< 2 Nyakati 1 >

1 Selemani mwana wa Daudi, aliimariswa katika utawala wake, na Yahwe Mungu wake alikuwa pamoja naye na alimpa nguvu nyingi sana.
And Solomon son of David strengthens himself over his kingdom, and his God YHWH [is] with him, and makes him exceedingly great.
2 Sulemani akasema kwa Israleli wote, na maakida wa maelfu na wa mamia, na kwa waamuzi, na kwa kila mfalme kiongozi katika Israeli yote, wakuu wa kaya.
And Solomon says to all Israel, to heads of the thousands, and of the hundreds, and to the ones judging, and to every honorable one of all Israel, heads of the fathers,
3 Hivyo Sulemani na kusanyiko lote wakaenda pamoja naye sehemu ya juu iliyokuwa Gibeoni, maana ndipo palikuwepo hema ya kukutania ya Mungu, ambayo Musa mtumishi wa Yahwe, alikuwa ameitengeneza jangwani.
and they go—Solomon, and all the assembly with him—to the high place that [is] in Gibeon, for God’s Tent of Meeting has been there, that Moses, servant of YHWH, made in the wilderness,
4 Lakini Daudi alikuwa ameleta pale sanduku la Mungu kutoka Kiriath yeriam hadi sehemu ambayo alikuwa ametayarisha, maana alikuwa ameliandalia hema huko katika Yerusalemu.
but David had the Ark of God brought up from Kirjath-Jearim to the [place] David had prepared for it, for he stretched out a tent for it in Jerusalem;
5 Zaidi ya hayo, madhabahu ya shaba iliyotengenezwa na Bezaleli mwana wa uri mwana wa Huri ilikuwepo huko kabla ya mbele ya madhabahu ya Yahwe; Sulemani na kusanyiko wakaenda ilikokuwa. (Maandiko ya zamani yanasema
and the altar of bronze that Bezaleel son of Uri, son of Hur made, he put before the Dwelling Place of YHWH; and Solomon and the assembly seek Him [there].
6 Selemani akaenda huko kwenye kwenye madhabahu ya shaba mbele za Yahwe, ambayo ilikuwepo mahali pa hema ya kukutamia, na akatoa sadaka elfu za kuteketezwa juu yake.
And Solomon goes up there, on the altar of bronze, before YHWH, that [is] at the Tent of Meeting, and causes one thousand burnt-offerings to ascend on it.
7 Mungu akamtokea Selemani usiku huo na akasema kwake, “Omba! Nikupe nini?”
In that night God has appeared to Solomon and says to him, “Ask—what do I give to you?”
8 Selemani akasema kwa Mungu, “Umeonesha agano la uaminifu mkuu kwa Daudi baba yangu, na umenifanya mfalme katika nafasi yaye.
And Solomon says to God, “You have done great kindness with my father David, and have caused me to reign in his stead.
9 Sasa, Yahwe Mungu, ahadi yako kwa Daudi baba yangu itimie, maana umenifanya mfalme juu ya watu wengi kama mavumbi ya dunia.
Now, O YHWH God, Your word with my father David is steadfast, for You have caused me to reign over a people [as] numerous as the dust of the earth;
10 Sasa nipe hekima na maarifa, ili niweze kuwaongoza watu hawa, maana ni nani anayeweza kuwaamua watu wako, ambao ni wengi sana kwa idadi?”
now, give wisdom and knowledge to me, and I go out before this people, and I come in, for who judges this—Your great people?”
11 Mungu akasema kwa Selemani, “Kwa kuwa hili lilikuwa kwenye moyo wako, na kwa kuwa hujaomba mali, utajiri, au heshima, wala maisha ya wale wanaokuchukia, wala maish marefu kwa jili yako binafsi, lakini umeomba hekima na maarifa kwa ajili yako, ili uwatawale watu wangu, ambao juu yao nimekufanya mfame, na hivi ndivyo nitafanya.
And God says to Solomon, “Because that this has been with your heart, and you have not asked for riches, wealth, and honor, and the life of those hating you, and also have not asked for many days, and ask for wisdom and knowledge for yourself, so that you judge My people over which I have caused you to reign—
12 Sasa nitakupa hekima na maarifa, pia nitakupa mali na utajiri, na heshima, kuliko wafalme wote waliokuwepo kabla yako walivyokuwa, na baada yako hakuna yeyote atakayekuwa navyo.”
the wisdom and the knowledge is given to you, and riches and wealth and honor I [also] give to you, that there has not been so to the kings who [are] before you, and after you it is not so.”
13 Kwa hiyo Selemani akaenda Yerusalemu kutoka sehemu ya juu iliyokuwepo Gibeoni, kutoka mbele ya hema ya kukutania; akatawala juu ya Israeli.
And Solomon comes in to Jerusalem [from] the high place that [is] in Gibeon, from before the Tent of Meeting, and reigns over Israel,
14 Selemani akakusanya magari na wanaume waendesha farasi, naye alikuwa na magari 1, 400 na waendesha farasi kumi na mbili elfu ambao aliwaweka katika miji ya magari, pamoja naye, mfalme katika Yerusalemu.
and Solomon gathers chariots and horsemen, and he has one thousand and four hundred chariots, and twelve thousand horsemen, and he places them in the cities of the chariots, and with the king in Jerusalem.
15 Mfalme akatengeneza fedha na dhahabu kuwa vitu vya kawaida kama mawe katika Yerusalemu, na mbao za mierezi kuwa kama miti ya mikuyu iliyomo katika nyanda za chini.
And the king makes the silver and the gold in Jerusalem as stones, and the cedars he made as sycamores that [are] in the low country, for abundance.
16 Selemani katika uagizaji wa farasi kutoka Misiri, wafanya biashara wake walinunua farasi kutoka Misiri kwa bei stahiki.
And the source of the horses that [are] for Solomon [is] from Egypt and from Keva; merchants of the king take [them] from Keva at a price,
17 Waliagiza gari kutoka Misiri kwa shekeli mia sita za fedha, na farasi mmoja kwa shekeli 150. Pia walinunua kutoka kwa wafalme wa Wahiti na wafalme wa Washamu.
and they come up, and bring out a chariot from Egypt for six hundred pieces of silver, and a horse for one hundred and fifty, and so for all the kings of the Hittites and the kings of Aram—they bring [them] out by their hand.

< 2 Nyakati 1 >