been. He made idols of the god Baal.
3 Zaidi ya hayo, akafukiza uvumba katika bonde la Beni Hinomu na akawaweka watoto wake ndani ya moto, kwa mjibu wa desturi za uzinzi za watu ambao Yahwe aliwafukuza nje ya nchi zao mbele za watu wa Israeli.
He burned incense in Hinnom Valley. He even [killed some of] his own sons [and] offered [them] as sacrifices to be completely burned. That imitated the disgusting customs of the people-groups who previously lived there, people whom Yahweh had expelled as the Israelis advanced through the land.
4 Akatoa sadaka na kufukiza uvumba katika sehemu za juu na juu ya vilima na chini ya kila mti wenye majani mabichi.
Ahaz offered sacrifices [to idols] at shrines on hilltops and under every big green tree.
5 Kwa hiyo Yahwe Mungu wa Ahazi, akamweka katika mikono ya mfalme wa Shamu. Waaramu wakamshinda na kuchukua kutoka kwake kundi kubwa la mateka, wakawapeleka Damesiki. Ahazi pia aliwekwa katika mikono ya mfalme wa Israeli ambaye alimshinda kwa mauji makuu.
Therefore Yahweh his God allowed his army to be defeated by the army of the king of Syria. They captured many soldiers of Judah and took them as prisoners to Damascus. The army of the king of Israel also defeated the army of Judah and killed very many of their soldiers.
6 Kwa maana Peka mwana wa Remalia, aliwaua katika Yuda wanajeshi 120, 00 kwa siku moja, wote walikuwa wanaume hodari, kwa maana walikuwa wamemsahau Yahwe, Mungu wa babu zao.
In one day the army of Remaliah’s son, King Pekah [of Israel], killed 120,000 soldiers in Judah. That happened because [the people of] Judah had abandoned Yahweh, the God whom their ancestors [worshiped].
7 Zikri, mtu mwenye nguvu kutoka Efraimu, akawaua Maaseya mwana wa mfalme, Azrikamu, mwangalizi mkuu wa ikulu, na Elkana, ambaye alikuwa karibu na mfalme.
Zicri, a warrior from the tribe of Ephraim, killed king Ahaz’s son Maaseiah, Azrikam the officer in charge of the palace, and Elkanah, the king’s assistant.
8 Jeshsi la Israeli likachukua mateka kutoka kwa ndugu zao 200, 000 wake, wana, na mabinti. Pia wakachukua nyara nyingi, ambazo walipeleka Samaria.
The soldiers of Israel captured 200,000 of the people of Judah, including many wives and sons and daughters [of the soldiers of Judah]. They also seized and took back to Samaria many valuable things.
9 Lakini nabii wa Yahwe alikuwapo huko, jina lake aliitwa Odedi. Alikwenda nje kukutana na jeshi likiingia Samaria. Akawaambia, “Kwa sababu Yahwe, Mungu wa babu zenu, alikuwa na hasiri na Yuda, akawatia katika mikono yenu. Lakini mmewaua katika hasira inayofika juu mbinguni.
But a prophet of Yahweh whose name was Obed was there [in Samaria]. He went out of the city to meet the army when it returned to Samaria. He said to them, “Because Yahweh, the God whom your ancestors [belonged to], was angry with [the people of] Judah, he allowed you to defeat them. But God has seen the cruel way that you slaughtered them.
10 Sasa ninyi badala ya kuwahifadhi wanaume na wanawake wa Yuda na Yerusalemu kama watumwa wenu. Lakini je hamko na hatia ya dhambi zenu zidi ya Yahwe Mungu wenu?
And now you want to [sin by] causing men and women from Judah to become your slaves, but you have certainly also sinned against Yahweh our God!
11 Sasa basi, nisikilizeni: warudisheni wafubgwa, ambao mmewachukua wa ndugu zenu, kwa maana ghadhabu ya Yahwe iko juu yenu.”
So listen to me! Send back [to Judah] your fellow-countrymen whom you have captured, because Yahweh is extremely angry with you [for what you did to them].”
12 Kisha baadhi ya viongozi wa watu wa Efraimu—Azaria mwana wa Yohanani, Berekia mwana wa Meshiremothi, na Yehizikia mwana wa Shalumu, na Amasa mwana wa Hadlai, wakasimama kinyume na wale waliorudi kutoka vitani.
Then some of the leaders of [the tribe of] Ephraim—Azariah the son of Jehohanan, Berekiah the son of Meshillemoth, Jehizkiah the son of Shallum, and Amasa the son of Hadlai—rebuked those who were returning from the battle.
13 Wakasema kwao, “Lazimaa msiwaleta wafungwa hapa, kwa kuwa mlikusudia jambo ambalo litaleta juu yetu dhambi dhidi ya Yahwe, kuongeza dhambi juu yetu na makosa yetu, kwa maana makosa yetu ni makuu, na kuna hasira kali dhidi ya Israeli.”
They said to them, “You must not bring those prisoners here! If you do that, Yahweh will consider that we are guilty of sinning. We are already guilty of committing many sins; do you want to cause us to be even more guilty by committing another sin? God is already very angry with [us people of] Israel!”
14 Hivyo watu wenye silaha wakawaacha wafungwa na mateka mbele ya viongozi wa Israeli na kusanyiko lote
So, while their leaders and others were watching, the soldiers released the prisoners, and also gave back to them the valuable things that they had captured.
