< 2 Nyakati 28 >
1 Ahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, na akatawala miaka kumi na sita katika Yerusalemu. Hakufanya yaliyoadili katika macho ya Yahwe, kama Daudi babu yake alivyokuwa amefanya.
Ahaz was twenty years old when he had begun to reign, and he reigned for sixteen years in Jerusalem. He did not do what is right in the sight of the Lord, as his father David did.
2 Badala yake, alitembea katika njia za wafalme wa Israeli; pia alitengeneza sanamu za kusubu kwa ajila ya Mabaali.
Instead, he walked in the ways of the kings of Israel. Moreover, he also cast statues for the Baals.
3 Zaidi ya hayo, akafukiza uvumba katika bonde la Beni Hinomu na akawaweka watoto wake ndani ya moto, kwa mjibu wa desturi za uzinzi za watu ambao Yahwe aliwafukuza nje ya nchi zao mbele za watu wa Israeli.
It is he who burned incense in the Valley of the son of Hinnom. And he purified his sons by fire, in accord with the ritual of the nations that the Lord put to death at the advent of the sons of Israel.
4 Akatoa sadaka na kufukiza uvumba katika sehemu za juu na juu ya vilima na chini ya kila mti wenye majani mabichi.
Also, he was sacrificing and burning incense in the high places, and on the hills, and under every leafy tree.
5 Kwa hiyo Yahwe Mungu wa Ahazi, akamweka katika mikono ya mfalme wa Shamu. Waaramu wakamshinda na kuchukua kutoka kwake kundi kubwa la mateka, wakawapeleka Damesiki. Ahazi pia aliwekwa katika mikono ya mfalme wa Israeli ambaye alimshinda kwa mauji makuu.
And so the Lord, his God, delivered him into the hand of the king of Syria, who struck him and took great plunder from his kingdom. And he carried it away to Damascus. Also, he was delivered into the hands of the king of Israel, and he struck him with great affliction.
6 Kwa maana Peka mwana wa Remalia, aliwaua katika Yuda wanajeshi 120, 00 kwa siku moja, wote walikuwa wanaume hodari, kwa maana walikuwa wamemsahau Yahwe, Mungu wa babu zao.
And Pekah, the son of Remaliah, killed, on one day, one hundred twenty thousand, all of them men of war from Judah, because they had forsaken the Lord, the God of their fathers.
7 Zikri, mtu mwenye nguvu kutoka Efraimu, akawaua Maaseya mwana wa mfalme, Azrikamu, mwangalizi mkuu wa ikulu, na Elkana, ambaye alikuwa karibu na mfalme.
In the same time, Zichri, a powerful man of Ephraim, killed Maaseiah, the son of the king, and Azrikam, the governor of his house, and also Elkanah, who was second to the king.
8 Jeshsi la Israeli likachukua mateka kutoka kwa ndugu zao 200, 000 wake, wana, na mabinti. Pia wakachukua nyara nyingi, ambazo walipeleka Samaria.
And the sons of Israel seized, from their brothers, two hundred thousand women, boys, and girls, and immense plunder. And they took it away to Samaria.
9 Lakini nabii wa Yahwe alikuwapo huko, jina lake aliitwa Odedi. Alikwenda nje kukutana na jeshi likiingia Samaria. Akawaambia, “Kwa sababu Yahwe, Mungu wa babu zenu, alikuwa na hasiri na Yuda, akawatia katika mikono yenu. Lakini mmewaua katika hasira inayofika juu mbinguni.
At that time, there was a prophet of the Lord there, named Oded. And going out to meet the army arriving in Samaria, he said to them: “Behold, the Lord, the God of your fathers, having become angry against Judah, has delivered them into your hands. But you have killed them by atrocities, so that your cruelty has reached up to heaven.
10 Sasa ninyi badala ya kuwahifadhi wanaume na wanawake wa Yuda na Yerusalemu kama watumwa wenu. Lakini je hamko na hatia ya dhambi zenu zidi ya Yahwe Mungu wenu?
Moreover, you wanted to subjugate the sons of Judah and Jerusalem as your men and women servants, which is a work that should never be done. And so you sinned in this matter against the Lord your God.
11 Sasa basi, nisikilizeni: warudisheni wafubgwa, ambao mmewachukua wa ndugu zenu, kwa maana ghadhabu ya Yahwe iko juu yenu.”
But listen to my counsel, and release the captives, whom you have brought from your brothers. For a great fury of the Lord is hanging over you.”
12 Kisha baadhi ya viongozi wa watu wa Efraimu—Azaria mwana wa Yohanani, Berekia mwana wa Meshiremothi, na Yehizikia mwana wa Shalumu, na Amasa mwana wa Hadlai, wakasimama kinyume na wale waliorudi kutoka vitani.
And so, some of the leaders of the sons of Ephraim, Azariah, the son of Johanan, Berechiah, the son of Meshillemoth, Jehizkiah, the son of Shallum, and Amasa, the son of Hadlai, stood up against those who were arriving from the battle.
13 Wakasema kwao, “Lazimaa msiwaleta wafungwa hapa, kwa kuwa mlikusudia jambo ambalo litaleta juu yetu dhambi dhidi ya Yahwe, kuongeza dhambi juu yetu na makosa yetu, kwa maana makosa yetu ni makuu, na kuna hasira kali dhidi ya Israeli.”
