< 1 Timotheo 1 >
1 Paulo, Mtume wa Kristo Yesu, kulingana na amri ya Mungu na Mwokozi wetu Yesu Kristo aliye ujasiri wetu,
PAUL, a legate of Jesus the Messiah, by the command of God our life-giver, and of the Messiah, Jesus our hope;
2 kwa Timotheo mwanangu wa kweli katika imani: Neema, rehema na amani zitokazo kwa Mungu Baba na Kristo Yesu Bwana wetu.
to Timothy, my true son in the faith: grace and mercy and peace, from God our Father, and the Messiah, Jesus our Lord.
3 Kama nilivyokusihi nilipoondoka kwenda Makedonia, ubaki Efeso ili kwamba uweze kuwaamru watu fulani wasifundishe mafundisho tofauti.
When I was going into Macedonia, I requested thee to remain at Ephesus, and to charge certain persons not to teach different doctrines;
4 Pia wasisikilize hadithi na orodha za nasaba zisizo na mwisho. Haya husababisha mabishano zaidi kuliko kuwasaidia kuendeleza mpango wa Mungu wa imani.
and not to throw themselves into fables and stories about genealogies, of which there is no end, which produce contention rather than edification in the faith of God.
5 Basi lengo la agizo hili ni upendo utokao katika moyo safi, katika dhamiri nzuri na katika imani ya kweli.
Now the end of the command is love, which is from a pure heart, and from a good conscience, and from true faith.
6 Baadhi ya watu wamelikosa lengo wakayaacha mafundisho haya na kugeukia mazungumzo ya kipumbavu.
But from these some have strayed, and have turned aside to vain words;
7 Wanataka kuwa waalimu wa sheria, lakini hawafahamu wanachosema au wanachosisitiza.
because they wished to be teachers of the law, while they understood not what they speak, nor the thing about which they contend.
8 lakini tunajua kwamba sheria ni njema kama mtu ataitumia kwa usahihi.
Now, we know, that the law is a good thing, if a man conduct himself in it, according to the law,
9 Tunajua kuwa, sheria haikutungwa kwa ajili ya mtu mwenye haki, bali kwa ajili ya wavunja sheria na waasi, watu wasio wataua na wenye dhambi, na ambao hawana Mungu na waovu. Imetungwa kwa ajili ya wauao baba na mama zao, kwa ajili ya wauaji,
he knowing that the law was not established for the righteous, but for the evil, and the rebellious, and the ungodly, and the sinful, and the perverse and for the impure, and for smiters of their fathers and smiters of their mothers, and for murderers,
10 kwa ajili ya waasherati, kwa ajili ya watu wazinzi, kwa ajili ya wale wanaoteka watu na kuwafanya watumwa, kwa ajili ya waongo, kwa ajili ya mashahidi wa uongo, na yeyote aliye kinyume na maelekezo ya uaminifu.
and for whoremongers, and for copulators with males, and for the stealers of free people, and for liars, and for violators of oaths, and for whatever is contrary to sound doctrine,
11 Malekezo haya yanatokana na injili yenye utukufu ya Mungu mwenye kubarakiwa ambayo kwayo nimeaminiwa.
namely that of the glorious gospel of the blessed God, with which I am intrusted.
12 Ninamshukuru Yesu Kristo Bwana wetu. Alinitia nguvu, kwa kuwa alinihesabu mimi kuwa mwaminifu, na akaniweka katika huduma.
And I thank him who strengthened me, even our Lord Jesus the Messiah; who accounted me faithful, and appointed me to his ministry;
13 Nilikuwa mtu wa kukufuru, mtesaji na mtu wa vurugu. Lakini nilipata rehema kwa sababu nilitenda kwa ujinga kwa kutoamini.
me I say, who before was a blasphemer, and a persecutor, and a reviler; but I obtained mercy, because I did it while ignorant and without faith.
14 Lakini neema ya Mungu wetu imejaa imani na upendo ulio katika Kristo Yesu.
And in me the grace of our Lord abounded, and faith and love, which is in Jesus the Messiah.
15 Ujumbe huu ni wa kuaminika na unastahili kupokelewa na wote, ya kuwa Kristo Yesu alikuja duniani kuokoa wenye dhambi. Mimi ni mbaya zaidi ya wote.
Faithful is the declaration, and worthy to be received, that Jesus the Messiah came into the world to give life to sinners, of whom I was the primary.
16 Lakini kwa sababu hii mimi nilipewa rehema ili kwamba ndani yangu mimi, awali ya yote, Kristo Yesu adhihirishe uvumilivu wote. Alifanya hivyo kama kielelezo kwa wote watakaomtumaini Yeye kwa ajili ya uzima wa milele. (aiōnios )
But for this cause had he mercy on me, that in me first Jesus the Messiah might display all his long suffering, for an example to them who were to believe on him unto life eternal. (aiōnios )
17 Na sasa kwa Mfalme asiye na ukomo, asiyekufa, asiyeonekana, Mungu pekee, iwe heshima na utukufu milele na milele. Amina. (aiōn )
And to the king eternal, incorruptible, and invisible, the sole God, be honor and glory for ever and ever! Amen. (aiōn )
18 Ninaliweka agizo hili mbele yako Timotheo, mtoto wangu. Nafanya hivi kulingana na unabii uliotolewa hapo kwanza kukuhusu wewe, ili kwamba uhusike katika vita njema.
This injunction I commit to thee, my son Timothy, according to the former predictions concerning thee, that in them thou mightest war this good warfare,
19 Fanya hivyo ili kwamba uwe na imani na dhamiri njema. Baadhi ya watu wameyakataa haya wakaangamiza imani.
in faith and a good conscience; for they who have repudiated this, have become destitute of faith;
20 Kama vile Himeneyo na Alekizanda ambao nimempa shetani ili wafundishwe wasikufuru.
like Hymeneus and Alexander, whom I have delivered up to Satan, that they may learn not to be blasphemers.