< 2 Nyakati 15 >
1 Roho ya Mungu ikaja juu ya Azaria mwana wa Odedi.
And the spirit of God came upon Azarias the son of Oded,
2 Akaenda nje kukutana na Asa na akamwambia, “Nisikilize, Asa, na Yuda wote na Benyamini: Yahwe yuko pamoja nanyi, pale mnapokuwa naye. Kama mtamtafuta, mtampata; lakini kama mtamsahau, atawasahau ninyi.
And he went out to meet Asa, and said to him: Hear ye me, Asa, and all Juda and Benjamin: The Lord is with you, because you have been with him. If you seek him, you shall find: but if you forsake him, he will forsake you.
3 Sasa kwa muda mrefu, Israeli hawakuwa na Mungu wa kweli, bila kuhani wa kufundisha, na bila sheria.
And many days shall pass in Israel without the true God, and without a priest a teacher, and without the law.
4 Lakini katika dhiki yao wakamrudia Yahwe, Mungu wa Israeli, na wakamtafuta, wakamta.
And when in their distress they shall return to the Lord the God of Israel, and shall seek him, they shall find him.
5 Katika nyakati hizo hapakuwa na amani kwake aliyesafiri kwend mbali, wala kwake aliyesafiri kuja hapa; badala yake shsida kubwa zilikuwa juu ya wenyeji wote wa wanchi.
At that time there shall be no peace to him that goeth out and cometh in, but terrors on every side among all the inhabitants of the earth.
6 Waligawanyika vikundi vikundi, taifa dhidi ya taifa, na mji dhidi ya mji, kwa maana Mungu aliwapa shsida za kila aina ya kila mateso.
For nation shall fight against nation, and city against city, for the Lord will trouble them with all distress.
7 Lakini muwe hodari, na msiuache mkono wenu kuwa dhaifu, kwa maana kazi yen itapewa thawabu.”
Do you therefore take courage, and let not your hands he weakened: for there shall be a reward for your work.
8 Asa aliposikia maneno haya, unabii wa odedi nabii, akajipa ujasiri na kuviondosha mbali vitu vya kuchukiza kutoka nchi yote ya Yuda na Benyamini, na kutoka miji yote aliyokuwa ameiteka kuanzia kilima cha nchi ya Efraimu, na akaijenga tena madhabahu ya Yahwe, ambayo ilikuwa mbele ya ukumbi wa nyumba ya Yahwe.
And when Asa had heard the words, and the prophecy of Azarias the son of Oded the prophet, he took courage, and took away the idols out of all the land of Juda, and out of Benjamin, and out of the cities of mount Ephraim, which he had taken, and he dedicated the altar of the Lord, which was before the porch of the Lord.
9 Akawakusanya Yuda wote na Benyamini, na wae waliokaa pamoja nao—watu wa kutoka Efraimu na Manase, na kutoka Simeoni. Kwa maana walikuja kwake katika hesabu kubwa kutoka Israeli, walipoona kwamba Yahwe Mungu wake alikuwa pamoja naye.
And he gathered together all Juda and Benjamin, and the strangers with them of Ephraim, and Manasses, and Simeon: for many were come over to him out of Israel, seeing that the Lord his God was with him.
10 Kwa hiyo wakakusanyika katika Yerusalemu katika mwezzi wa tatu, katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Asa.
And when they were come to Jerusalem in the third month, in the fifteenth year of the reign of Asa,
11 Katika siku hiyo walimtolea Yahwe dhabihu baadhi ya nyara ambazo walikuwa wameleta; ng'mbe wa kulima mia saba na kondoo na mbuzi elfu saba.
They sacrificed to the Lord in that day of the spoils, and of the prey, that they had brought, seven hundred oxen, and seven thousand rams.
12 Wakaingia kataika agano kwa ajili ya kumtafuta Yahwe, Mungu wa babau zao, kwa moyo wao wote na roho yao yote.
And he went in to confirm as usual the covenant, that they should seek the Lord the God of their fathers with all their heart, and with all their soul.
13 Wakakubaliana kwamba yeyote atakepuuzia kumtafuta Yahwe, Mungu wa Israeli, atapaswa kuuawa, iwe mdogo ama mkubwa, iwe mwanaume ama mwanamke.
And if any one, said he, seek not the Lord the God of Israel, let him die, whether little or great, man or woman.
14 Wakaapa kwa Yahwe kwa sauti kubwa, kwa kelele, na kwa sauti za tarumbeta na baragumu.
And they swore to the Lord with a loud voice with joyful shouting, and with sound of trumpet, and sound of comets,
15 Yuda wote wakakifurahia kile kiaapo. kwa maana walikuwa wameapa kwa moyo wao wote, na walimtafuta Mungu kwa nia yao yote, na walimuona. Yahwe akawapa amani pande zote.
All that mere in Juda with a curse: for with all their heart they swore, and with all their will they sought him, and they found him, and the Lord gave them rest round about.
16 Pia akamwondoa Maaka, asiwe malikia, kwa sababu alikuwa amefanya sanamu ya kuchukiza ya Maashera. Asa akaivunja vunja sanamu ya kuchukiza, akaiweka kwenye mavumbi akaichoma moto huko kijitoni Kidroni.
Moreover Maacha the mother of king Asa he deposed from the royal authority, because she had made in a grove an idol of Priapus: and he entirely destroyed it, and breaking it into pieces, burnt it at the torrent Cedron.
17 Lakini sehemu za juu hazikuwa zimeondolewa nje ya Israeli. Vile vile, Moyo wa Asa ulijitoa kikamilifu siku zake zote.
But high places were left in Israel: nevertheless the heart of Asa was perfect all his days.
18 Akaleta kwenye nyumba ya Mungu vitu vya baba yake na vitu vyake mwenyewe vilivyokuwa vya Yahwe: vitu vya fedha na dhahabu.
And the things which his father had vowed, and he himself had vowed, he brought into the house of the Lord, gold and silver, and vessels of divers uses.
19 Hapakuwa na vita zaidi hadi miaka thelathini na mitano ya utawala wa Asa.
And there was no war unto the five and thirtieth year of the kingdom of Asa.