< 1 Timotheo 6 >

1 Wale wote walio chini ya nira kama watumwa wawachukulie mabwana zao kama wenye heshima zote, wanatakiwa kufanya hivyo ili jina la Mungu na mafundisho yasitukanwe.
LET as many slaves as are under the yoke account their own masters worthy of all honour, that the name of God and the doctrine be not blasphemed.
2 Watumwa wenye mabwana waaminio wasiwadharau kwa sababu wao ni ndugu. Badala yake, wawatumikie zaidi. Kwa sababu mabwana wanaosaidiwa kazi zao ni waamini na wanapendwa. Fundisha na kuyatangaza mambo haya.
But they who have believing masters, let them not think less of them, because they are brethren; but serve them the rather, because they are faithful and beloved, who have equally partaken of the benefit. These things teach and enjoin.
3 Iwapo mtu fulani anafundisha kwa upotovu na hayapokei maelekezo yetu yenye kuaminika, ambayo ni maneno ya Bwana wetu Yesu Kristo, iwapo hawalikubali fundisho liongozalo kwenye utauwa.
If any man teach another doctrine, and attend not to the sound words, which are those of Jesus Christ our Lord, and to the doctrine which is according to godliness;
4 Mtu huyo anajivuna na hajui chochote. Badala yake, ana vurugu na mabishano juu ya maneno. Maneno haya huzaa wivu, ugomvi, matukano, shuku mbaya,
he is conceited, knowing nothing, but delirious with disputes and quarrels about words, from whence come wrath, contentions, evil speakings, wrong suspicions,
5 na vurugu za mara kwa mara kati ya watu wenye akili zilizoharibika. Wanaiacha kweli. Wanafikiri kwamba utauwa ni njia ya kuwa matajiri”
perverse wranglings of men corrupt in mind, and destitute of truth, who think to make gain of godliness; depart from such men.
6 Sasa utauwa na kuridhika ni faida kubwa.
But godliness with contentment is great gain.
7 Kwa maana hatukuja na chochote duniani. Wala hatuwezi kuchukua chochote kutoka duniani.
For that we brought nothing into the world is evident, neither can we carry any thing out of it.
8 Badala yake, tutosheke na chakula na mavazi.
Having then food and raiment, let us be therewith content.
9 Sasa hao watakao kuwa na mali huanguka katika majaribu, katika mtego. Huanguka katika upumbavu mwingi na tamaa mbaya, na katika kitu chochote kinachowafanya watu wazame katika maangamizi na uharibifu.
For they who will be rich fall into temptation and a snare, and into many foolish and hurtful passions, which sink men in the abyss of destruction and perdition.
10 Kwa kuwa kupenda fedha ni chanzo cha aina zote za uovu. Watu ambao hutamani hiyo, wamepotoshwa mbali na imani na wamejichoma wenyewe kwa huzuni nyingi.
For the love of money is the root of all evils, which some coveting, have wandered away from the faith, and pierced themselves through with many sorrows.
11 Lakini wewe mtu wa Mungu, yakimbie mambo hayo. Fuata haki, utauwa, uaminifu, upendo, usitahimilivu, na upole.
But thou, O man of God, flee from these things; but pursue righteousness, godliness, faith, love, patience, meekness.
12 Piga vita vizuri vya imani. Shikilia uzima wa milele ulioitiwa. Ilikuwa ni kwa sababu hii kwamba ulitoa ushuhuda mbele ya mashahidi wengi kwa kile kilicho chema. (aiōnios g166)
Strain every nerve in the noble conflict of faith, lay fast hold on eternal life, unto which also thou hast been called, and hast confessed the good confession before many witnesses. (aiōnios g166)
13 Nakupa amri hii mbele za Mungu, anayesababisha vitu vyote kuishi, na mbele ya Yesu Kristo, aliyenena iliyo kweli kwa Pontio Pilato:
I conjure thee in the presence of God, who giveth life to all things, and of Christ Jesus, who witnessed that noble confession before Pontius Pilate;
14 itunze amri kwa ukamilifu, pasipo mashaka, hadi ujio wa Bwana wetu Yesu Kristo.
that thou observe this injunction spotless, irreproachable, unto the appearing of our Lord Jesus Christ:
15 Mungu atadhihirisha ujio wake kwa wakati sahihi- Mungu, Mbarikiwa, nguvu pekee, Mfalme anayetawala, Bwana anayeongoza.
which in his own appointed times he will shew forth, who is the blessed and only Potentate, the King of kings, and Lord of lords;
16 Peke yake anaishi milele na akaaye katika mwanga usiokaribiriwa. Hakuna mtu awezaye kumwona wala awezaye kumtazama. Kwake iwe heshima na uweza wa milele. Amina. (aiōnios g166)
who alone possesseth immortality, inhabiting light inaccessible, whom no man hath seen, nor can see: to whom be honour and glory eternal. Amen. (aiōnios g166)
17 Waambie matajiri katika ulimwengu huu wasijivune, na wasitumaini katika utajiri, ambao siyo wa uhakika. Badala yake, wanapaswa kumtumaini Mungu. Ambaye hutupatia utajiri wote wa kweli ili tufurahie. (aiōn g165)
Charge the rich in this world not to be lifted up with pride, nor to trust on the stability of wealth, but on the living God, who giveth us richly all things for our enjoyment; (aiōn g165)
18 Waambie watende mema, watajirike katika kazi njema, wawe wakarimu, na utayari wa kutoa.
to do good, to be rich in generous actions, to take pleasure in liberality, ready to distribute;
19 Katika njia hiyo watajiwekea msingi mzuri kwa mambo yajayo, ili kwamba waweze kushika maisha halisi.
laying up treasure for themselves a noble foundation against the time to come, that they may lay hold on eternal life.
20 Timotheo, linda kile ulichopewa. Jiepushe na majadiliano ya kipumbavu na mabishano yenye kujipinga ambayo kwa kwa uongo huitwamaarifa.
O Timothy, guard the sacred deposit, avoiding profane trifling talk, and antitheses of misnamed science:
21 Baadhi ya watu huyatangaza mambo haya, na hivyo wameikosa imani. Neema na iwe pamoja nawe.
which some affecting have erred concerning the faith. Grace be with thee.―Amen. The first epistle was written from Laodicea, which is the metropolis of Phrygia Pacatiana.

< 1 Timotheo 6 >