< 1 Timotheo 6 >
1 Wale wote walio chini ya nira kama watumwa wawachukulie mabwana zao kama wenye heshima zote, wanatakiwa kufanya hivyo ili jina la Mungu na mafundisho yasitukanwe.
Let those who are under the yoke as slaves esteem their masters as worthy of all honor, so that the name of God and the teachings be not blasphemed.
2 Watumwa wenye mabwana waaminio wasiwadharau kwa sababu wao ni ndugu. Badala yake, wawatumikie zaidi. Kwa sababu mabwana wanaosaidiwa kazi zao ni waamini na wanapendwa. Fundisha na kuyatangaza mambo haya.
Those whose masters are Christian believers must not treat them with disrespect, because they are brothers; nay, rather slave for them the better because those who get the benefit of their services are believing and beloved. Continue to teach and preach this.
3 Iwapo mtu fulani anafundisha kwa upotovu na hayapokei maelekezo yetu yenye kuaminika, ambayo ni maneno ya Bwana wetu Yesu Kristo, iwapo hawalikubali fundisho liongozalo kwenye utauwa.
If any one teaches heterodoxy, and refuses to consent to the wholesome words of the Lord Jesus Christ, and to the teachings of religion,
4 Mtu huyo anajivuna na hajui chochote. Badala yake, ana vurugu na mabishano juu ya maneno. Maneno haya huzaa wivu, ugomvi, matukano, shuku mbaya,
he is puffed up with conceit and knows nothing, but is doting about disputations and a strife of words. These give rise to envy, quarrels, railings, evil suspicions,
5 na vurugu za mara kwa mara kati ya watu wenye akili zilizoharibika. Wanaiacha kweli. Wanafikiri kwamba utauwa ni njia ya kuwa matajiri”
and wrangling between men whose minds are corrupt and destitute of the truth; who suppose that godliness is a source of gain.
6 Sasa utauwa na kuridhika ni faida kubwa.
Now godliness with contentment is truly gainful;
7 Kwa maana hatukuja na chochote duniani. Wala hatuwezi kuchukua chochote kutoka duniani.
for we have brought nothing into the world, and it is certain we can carry nothing out!
8 Badala yake, tutosheke na chakula na mavazi.
So if we have food and shelter, let us be content with that.
9 Sasa hao watakao kuwa na mali huanguka katika majaribu, katika mtego. Huanguka katika upumbavu mwingi na tamaa mbaya, na katika kitu chochote kinachowafanya watu wazame katika maangamizi na uharibifu.
Those who desire to be rich fall into the snares of temptation and many foolish and hurtful lusts, which drown men in destruction and perdition.
10 Kwa kuwa kupenda fedha ni chanzo cha aina zote za uovu. Watu ambao hutamani hiyo, wamepotoshwa mbali na imani na wamejichoma wenyewe kwa huzuni nyingi.
For the love of money is a source of all kinds of evil; and in their eager desire to be rich some have been led astray form the faith, and have pierced themselves with many sorrows.
11 Lakini wewe mtu wa Mungu, yakimbie mambo hayo. Fuata haki, utauwa, uaminifu, upendo, usitahimilivu, na upole.
But you, O servant of God, flee from these things, and run after integrity, piety, faith, love, stedfastness, gentleness.
12 Piga vita vizuri vya imani. Shikilia uzima wa milele ulioitiwa. Ilikuwa ni kwa sababu hii kwamba ulitoa ushuhuda mbele ya mashahidi wengi kwa kile kilicho chema. (aiōnios )
Keep contending in the noble contest of the faith; seize hold on eternal life, to which you were called when you confessed the good confession in the presence of many witnesses. (aiōnios )
13 Nakupa amri hii mbele za Mungu, anayesababisha vitu vyote kuishi, na mbele ya Yesu Kristo, aliyenena iliyo kweli kwa Pontio Pilato:
In the presence of God who gives life to all, and of Christ Jesus who bore witness to the good confession before Pontius Pilate,
14 itunze amri kwa ukamilifu, pasipo mashaka, hadi ujio wa Bwana wetu Yesu Kristo.
I charge you, keep your commission spotless and irreproachable until the appearing of our Lord Jesus Christ.
15 Mungu atadhihirisha ujio wake kwa wakati sahihi- Mungu, Mbarikiwa, nguvu pekee, Mfalme anayetawala, Bwana anayeongoza.
For in his own good time this will be brought about by that blessed and only potentate, King of kings and Lord of lords,
16 Peke yake anaishi milele na akaaye katika mwanga usiokaribiriwa. Hakuna mtu awezaye kumwona wala awezaye kumtazama. Kwake iwe heshima na uweza wa milele. Amina. (aiōnios )
who alone possesses immortality, who dwells in light that none can approach, whom no man has ever seen or can see; to whom be honor and power everlasting. Amen. (aiōnios )
17 Waambie matajiri katika ulimwengu huu wasijivune, na wasitumaini katika utajiri, ambao siyo wa uhakika. Badala yake, wanapaswa kumtumaini Mungu. Ambaye hutupatia utajiri wote wa kweli ili tufurahie. (aiōn )
Charge the rich of this world not to be supercilious, nor to trust in uncertain riches, but in God, who provides all things richly for our use. (aiōn )
18 Waambie watende mema, watajirike katika kazi njema, wawe wakarimu, na utayari wa kutoa.
Charge them to practise benevolence, to be rich in good works, to be open-handed and generous,
19 Katika njia hiyo watajiwekea msingi mzuri kwa mambo yajayo, ili kwamba waweze kushika maisha halisi.
laying up right good treasure for themselves in the world to come, in order that they may obtain the Life which is life indeed.
20 Timotheo, linda kile ulichopewa. Jiepushe na majadiliano ya kipumbavu na mabishano yenye kujipinga ambayo kwa kwa uongo huitwamaarifa.
O, Timothy, guard the treasure which is committed to you. Shun the profane babblings and contradictions of the falsely called "knowledge"
21 Baadhi ya watu huyatangaza mambo haya, na hivyo wameikosa imani. Neema na iwe pamoja nawe.
which some professing have erred from the faith. Grace be with you.