< 2 Nyakati 17 >

1 Yehoshafati mwana wa Asa akawa mfalme katika nafasi yake. Yehoshafati akajiimarisha dhidi ya Israeli.
Josaphat, son fils, régna à sa place et se fortifia contre Israël.
2 Akaweka majeshi katika miji yote Yuda yenye ngome, na akaweka magereza katika nchi ya Yuda na katika miji ya Efraimu, ambayo Asa baba yake alikuwa ameiteka.
Il plaça des forces dans toutes les villes fortes de Juda, et il établit des garnisons dans le pays de Juda et dans les villes d'Ephraïm, dont Asa, son père, s'était emparé.
3 Yahwe alikuwa pamoja na Yehoshafati kwa sababu alitembea katika njia za kwanza za baba yake Daudi, na hakuwatafuta Mabaali. (Baadhi ya mandiko ya kale hayana “Daudi”, na baadhi ya matoleo ya kisasa yameacha hili jina “Daudi).
Yahvé fut avec Josaphat, parce qu'il marcha dans les premières voies de David, son père, et qu'il ne chercha pas les Baals,
4 Badala yake, alimtegemea Mungu wa baba yake, na alitembea katika amri zake, siyo katika tabia ya Israeli.
mais qu'il chercha le Dieu de son père, et qu'il marcha dans ses commandements, et non dans les voies d'Israël.
5 Kwa hiyo Yahwe akaimarisha sheria katika mkono wake; Yuda wote wakaleta kodi kwa Yehoshafati. Alikuwa na utajiri na heshima kubwa.
C'est pourquoi Yahvé affermit le royaume entre ses mains. Tout Juda apportait un tribut à Josaphat, et il eut des richesses et des honneurs en abondance.
6 Moyo wake ulikuwa umejikita katika njia za Yahwe. Pia aliziondoa sehemu za juu na Maashera mbali na Yuda.
Son cœur s'élevait dans les voies de l'Éternel. Il fit disparaître de Juda les hauts lieux et les mâts d'ashère.
7 Katika mwaka wa tatu wa utawala wake aliwatuma wakuu wake Ben-haili, Obadia, Zekaria, Nethania, na Mikaya, ili wafundishe katika miji ya Yuda.
La troisième année de son règne, il envoya ses chefs, Ben Haïl, Abdias, Zacharie, Nethaneel et Michée, enseigner dans les villes de Juda,
8 Pamoja nao walikuwepo Walawi: Shemaya, Nethanieli, Zebadia, Asaheli, Shemiramothi, Yehonathani, Adoniya, Tobia, na Tob-adonia, pamoja nao walikuwepo makuhani Elishama na Yehoramu.
et avec eux des Lévites, Schemaeja, Nethania, Zebadia, Asaël, Schemiramoth, Jehonathan, Adonija, Tobija et Tobadonija, les Lévites, et avec eux Élischama et Joram, les prêtres.
9 Walifundisha katika Yuda, wakiwa na kitabau cha sheria ya Yahwe. Wakaenda karibu miji yote ya Yuda na kufundisha miongoni mwa watu.
Ils enseignaient en Juda, ayant avec eux le livre de la loi de Yahvé. Ils parcoururent toutes les villes de Juda et enseignèrent parmi le peuple.
10 Hofu ya Yahwe ikashuka juu ya falme zote za nchi, zilizouzunguka Yuda, kwa hiyo hazikufanya vita dhidi ya Yehoshafati.
La crainte de Yahvé s'abattit sur tous les royaumes des pays qui entouraient Juda, de sorte qu'ils ne firent pas la guerre à Josaphat.
11 Baadhi ya Wafilisti wakamletea Yehoshafati zawadi, fedha kama kodi. Waarabu pia wakamletea makundi, 7, 700 kondoo waume, na mbuzi 7, 770.
Des Philistins apportèrent à Josaphat des présents et de l'argent en guise de tribut. Les Arabes lui apportèrent aussi des troupeaux: sept mille sept cents béliers et sept mille sept cents chèvres mâles.
12 Yehoshafati akawa na nguvu sana.
Josaphat devint extrêmement grand, et il bâtit en Juda des forteresses et des villes de commerce.
13 Akajenga ngome na miji ya maghala katika Yuda. Alikuwa na kazi nyingi katika miji ya Yuda, na wanajeshsi—imara, wanaume hodari—katika Yerusalemu.
Il eut de nombreux ouvrages dans les villes de Juda, et des hommes de guerre, des vaillants hommes, à Jérusalem.
14 Hapa ni rodha yao, wamepangwa kwa majina ya nyumba za baba zo: Kutoka Yuda, maakida wa maelfu; Adna yule jemedari, na pamoja naye wanaume wa kwenda vitani 300, 000;
Voici leur dénombrement, selon les maisons de leurs pères: De Juda, les chefs de milliers: Adna, chef, et avec lui trois cent mille vaillants hommes;
15 akifuatiwa na Yehonani jemedari, na pamoja naye wanaume 280, 00;
à côté de lui, Jochanan, chef, et avec lui deux cent quatre-vingt mille hommes;
16 akifuatiwa na Amasia mwana wa Zikri, ambaye kwa hiari alijitoa kumtumikia Yahwe; na pamoja naye wanaume wa kwenda vitani 200, 000.
à côté de lui, Amasia, fils de Zicri, qui s'offrit volontairement à l'Éternel, et avec lui deux cent mille vaillants hommes.
17 Kutoka Benyamini: Eliada mtu jasiri, na pamoja naye watu 200, 000 waliovaa upinde na ngao;
De Benjamin: Eliada, vaillant homme, et avec lui deux cent mille hommes armés de l'arc et du bouclier;
18 akifutiwa na Yehozabadi, na pamoja naye askari 180, 000 waliotayari kwa vita.
et à côté de lui Jehozabad, et avec lui cent quatre-vingt mille hommes prêts à faire la guerre.
19 Hawa walikuwa ni wale ambao walimtumikia mfalme, miongoni mwao wale ambao mfalme aliwaweka katika miji ya ngome katika Yuda yote.
Tels étaient ceux qui servaient le roi, sans compter ceux que le roi plaça dans les villes fortes de tout Juda.

< 2 Nyakati 17 >