< 2 Nyakati 13 >

1 Katika mwaka wa kumi na nane wa Mfalme Yeroboamu, Abiya akaanza kutawala juu ya Yuda.
In the eighteenth year of King Jeroboam, Abijah began to reign over Judah.
2 Akatawala kwa miaka mitatu katika Yerusalemu; jina la mama yake aliitwa Maaka, binti wa Urieli wa Gibea. Kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
He ruled for three years in Jerusalem; his mother's name was Macaiah, the daughter of Uriel of Gibeah. There was war between Abijah and Jeroboam.
3 Abiya akaingia vitani na jeshi la askari, wenye nguvu, hodari, 400, 00 wanaume waliochaguliwa. Yeroboamu akapanga mistari ya vita dhidi yake yenye 800, 00 wanaume askari waliochaguliwa, wenye nguvu, hodari.
Abijah went into battle with an army of strong, courageous soldiers, 400,000 chosen men. Jeroboam placed battle lines against him with 800,000 chosen men, strong, courageous soldiers.
4 Abiya akasimama juu ya mlima Semaraimu, uliopo katika kilima cha nchi ya Efraimu, na akasema, “Nisikilizeni, Yeroboamu na Israeli wote!
Abijah stood on Mount Zemaraim, which is in the hill country of Ephraim, and said, “Listen to me, Jeroboam and all Israel!
5 Hamjui kwamba Yahwe, Mungu wa Israeli, alitoa sheria juu ya Israeli kwa Daudi milele, kwake na kwa wanaye kwa agano rasimi?
Do you not know that Yahweh, the God of Israel, gave the rule over Israel to David forever, to him and to his sons by a formal covenant?
6 Bado Yeroboamu mwana wa Nebati, mtumishi wa Selemani mwana wa Daudi, akainuka na kuasi dhidi ya bwana wake.
Yet Jeroboam son of Nebat, the servant of Solomon son of David, rose up and rebelled against his master.
7 Watu wabaya, washirika wa karibu, wakamkusanyikia, wakamjia kinyume Rehoboamu mwana wa Selemani, wakati Rehoboamu alipokuwa mdogo na asiye na uzoefu na hakuweza kuwamudu.
Worthless men, base fellows, gathered to him. They came against Rehoboam son of Solomon, when Rehoboam was young and inexperienced and could not withstand them.
8 Sasa mnasema kwamba mnaweza kuuzuia utawala wa Yahwe wenye nguvu katika mkono wa uzao wa Daudi. Ninyi ni jeshsi kubwa, na pamoja nanyi kuna ndama wa dhahabu ambao Yeroboamu alitengeneza kama miungu kwa ajili yenu.
So now you plan to resist the kingdom of Yahweh that is held within the hand of the descendants of David, because you are a large army, and you have the golden calves that Jeroboam made to be your gods.
9 Hamkuwafukuza nje makuhani wa Yahwe, uzao wa Haruni, na Walawi? Hamkujifanyia makuhani katika namna ya watu wa nchi zingine? Yeyote ajaye kujitakasa mwenyewe na ngo'mbe dume kijana, na madume ya kondoo anaweza kuwa kuhani wa kile ambacho siyo miungu.
But did you not drive out the priests of Yahweh, the descendants of Aaron, and the Levites, and make priests of your own in the same way as the people of other lands do? Whoever comes to serve as a priest, sacrificing a young bullock and seven rams, he becomes a priest of what are not gods.
10 Lakini kwetu, Yahwe ni Mungu wetu, na hatujamsahau. Tuna makuhani, uzao wa Haruni, wakimtumikia Yahwe, na Walawi, ambao wako kataika kazi yao.
But as for us, Yahweh is our God, and we have not forsaken him. We have priests, descendants of Aaron, serving Yahweh, and the Levites, who are at their work.
11 Kila asubuhi na jioni humtolea Yahwe sadaka za kuteketezwa na uvumba mtamu. Pia hupanga mkate wa uwepo juu ya meza takatifu; pia huweka kinara cha dhahabu pamoaja na taa zake, ili watoe sadaka kila jioni. sisi huzishika sheria za Yahwe, Mungu wetu, Lakini ninyi mmemsahau.
Every morning and evening they burn for Yahweh burnt offerings and sweet incense. They also arrange the bread of the presence on the pure table; they also tend the lampstand of gold with its lamps, for them to burn every evening. We keep the commandments of Yahweh, our God, but you have forsaken him.
12 Ona, Mungu yuko pamoja nasi katika vichwa vyetu, na makuhani wake wako hapa na tarumbeta kwa ajili ya kutoa sauti dhidi yenu. Watu wa Israeli, msipigane na Yahwe, Mungu wa babu zenu, kwa maana hamtafanikiwa.”
See, God is with us at our head, and his priests are here with the trumpets to sound an alarm against you. People of Israel, do not fight against Yahweh, the God of your ancestors, for you will not succeed.”
13 Lakini Yeroboamu akaandaa mavamizi nyuma yao; jeshi lake lilikuwa mbele ya Yuda, na wavamizi nyuma yao.
But Jeroboam prepared an ambush behind them; his army was in front of Judah, and the ambush was behind them.
14 Yuda walipoanagalia nyuma, tanzama, mapigano yalikuwa pote mbele na nyuma yao. Wakamlilia Yahwe kwa sauti, na makuhani wakayapuliza matarumbeta.
When Judah looked back, behold, the fighting was both in front of them and behind them. They cried out to Yahweh, and the priests blew the trumpets.
15 Kisha wanaume wa Yuda wakapiga kelele; walipopiga kele, ikawa kwamba Mungu akampiga Yeroboamu na Israeli wote mbele ya Abiya na Yuda.
Then the men of Judah gave a shout; as they shouted, it came about that God struck Jeroboam and all Israel before Abijah and Judah.
16 Watu wa Israeli wakakimbia mbele ya Yuda, na akawatia kwenye mkono wa Yuda.
The people of Israel fled before Judah, and God gave them into the hand of Judah.
17 Abiya na jeshi lake wakawaua kwa mauji makuu; 500, 000 watu wanaume waliochaguliwa wa Israeli wakaanguka wamekufa.
Abijah and his army killed them with great slaughter; 500,000 chosen men of Israel fell dead.
18 Katika namna hii hii, watu wa Israeli wakatiishwa chini wakati huo, watu wa Yuda wakashinda kwa sababu walimtegemea Yahwe, Mungu wa babu zao.
In this way, the people of Israel were subdued at that time; the people of Judah won because they relied on Yahweh, the God of their ancestors.
19 Abiya akamshawishi Yeroboamu; akachukua miji kutoka kwake; Betheli pamoja na vijiji vyake, Yeshana pamoja na vijiji vyake, na Efroni pamoaaja na vijij vyake.
Abijah pursued Jeroboam; he took cities from him: Bethel with its villages, Jeshanah with its villages, and Ephron with its villages.
20 Yeroboamu hakupata naguvu tena katika siku za Abiya; Yahwe akampiga, na akafa.
Jeroboam never recovered power again during the days of Abijah; Yahweh struck him, and he died.
21 Lakini Abiya akawa na nguvu sana; akachukua wanawake kumi na nne kwa ajili yake na akawa baba wa wana ishirini na mbili na mabinti kumi na sita.
But Abijah became powerful; he took fourteen wives for himself and became the father of twenty-two sons and sixteen daughters.
22 Matendo ya Abiya yaliyosalia, tabia yake na maneno yake yameeandikwa katika kamusi ya nabii Ido.
The rest of Abijah's deeds, his behavior, and words are written in the history of the prophet Iddo.

< 2 Nyakati 13 >