< 2 Nyakati 16 >

1 Katika mwaka wa thelathini na sita wa utawala wa Asa, Baasha, mfalme wa Israeli, akatenda kwa ukatili dhidi ya Yuda na akaujenga Rama, ili kwamba asimruhusu mtu yeyote kutoka wala kuingia katika nchi ya Asa, mfalme wa Yuda.
In the thirty-sixth year of Asa's reign, Baasha, king of Israel, invaded Judah. He fortified Ramah to stop anyone coming from or going to Asa, king of Judah.
2 Kisha Asa akaitoa fedha na dhahabu nje ya vyumba vya kuhifadhia katika nyumba ya Yahwe na nje ya nyumba ya mfalme, na akaituma kwa Ben Hadadi mfalme wa Aramu, ambaye aliishi Dameski. Akasema, pawe na agano kati yako na mimi, kama palivyokuwa na agano kati ya baba yangu na baba yako. Angalia, nimekutumia fedha na dhahabu.
Asa took the silver and gold from the treasuries of the Lord's Temple and the king's palace and sent them to Ben-hadad, king of Syria, who lived in Damascus, with a message that said:
3 Livunje agano lako na Baasha, mfalme wa Israeli, ili kwamba aniache.”
“Make an alliance between me and you like the one between my father and your father. Look at the silver and gold I've sent you. Go ahead and break your agreement with Baasha, king of Israel, so that he will leave me and go home.”
4 Ben Hadadi akamsikiliza mfalme Asa na kutuma maakida wa majeshsi dhidi ya miji ya Israeli. Wakavamia Iyoni, Dani, Abelimaimu, na miji yoye ya kuhifadhia ya Naftali.
King Ben-hadad did as Asa had asked, and he sent his armies and their commanders to attack the towns of Israel. They conquered Ijon, Dan, Abel-maim, and all the storehouse towns of Naphtali.
5 Ikawa kwamba Baasha aliposikia hili, akaacha kuujenga Rama, na akaistisha kazi yake.
When Baasha heard about it, he stopped fortifying Ramah and gave up his project.
6 Kisha Asa mfalme akawachukua Yuda wote pamoja naye. Wakayabeba mawe na mbao za Rama ambazo Baasha alikuwa anajengea ule mji. Kisha Mfalme Asa alitumia vifaa hivyo vya ujenzi kwa ajili ya kuijenga Gaba na Mispa.
So King Asa went with all the men of Judah, and they carried away from Ramah the stones and the timbers Baasha had used for building, and with them he built up Geba and Mizpah.
7 Wakati huo Hanani mwonaji akaenda kwa Asa, mfalme wa Yuda, na akamwambia, “Kwa sababu umemtegemea mfalme wa Aramu, na hukumtegemea Yahwe Mungu wako, jeshi la mfalme wa Aramu limetoroka nje ya mikono yako.
But right then Hanani the seer came to Asa, king of Judah, and told him, “Because you have put your trust in the king of Aram and have not put your trust in the Lord your God, your opportunity to destroy the army of the king of Aram has gone.
8 Waethiopia na Walubi hawakuwa jesi kubwa, wenye magari mengi na wapanda farasi wengi? Na bado, kwa sababau ulimtegemea Yahwe, alikupa ushindi juu yao.
Didn't the Ethiopians and Libyans have a huge army with many chariots and horsemen? Yet because you trusted in the Lord, he made you victorious over them.
9 Kwa maana macho ya Yahwe hukimbia kila mahali katika dunia yote, ili kwamba ajioneshe mwenyewe shujaa kwa niaba ya wale amabao mioyo yao ni mikamilifu kumwelekea yeye. Lakini umetenda kipumbavu katika jambo hili. Kwa maana tangu sasa na kuendelea, utakuwa na vita.” Kisha Asa akamkasirikia mwonaji, akamuweka gerezani, kwa maana alikuwa na hasira naye juu ya jambao
For the Lord looks all over the earth for the opportunity to show his power on behalf of those who are completely and sincerely devoted to him. You have acted stupidly in doing this. So from now on you will always be at war.”
10 hili. Wakati huo huo, aliwagandamiza baadhi ya watu
Asa was angry with the seer. He was so angry with him over this that he put him in prison. At this same time Asa started to mistreat some of the people.
11 Tazma, matendo ya Asa, kutoka mwanzo hadi mwisho, tazama, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
The rest of what Asa did, from beginning to end, is written down in the Book of the Kings of Judah and Israel.
12 Katika mwaka wa thelathini na tisa wa utawala wake, Asa alipata ugnjwa kwenye miguu yake; ugonjwa wake ulikuwa mkali sana. Hata hivyo, hakutafuta msaada kutoka kwa Yahwe, lakini kutoka kwa waganga tu.
In the thirty-ninth year of his reign, Asa had trouble with disease in his feet, which only became worse and worse. Yet even in his sickness he did not turn to the Lord, but only the physicians.
13 Asa akalala pamoja na babu zake; alikufa katika mwaka wa arobaiani na moja wa utawala wake. Wakamzika katika kaburi lake, ambalo alilichimba mwenyewe katika mji wa Daudi.
Asa died in the forty-first year of his reign.
14 Walimlaza juu ya kitanda kilichokuwa kimewekewa manukato na aina mbali mbali ya dawa zilizotayarishwa na wale mafundi wa manukato. KIsha wakatengeneza moto kwa heshima yake.
He was buried in the tomb that he had prepared for himself in the City of David. They placed him on a bed full of spices, perfumed oils, and fragrances. Then they made a great fire to honor him.

< 2 Nyakati 16 >