< 2 Nyakati 2 >
1 Sasa Selemani akaamuru kulijengea nyumba jina la Yahwe na nyumamba kwa ajili ya ikulu ya ufalme wake.
撒羅滿決定為上主的名建造聖殿,為自己修築王宮。
2 Selemeni akateua wanaume elfu sabini wabebe mizigo, na wanaume elfu themanini wa kukata mbao katika mlima, na wanaume 3, 600 kwa ajili ya kusimamia.
撒羅滿點派了七萬人作運夫,八萬人在山上鑿石,三千六百人作監工。
3 Selemani akatuma ujumbe kwa Hiramu, mfalme wa Tiro, ukisema, “Kama ulivyofanya na Daudi baba yangu, ulivyomtumia magogo ya mierezi ili ajenge nyumba ya kuishi, fanya hivyo hivyo na mimi.
撒羅滿遣使向提洛王希蘭說:「有如你怎樣對待了我父達味,給他運來了香柏木,建造他居住的宮殿,也請你如此對待我。
4 Tazama, niko karibu kujenga nyumba kwa ajili ya jina la Yahwe Mungu wangu, kuiweka wakifu kwake, kwa ajili ya kumtolea sadaka za kuteketezwa zenye viungo vitamu mbele zake, kwa ajili ya mkate wa uwepo, na kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa asubuhi na jioni, katika siku za Sabato na za mwezi mpya, na katika sikukuu zilizoteuliwa kwa ajili ya Yahwe Mungu wetu. Hii itakuwa milele, kwa Israeli.
我現今要為上主我的天主的名,建造一座聖殿,奉獻給他,在他面前焚燒芬芳的香料,永遠獻上供餅,每日早晚、安息日、月朔,以及上主我們天主的節日,奉獻全燔祭:這為以色列人是永久的事。
5 Nyumba nitakayoijenga itakuwa kubwa sana, maana Mungu wetu ni mkuu kuliko miungu mingine yote.
我建造的殿宇必須廣大,因為我們的天父大於諸神。
6 Lakini ni nani anayeweza kumjengea Mungu nyumba, kama dunia yote na hata mbigu yenyewe haviwezi kumtosha? Mimi ni nani hata nimjengee nyumba, ispokuwa sadaka kwa ajili ya sadaka za kufukiza mbele zake?
然而,誰有能力為他建造一座殿宇﹖天與諸天之天,尚容不下他。我是誰,竟能為他建造殿宇﹖不過只是為在他面前焚香罷了!
7 Kwa hiyo nileteeni mtu mwenye ujuzi wa kazi katika kazi ya dhahabu, fedha, shaba, na chuma, na ya dhambarau, na nyekundu, na sufu ya samawati, mtu anayejua kutengeza aina zote za mapambo ya mbao. Atakuwa na watu wenye ustadi waliopamoja nami katika Yuda na Yerusalemu, ambao Daudi baba yangu aliwaweka.
現在,請你給我派一位技師來,他要精於金、銀、銅、鐵,以及紫紅、朱紅、藍線等工作;並且還應會各種雕刻,好與我父親達味在猶大和耶路撒冷所準備的技術人員一同工作。
8 Nitumieni pia mierezi, miberoshi, na miti ya msandali kutoka Lebanoni, maana najua ya kuwa watumishi wako wanajua jinsi ya kukata mbao katika Lebanoni. Angalia, watumishi wangu watakuwa na watumishi wako,
請你由黎巴嫩給我運香柏、松柏和檀香木來,因為我知道你的僕人善於砍伐黎巴嫩的木材;我的僕人將與你的僕人一同工作。
9 ili kwamba watayarishe mbao nyingi kwa ajili yangu, maana nyumba ninayotaka kuijenga itakuwa kubwa na ya ajabu.
他們要為我大量預備木材,因為我要建造的殿宇極其廣大。
10 Angalia, nitawapa watumishi wako, watu watakaozikata mbao, kori ishirini elfu za ngano ya aridhini, kori ishirini elfu za shayiri, bathi ishirini elfu za mvinyo, na bathi ishirini elfu za mafuta.” (Maandishsi ya kale yanasema: “kori ishirini elfu za ngano kama chakula”).
至於你那些伐木砍樹的僕人,我必供給他們食糧,小麥二萬「苛爾,」大麥二萬「苛爾,」酒兩萬「巴特,」油兩萬「巴特。」[提洛王應允合作]
11 Kisha Hiramu, mfalme wa Tiro, akajibu kwa maandishi, ambayo alimtumia Selemani: “Kwa kuwa Yahwe anawapenda watu wake, amekufanya kuwa mfalme juu yao.”
提洛王希蘭回信給撒羅滿說:「上主由於愛慕自己的百姓,所以立你作了他們的君王。」
12 Zaidi ya hayo, Hiramu akasema, “Abarikiwe Yahwe, Mungu wa Israeli, aliyeziumba mbingu na dunia, amempa Daudi mwana mwenye hekima, mwenye karama ya busara na uelewa, ambaye atajenga nyumba kwa aajili ya Yahwe, na nyumba kwa ajili ya ufalme wake.
希蘭又說:「創造天地的上主以色列的天主應受讚美! 因為他賜給了達味王一個智慧的兒子,聰明機敏,可為上主建造殿宇,為自己修築無宮。
13 Sasa nimemtum mtu mwenye ujuzi, mwenye karama ya uelewa, Hiramu, mtaalamu wangu.
我現在打發一個具有智慧和才學的人去,他名叫胡蘭阿彼,
14 Ni mwana wa mwanamke wa binti za Dani. Baba yake alikuwa mtu kutoka Tiro. Ana ujuzi katika kazi za dhahabu, fedha, shaba, chuma, mawe, na katika mbao, na katika dhambarau, samawati, na sufu yenkundu, na kitani safi. Pia ana ujuzi katika kutengeneza michoro ya aina yoyote na katika kubuni kitu chochote. Apatiwe nafsi miongoni mwa watumishi wako wenye ujuzi, na pamoja na wale wa bwana wangu, Daudi, baba yako.
是一丹支派女人的兒子,他父親是提洛人,他精於金、銀、銅、鐵、石、木紫色、紅色、藍色、細麻,以及朱紅線各種工作,善於各種雕刻,又能設計各種托於他的技工。這人可與你的技師和你父親我主達味的技師,一同工作。
15 Sasa, ngano na shayiri, mafuta na mvinyo, ambayo bwana wangu aliisema, na apeleke sasa vitu hivi kwa watumishi wake.
我主談及的小麥、大麥、油和酒,請即運來分配給僕人。
16 Tutakata mbao kutoka Lebanoni, mbao nyingi kadri unavyohitaji. Tutazileta kwako kama mitumbwi kupitia bahari kwenda Yafa, na utazibeba hadi Yerusalemu.”
我們必照你所需要的,在黎巴嫩砍伐樹木,編成木筏,由海上運到約培;以後你運到耶路撒冷。選派工匠
17 Selemani akawahesabu watu wageni waliokuwa katika nchi ya Israeli, kwa kutumia njia ya Daudi, baba yake, aliyoitumia kuwahesabu. Walikutwa wako 153, 600.
撒羅滿按照他父親達味所統計過的數目,又統計了住在以色列境內的一切外方人,共計十五萬三千六百人,
18 Miongoni mwao aliwateua sabini elfu ili wabebe mizigo, themanini elfu kuwa wakataji wa mbao katika milima, na 3, 600 kuwa wasimamizi wa kuwasimamia watu wafanye kazi.
委派其中的七萬人作運夫,八萬人在山上鑿石,安千六百人作監工,督促人民工作。