< 2 Nyakati 26 >
1 Watu wote wa Yuda wakamchukua Uzia, ambaye alikuwa na aumri wa mika kumi na sita, na wakamfanya mfalme katika nafasi ya baba yake Amazia.
Then all the people of Iudah tooke Vzziah, which was sixteene yeere olde, and made him King in the steade of his father Amaziah.
2 Ndiye aliuyeijenga tena Elathi na kuurejesha kwa Yuda. Baada ya hapo mfalme akalala pamoja na babu zake.
He buylt Eloth, and restored it to Iudah after that the King slept with his fathers.
3 Uzia alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala. Akatawala miaka ishirini na mabili katika Yerusalemu. Jina la mama yake lilikuwa Yekolia; alikuwa wa Yerusalemu.
Sixteene yeere olde was Vzziah, when he began to reigne, and he reigned two and fiftie yere in Ierusalem, and his mothers name was Iecoliah of Ierusalem.
4 Akafanya yaliyokuwa sahihi katika macho ya Yahwe, akiufuata mfano wa baba yake, katika kila jamabo.
And hee did vprightly in the sight of the Lord, according to al that his father Amaziah did.
5 Alijitoa kumtafuta Mungu katiaka siku za Zekaria, ambaye alimpa maelekezo kwa ajili ya kumtii Mungu. Kadri alivyomtafuta Yaahwe, Mungu alimfanikisha.
And he sought God in the dayes of Zechariah (which vnderstoode the visions of God) and when as he sought the Lord, God made him to prosper.
6 Uzia akaenda na kupigana zidi ya Wafilisti. Akaubomoa ukuta wa mji wa Gathi, Yabne, na Ashdodi; akajenga miji katika nchi ya Ashdodi na miongoni mwa Wafilisti.
For he went forth and fought against the Philistims and brake downe the wall of Gath, and the wall of Iabneh, and the wall of Ashdod, and built cities in Ashdod, and among the Philistims.
7 Mungu aakaamsaidia zidi ya Wafilist, zidi ya Waarabu waliokuwa wakiishi Gur - baali, na zidi ya Wameuni.
And God helped him against ye Philistims, and against the Arabians that dwelt in Gur-baal and Hammeunim.
8 Waamoni wakalipa kodi kwa Uzia, na umaarufu wake ukaenea, hata kufika maingilio ya Misiri, kwa sababu alikuwa ameanza kuwa maarufu.
And the Ammonites gaue gifts to Vzziah, and his name spred to the entring in of Egypt: for he did most valiantly.
9 Zaidi ya hayo, Uzia akajenga minara katika Yerusalemu katika kona ya Lango, kwenye Lango la Bonde, na pa kwenye kona ya ukuta, na akavizungushia ngome.
Moreouer Uzziah buylt towres in Ierusalem at the corner gate, and at the valley gate, and at the turning, and made them strong.
10 Akajenga minara ya ulinzi katika nyika na akachimba mabwawa, kwa maana alikuwa na ng'ombe wengi, katika visiwa vya chini na katika nchi tambarare. Alikuwa na wakulima na wapandaji wa zabibu katika mwinuko wa nchi na katika mashamba yenye rutuba, kwa maana alipenda kulima.
And he built towres in the wildernesse, and digged many cisternes: for he had much cattell both in the valleyes and playnes, plowmen, and dressers of vines in the mountaines, and in Carmel: for he loued husbandrie.
11 Zaidi ya hayo, Uzia alikuwa na jeshi la wanaume wa kupigana vita ambao walienda vitani katika makundi ambayo idadi yake ilikuwa imehesabiwa na Yeieli, mwandishi. na Maaseya, afisa, chini ya mamlaka ya Hanania, mmoja wa maamri jeshi wa mfalme.
Vzziah had also an hoste of fighting men that went out to warre by bandes, according to the count of their nomber vnder the hande of Ieiel the Scribe, and Maaseiah the ruler, and vnder the hand of Hananiah, one of the Kings captaines.
12 Jumla ya wakuu wa nyumba za mababu, watu wa kupigana vita, walikuwa 2, 600.
The whole nomber of the chiefe of the families of the valiant men were two thousande and sixe hundreth.
13 Chini ya mkono wao kulikuwa na jeshi la watu 307, 500 ambao walifanya vita kwa nguvu ili kumsaidia mfalme idi ya maadui.
And vnder their hande was the armie for warre, three hundreth and seuen thousand, and fiue hundreth that fought valiantly to helpe the King against the enemie.