15 Watu ambao walipangwa kwa majina wakanyanyuka na kuwachukua wafungwa, na kuwavika wote waliokuwa uchi miongoni mwa mateka. Wakawavika na kuwapa viatu. Wakawapa chakula wale na kunywa. Wakawahudumia majeraha yao na kuwaweka waliodhaifu juu ya punda. Wakawarudisha kwenye familia zao katika Yeriko, (Ulioitwa mji wa mitende). Kisha wakarudi Samaria.
The leaders who were selected took some of the clothes that the soldiers had taken from the prisoners and gave those clothes back to the people who were naked. They also gave to the prisoners sandals and other clothes and things to eat and drink, and they gave them olive oil to rub on their wounds. They gave donkeys to those who were very weak, in order that they could ride on them. Then they led them all to Jericho, the city that had many palm trees. Then those leaders [of Israel] returned to Samaria.
16 Wakati huo Mfalme Ahazi akatuma wajumbe kwa wafalme wa Ashuru kuwaomba wamsaidie.
About that time, King Ahaz sent [a message] to the king of Assyria requesting help.
17 Kwa maana Waedomu walikuwa wamekuja tena na kuvamia Yuda, wakachukua wafungwa.
[He did that because the army from] the Edom people-group had come again and attacked Judah and taken away many of the people of Judah as prisoners.
18 Wafilisti pia wakavamia miji ya nchi ya chini na ya Negebu ya Yuda. Waliichukua Beth-shemeshi, Ayaloni, Giderothi, SoKo pamoja na vijiji vyake, Timna pamoja na vijiji vyake. Wakaenda kuishi katika sehemu hizo.
At the same time, men from Philistia had raided/attacked towns in the foothills and in the southern desert of Judah. They had captured Beth-Shemesh, Aijalon, and Gederoth [cities], as well as Soco, Timnah and Gimzo [towns] and the nearby villages.
19 Kwa kuwa Yahwe aliishusha chini Yuda kwa sababu ya Ahazi, mfalme wa Israeli; kwa maana alikuwa ametenda maovu katika Yuda na alikuwa ametenda dhambi nzito sana dhidi ya Yahwe.
Yahweh [allowed those things to happen in order to] humble king Ahaz, because he had encouraged the people of Judah to do wicked things and had disobeyed Yahweh very much.
20 Tiglath-pileseri, mfalme wa Ashuru, akaja kwake na akampa tabu badala ya kumpa nguvu.
Tiglath-Pileser, the king of Assyria, sent [his army saying that they would] help Ahaz, but instead of helping him, they caused him to experience trouble.
21 Kwa kuwa Ahazi aliteka nyara nyumba ya Yahwe na nyumba ya mfalme na viongozi, kwa ajili ya kuvitoa vitu vya thamani kwa mfalme wa Ashuru. Lakini kufanya hivyo hakukumfaidisha yeye.
Ahaz’s [soldiers] took some of the [valuable] things from the temple and from the king’s palace and from other leaders of Judah and sent them to the king of Assyria [to pay him to help them], but the king of Assyria refused to help Ahaz.
22 Mfalme Ahazi huyu huyu akatenda dhambi hata zaidi dhidi ya Yahwe katika muda wa mateso yake.
While King Ahaz was experiencing those troubles, he disobeyed Yahweh even more.
23 Kwa maana aliwatolea dhabihu mingu wa Dameski, miungu ambao walimshinda. Akasema, “Kwa sababu miungu wa mfalme wa Aramu waliwasaidia, nitawatolea sadaka ili wanisaidie.” Lakini walikuwa watesi wake na Israeli yote.
He offered sacrifices to the gods that were worshiped in Damascus, whose [army] had defeated his [army]. He thought, “The gods that are worshiped by the kings of Syria have helped them, so I will offer sacrifices to those gods in order that they will help me.” But worshiping those gods caused Ahaz and all of Israel to be ruined.
24 Ahazi akazikusanya pamoja samani za nyumba ya Mungu na kuzikata vipande vipande. Akaifunga milango ya nyumba ya Yahwe na kuzitengeneza madhabahu kwa ajili yake mwenyewe katika kila kona ya Yerusalemu.
Ahaz gathered all the furnishings [that were used] in the temple and broke them into pieces. He locked the doors of the temple and set up altars [for worshiping idols] at every street corner in Jerusalem.
25 Katika kila mji wa Yuda akafanya sehemu za juu kwa ajili ya kutolea sadaka za kuteketezwa kwa miungu wengine. Akamfanya Yahwe, Mungu wa babu zake, akasirike.
In every town in Judah, his workers built shrines to burn sacrifices to other gods, and that caused Yahweh, the God whom their ancestors [worshiped], to be very angry.
26 Sasa matendo yake yaliyobaki, na njia zake zote, mwanzo na mwisho, ona, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
A record of the other things that Ahaz did while he was the king, from when he started to rule until he died, is written in the scroll called ‘The History of the Kings of Judah and Israel’.
27 Ahazi akalala pamoja na babu zake, na wakamzika katika mji, katika Yerusalemu, lakini hawakumleta kwenye makaburi ya wafalme wa Israeli. Hezekia, mwanaye, akawa mfamle katika nafasi yake.
Ahaz died and was buried in Jerusalem, but he was not buried in the tombs where the other kings [had been buried]. Then his son Hezekiah became the king.

< 2 Nyakati 28 >