And they said to them: “You shall not lead back captives to here, lest we sin against the Lord. Why are you willing to add to our sins, and to build upon our old offenses? For indeed, the sin is great, and the furious anger of the Lord is hanging over Israel.”
14 Hivyo watu wenye silaha wakawaacha wafungwa na mateka mbele ya viongozi wa Israeli na kusanyiko lote
And the warriors released the spoils and all that they had seized, in the sight of the leaders and the entire multitude.
15 Watu ambao walipangwa kwa majina wakanyanyuka na kuwachukua wafungwa, na kuwavika wote waliokuwa uchi miongoni mwa mateka. Wakawavika na kuwapa viatu. Wakawapa chakula wale na kunywa. Wakawahudumia majeraha yao na kuwaweka waliodhaifu juu ya punda. Wakawarudisha kwenye familia zao katika Yeriko, (Ulioitwa mji wa mitende). Kisha wakarudi Samaria.
And the men, whom we mentioned above, rose up and took the captives. All those who were naked, they clothed from the spoils. And when they had clothed them, and had given them shoes, and had refreshed them with food and drink, and had anointed them because of the hardship, and had cared for them, whoever was not able to walk and whoever was feeble in body, they set them upon beasts of burden, and they led them to Jericho, the city of palm trees, to their brothers, and they themselves returned to Samaria.
16 Wakati huo Mfalme Ahazi akatuma wajumbe kwa wafalme wa Ashuru kuwaomba wamsaidie.
In that time, king Ahaz sent to the king of the Assyrians, requesting assistance.
17 Kwa maana Waedomu walikuwa wamekuja tena na kuvamia Yuda, wakachukua wafungwa.
And the Edomites arrived and struck down many of Judah, and they seized great plunder.
18 Wafilisti pia wakavamia miji ya nchi ya chini na ya Negebu ya Yuda. Waliichukua Beth-shemeshi, Ayaloni, Giderothi, SoKo pamoja na vijiji vyake, Timna pamoja na vijiji vyake. Wakaenda kuishi katika sehemu hizo.
Also, the Philistines spread out among the cities of the plains, and to the south of Judah. And they seized Beth-shemesh, and Aijalon, and Gederoth, and also Soco, and Timnah, and Gimzo, with their villages, and they lived in them.
19 Kwa kuwa Yahwe aliishusha chini Yuda kwa sababu ya Ahazi, mfalme wa Israeli; kwa maana alikuwa ametenda maovu katika Yuda na alikuwa ametenda dhambi nzito sana dhidi ya Yahwe.
For the Lord had humbled Judah because of Ahaz, the king of Judah, since he had stripped it of help, and had shown contempt for the Lord.
20 Tiglath-pileseri, mfalme wa Ashuru, akaja kwake na akampa tabu badala ya kumpa nguvu.
And he led against him Tilgath-pilneser, the king of the Assyrians, who also afflicted him and laid waste to him, without resistance.
21 Kwa kuwa Ahazi aliteka nyara nyumba ya Yahwe na nyumba ya mfalme na viongozi, kwa ajili ya kuvitoa vitu vya thamani kwa mfalme wa Ashuru. Lakini kufanya hivyo hakukumfaidisha yeye.
And so Ahaz, despoiling the house of the Lord, and the house of the kings and the leaders, gave gifts to the king of the Assyrians, and yet it profited him nothing.
22 Mfalme Ahazi huyu huyu akatenda dhambi hata zaidi dhidi ya Yahwe katika muda wa mateso yake.
Moreover, in the time of his anguish, he also added to his contempt against the Lord. King Ahaz himself, by himself,
23 Kwa maana aliwatolea dhabihu mingu wa Dameski, miungu ambao walimshinda. Akasema, “Kwa sababu miungu wa mfalme wa Aramu waliwasaidia, nitawatolea sadaka ili wanisaidie.” Lakini walikuwa watesi wake na Israeli yote.
immolated victims to the gods of Damascus, those who had struck him. And he said: “The gods of the kings of Syria assist them, and so I will please them with victims, and they will help me.” But to the contrary, they had been the ruin of him and of all Israel.
24 Ahazi akazikusanya pamoja samani za nyumba ya Mungu na kuzikata vipande vipande. Akaifunga milango ya nyumba ya Yahwe na kuzitengeneza madhabahu kwa ajili yake mwenyewe katika kila kona ya Yerusalemu.
And so, Ahaz, having despoiled and broken apart all the vessels of the house of God, closed up the doors of the temple of God, and made for himself altars in all the corners of Jerusalem.
25 Katika kila mji wa Yuda akafanya sehemu za juu kwa ajili ya kutolea sadaka za kuteketezwa kwa miungu wengine. Akamfanya Yahwe, Mungu wa babu zake, akasirike.
Also, he constructed altars in all the cities of Judah, in order to burn frankincense, and so he provoked the Lord, the God of his fathers, to wrath.
26 Sasa matendo yake yaliyobaki, na njia zake zote, mwanzo na mwisho, ona, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
But the rest of his words, and all his works, the first and the last, have been written in the book of the kings of Judah and Israel.
27 Ahazi akalala pamoja na babu zake, na wakamzika katika mji, katika Yerusalemu, lakini hawakumleta kwenye makaburi ya wafalme wa Israeli. Hezekia, mwanaye, akawa mfamle katika nafasi yake.
And Ahaz slept with his fathers. And they buried him in the city of Jerusalem. And they did not allow him to be in the sepulchers of the kings of Israel. And his son, Hezekiah, reigned in his place.