< 2 Nyakati 15 >

1 Roho ya Mungu ikaja juu ya Azaria mwana wa Odedi.
L'Esprit de Dieu descendit sur Azaria, fils d'Oded.
2 Akaenda nje kukutana na Asa na akamwambia, “Nisikilize, Asa, na Yuda wote na Benyamini: Yahwe yuko pamoja nanyi, pale mnapokuwa naye. Kama mtamtafuta, mtampata; lakini kama mtamsahau, atawasahau ninyi.
Il alla à la rencontre d'Asa, et lui dit: « Écoute-moi, Asa, et tout Juda et Benjamin! Yahvé est avec vous tant que vous êtes avec lui; si vous le cherchez, vous le trouverez; mais si vous l'abandonnez, il vous abandonnera.
3 Sasa kwa muda mrefu, Israeli hawakuwa na Mungu wa kweli, bila kuhani wa kufundisha, na bila sheria.
Or, pendant longtemps, Israël a été sans le vrai Dieu, sans prêtre enseignant, et sans loi.
4 Lakini katika dhiki yao wakamrudia Yahwe, Mungu wa Israeli, na wakamtafuta, wakamta.
Mais quand, dans leur détresse, ils se sont tournés vers Yahvé, le Dieu d'Israël, et l'ont cherché, ils l'ont trouvé.
5 Katika nyakati hizo hapakuwa na amani kwake aliyesafiri kwend mbali, wala kwake aliyesafiri kuja hapa; badala yake shsida kubwa zilikuwa juu ya wenyeji wote wa wanchi.
En ces temps-là, il n'y avait pas de paix pour celui qui sortait et pour celui qui entrait, mais de grandes détresses pour tous les habitants des pays.
6 Waligawanyika vikundi vikundi, taifa dhidi ya taifa, na mji dhidi ya mji, kwa maana Mungu aliwapa shsida za kila aina ya kila mateso.
Ils furent mis en pièces, nation contre nation, et ville contre ville, car Dieu les troubla par toutes sortes d'épreuves.
7 Lakini muwe hodari, na msiuache mkono wenu kuwa dhaifu, kwa maana kazi yen itapewa thawabu.”
Mais vous, soyez forts! Ne laissez pas vos mains se relâcher, car votre travail sera récompensé. »
8 Asa aliposikia maneno haya, unabii wa odedi nabii, akajipa ujasiri na kuviondosha mbali vitu vya kuchukiza kutoka nchi yote ya Yuda na Benyamini, na kutoka miji yote aliyokuwa ameiteka kuanzia kilima cha nchi ya Efraimu, na akaijenga tena madhabahu ya Yahwe, ambayo ilikuwa mbele ya ukumbi wa nyumba ya Yahwe.
Lorsque Asa entendit ces paroles et la prophétie d'Oded le prophète, il prit courage et fit disparaître les abominations de tout le pays de Juda et de Benjamin et des villes qu'il avait prises dans la montagne d'Éphraïm, et il renouvela l'autel de l'Éternel qui était devant le portique de l'Éternel.
9 Akawakusanya Yuda wote na Benyamini, na wae waliokaa pamoja nao—watu wa kutoka Efraimu na Manase, na kutoka Simeoni. Kwa maana walikuja kwake katika hesabu kubwa kutoka Israeli, walipoona kwamba Yahwe Mungu wake alikuwa pamoja naye.
Il rassembla tout Juda et Benjamin, et ceux qui habitaient avec eux, d'Éphraïm, de Manassé et de Siméon, car ils étaient venus à lui en abondance d'Israël, quand ils virent que Yahvé son Dieu était avec lui.
10 Kwa hiyo wakakusanyika katika Yerusalemu katika mwezzi wa tatu, katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Asa.
Ils s'assemblèrent donc à Jérusalem au troisième mois, la quinzième année du règne d'Asa.
11 Katika siku hiyo walimtolea Yahwe dhabihu baadhi ya nyara ambazo walikuwa wameleta; ng'mbe wa kulima mia saba na kondoo na mbuzi elfu saba.
En ce jour-là, ils sacrifièrent à l'Éternel, sur le butin qu'ils avaient apporté, sept cents têtes de bétail et sept mille moutons.
12 Wakaingia kataika agano kwa ajili ya kumtafuta Yahwe, Mungu wa babau zao, kwa moyo wao wote na roho yao yote.
Ils conclurent l'alliance de chercher l'Éternel, le Dieu de leurs pères, de tout leur cœur et de toute leur âme;
13 Wakakubaliana kwamba yeyote atakepuuzia kumtafuta Yahwe, Mungu wa Israeli, atapaswa kuuawa, iwe mdogo ama mkubwa, iwe mwanaume ama mwanamke.
et que quiconque ne chercherait pas l'Éternel, le Dieu d'Israël, serait mis à mort, petit ou grand, homme ou femme.
14 Wakaapa kwa Yahwe kwa sauti kubwa, kwa kelele, na kwa sauti za tarumbeta na baragumu.
Ils jurèrent à l'Éternel d'une voix forte, en poussant des cris, avec des trompettes et des cornets.
15 Yuda wote wakakifurahia kile kiaapo. kwa maana walikuwa wameapa kwa moyo wao wote, na walimtafuta Mungu kwa nia yao yote, na walimuona. Yahwe akawapa amani pande zote.
Tout Juda se réjouit de ce serment, car ils avaient juré de tout leur cœur, ils l'avaient cherché de tout leur désir, et ils l'avaient trouvé. Alors Yahvé leur donna du repos tout autour.
16 Pia akamwondoa Maaka, asiwe malikia, kwa sababu alikuwa amefanya sanamu ya kuchukiza ya Maashera. Asa akaivunja vunja sanamu ya kuchukiza, akaiweka kwenye mavumbi akaichoma moto huko kijitoni Kidroni.
Il enleva aussi à Maaca, mère du roi Asa, le titre de reine-mère, parce qu'elle avait fait une image abominable d'Astarté; Asa abattit son image, la réduisit en poussière, et la brûla au torrent de Cédron.
17 Lakini sehemu za juu hazikuwa zimeondolewa nje ya Israeli. Vile vile, Moyo wa Asa ulijitoa kikamilifu siku zake zote.
Mais les hauts lieux ne furent pas enlevés d'Israël; cependant le cœur d'Asa fut parfait pendant toute sa vie.
18 Akaleta kwenye nyumba ya Mungu vitu vya baba yake na vitu vyake mwenyewe vilivyokuwa vya Yahwe: vitu vya fedha na dhahabu.
Il apporta à la maison de Dieu les choses que son père avait consacrées et qu'il avait lui-même consacrées, de l'argent, de l'or et des ustensiles.
19 Hapakuwa na vita zaidi hadi miaka thelathini na mitano ya utawala wa Asa.
Il n'y eut plus de guerre jusqu'à la trente-cinquième année du règne d'Asa.

< 2 Nyakati 15 >