14 Uzia akaandaa kwa ajili yao—kwa ajili ya jeshi lote — ngao, mikuki, chapeo, deraya za majini, nyuta, na mawe ya kurusha.
And Vzziah prepared them throughout all the hoste, shieldes, and speares, and helmets, and brigandines, and bowes, and stones to sling.
15 Katka Yerusalemu alijenga mitambo, iliyobuniwa na watu wenye ujuzi, ili iwe juu ya minara na juu ya buruji, kwa ajili ya kurushia mishale na mawe makaubwa. Umaarufu wake ukaenea hadi nchi za mbali, kwa maana alisaidiwa sana hadi alipokuwa na ngavu sana.
He made also very artificial engins in Ierusalem, to be vpon the towres and vpon the corners, to shoote arrowes and great stones: and his name spred farre abroade, because God did helpe him marueilously, till he was mightie.
16 Lakini Uzia alipokuwa amekuwa na nguvu nyingi, moyo wake ulijiinua akatenda kwa uovu; akafanya makosa zidi ya Yahwe, Mungu wake, kwa maana alienda kwenye nyumba ya Yahwe kwa ajili ya kufukiza uvumba juu ya madhabahu ya kufukizia.
But when he was strong, his heart was lift vp to his destruction: for he transgressed against the Lord his God, and went into the Temple of the Lord to burne incense vpon the altar of incense.
17 Azaria, kuhani, akamfuata, na pamoja naye makuhanai themanini wa Yahwe, ambao walikuwa watu wenye ujasiri.
And Azariah the Priest went in after him, and with him foure score Priests of the Lord, valiant men.
18 Walimzuia Uzia, mfalme, na wakasema kwake, “Siyo jukumu lako, Uzia, kumtolea Yahwe uvumba, bali ni kazi ya makuhani, wana wa Haruni, amabao wametengwa kwa ajili ya kutoa sadaka za uvumba. Toka nje ya sehemu takatifu, kwa maana huna uaminifu na hautaheshimiwa na Yahwe Mungu.”
And they withstoode Vzziah the King, and said vnto him, It perteineth not to thee, Vzziah, to burne incense vnto the Lord, but to the Priests the sonnes of Aaron, that are consecrated for to offer incense: goe forth of the Sanctuarie: for thou hast transgressed, and thou shalt haue none honour of the Lord God.
19 Kisha Uzia akakasirika. Alikuwa ameshikilia chetezo mkononi kwa ajili ya kufukiza uvumba. Wakati alipowaghadhabikia makuhani, ukoma ukatokea juu ya uso wake mbele ya makuhani katika nyumba ya Yahwe, pembeni mwa madhabahu ya uvumba.
Then Vzziah was wroth, and had incense in his hand to burne it: and while he was wroth with the Priestes, the leprosie rose vp in his forehead before the Priestes in the house of the Lord beside the incense altar.
20 Azaria kuhani mkuu na makuhani wote wakamwanagalia, na, tazama, alikuwa amepatwa ukoma juu ya uso wake. Walimwondoa pale haraka. Kwa hakika, aliharakisha kwenda nje, kwa maana Yahwe alikuwa amempiga.
And when Azariah the chiefe Priest with al the Priestes looked vpon him, behold, he was leprous in his forehead, and they caused him hastily to depart thence: and he was euen compelled to go out, because the Lord had smitten him.
21 Uzia, mfalme, alikuwa mwenye ukoma hadi siku ya kufa kwake na aliishi katika nyumba ya kutengwa tangu alipokuwa mwenye ukoma, kwa maan alitengwa na nyumba ya Yahwe. Yothamu, mwanaye, alikuwa mkuu wa anyumba ya mfalme na aliwatawala watu wa nchi.
And Vzziah the king was a leper vnto the day of his death, and dwelt as a leper in an house apart, because he was cut off from the house of ye Lord: and Iotham his sonne ruled ouer the Kings house, and iudged the people of the land.
22 Mambo mengine kuhusu Uzia, mwanzo na mwisho, yako katika kile ambacho Isaya, mwana wa Amozi, nabii, aliandika.
Concerning the rest of the acts of Vzziah, first and last, did Isaiah the Prophet the sonne of Amoz write.
23 Kwa hiyo Uzia akalala pamoja na babu zake; walimzka pamoja na babu zake katika uwanja wa maziko wa Mfalme, kwa maana walisema, “Ni mwenye ukoma”. Yothamu, mwanaye, akawa mfalme katika nafasi yake.
So Vzziah slept with his fathers, and they buryed him with his fathers in the fielde of the burial, which perteined to the kings: for they said, He is a leper. And Iotham his sonne reigned in his steade.