< 1 Timotheo 5 >

1 Usimkemee mwanamume mzee. Bali mtiye moyo kama baba yako. Uwatiye moyo vijana wa kiume kana kwamba ni ndugu zako.
Rebuke not an elder, but exhort him as a father; the younger men as brothers:
2 Uwatiye moyo wanawake wazee kama mama zako, na wanawake vijana kama dada zako kwa usafi wote.
the elderly women as mothers; the younger women as sisters, in all purity.
3 Waheshimu wajane, wale walio wajane kweli kweli.
Honor widows who are truly widows.
4 Lakini kama mjane ana watoto au wajukuu, waache kwanza wajifunze kuonesha heshima kwa watu wa nyumbani mwao wenyewe. Waache wawalipe wazazi wao mema, kwa kuwa hii inapendeza mbele za Mungu.
But if any widow has children, or grandchildren, let them first learn to show piety to their own house, and to give benefactions to their ancestors: for this is acceptable in the sight of God.
5 Lakini mjane kweli kweli ni yule aliyeachwa peke yake. Naye huweka tegemeo lake kwa Mungu. Siku zote hudumu katika sala na maombi usiku na mchana.
She who is truly a widow, and left alone, hopes in God, and abides in prayers and supplication night and day;
6 Hata hivyo, mwanamke yule aishiye kwa anasa amekufa, ingawaje yu hai.
but she who is wanton is dead though living.
7 Na uyahubiri haya mambo ili kwamba wasiwe na lawama.
Indeed command these things, in order that they may be blameless.
8 Ila kama mtu asipowatunza ndugu zake, hususani wale walioko nyumbani mwake, ameikana imani na ni mmbaya kuliko mtu asiye amini.
But if any one provides not for his own, and especially those of his own house, he has denied the faith, and is worse than an infidel.
9 Basi mwanamke aandikishwe kwenye orodha kama mjane akiwa na umri usiopungua miaka sitini, na ni mke wa mume mmoja.
Let a widow not be taken into account under three score years, the wife of one husband,
10 Lazima awe amejulikana kwa matendo mema, ikiwa ni kwamba amewajali watoto, au ameshakuwa mkarimu kwa wageni, au ameosha miguu ya waaminio, au alimesaidia ambao wamekuwa wakiteswa, au alijitoa kwa kazi yeyote njema.
being witness in beautiful works; if she has brought up children, if she has entertained strangers, if she has washed the feet of saints, if she has succored those in tribulation, if she has followed in every good work.
11 Lakini kwa wale wajane vijana, kataa kuwaandikisha kwenye orodha ya wajane. Kwa kuwa wakiingia kwenye matamanio ya kimwili dhidi ya Kristo, wanataka kuolewa.
But reject the younger widows: for when they may wax wanton against Christ, they wish to marry;
12 Kwa njia hii huingia kwenye hatia kwa kuwa huvunja kujitoa kwao kwa awali.
having condemnation, because they have rejected their first faith:
13 Na pia huingia kwenye mazoea ya uvivu. Wao huzunguka nyumba kwa nyumba. Si tu kwamba ni wavivu, bali pia huwa wasengenyaji na na wenye kuingilia mambo ya wengine. Wao husema mambo wasiyopaswa kuyasema.
and at the same time they learn to be idle, going about houses; and not only idle, but also loquacious even busybodies, speaking things which they ought not.
14 Kwa hiyo mimi nataka wanawake vijana waolewe, wazae watoto, wasimamie nyumba zao, ili kutokumpa adui nafasi ya kutushitaki kwa kufanya dhambi.
Therefore I wish the younger women to marry, to raise up children, to rule the house, to give no occasion to the adversary for the sake of reproach;
15 Kwa sababu baadhi yao wameshamgeukia Shetani.
for already certain ones have turned away after Satan.
16 Kama mwanamke yeyote aaminiye ana wajane, basi na awasaidie, ili kanisa lisilemewe, ili liweze kuwasaidia wale walio wajane kweli kweli.
If any faithful woman has widows, let her support them, and let not the church be burdened; in order that she may give her attention to those who are truly widows.
17 Basi wazee wale watawalao vyema wahesabiwe kuwa wamestahili heshima maradufu, hasa wale wanaojishughulisha na kufundisha neno la Mungu.
Let the elders who stand before the people beautifully, be considered worthy of double remuneration, especially those laboring in the word and teaching.
18 Kwa kuwa maandiko yanasema, “Usimfumbe ng'ombe kinywa apulapo nafaka,” na “Mfanya kazi anastahili mshahara wake.”
For the scripture says, Thou shalt not muzzle the ox that treadeth out the corn: and, The laborer is worthy of his hire.
19 Usipokee mashitaka dhidi ya mzee isipokuwa kuna mashahidi wawili au watatu.
Bring not an accusation against an elder, except before two or three witnesses.
20 Waonye wakosaji mbele ya watu wote ili wengine waliobaki labda wataogopa.
Convict those who sin before all, in order that the rest may also have fear.
21 Nakuagiza kwa dhati mbele ya Mungu, na mbele ya Kristo Yesu, na malaika wateule, kwamba uzitunze maagizo haya bila ubaguzi wowote, na kwamba usifanye jambo lolote kwa upendeleo.
I testify before God, and Jesus Christ, and the elect angels, that you must guard these things without prejudice, doing nothing by partiality.
22 Usimwekee mtu yeyote mikono haraka. Usishiriki dhambi ya mtu mwingine. Yakupasa kujitunza mwenyewe uwe usafi.
Lay hands quickly on no one, and be not partaker of other men's sins.
23 Hakupasi kunywa maji pekee. Badala yake, unywe mvinyo kidogo kwa ajili ya tumbo na magonjwa yako ya mara kwa mara.
Keep yourself pure. No longer drink water, but use a little wine for the sake of your stomach and on account of your frequent sickness.
24 Dhambi za baadhi ya watu hujulikana kwa uwazi, na huwatangulia hukumuni. Lakini baadhi ya dhambi hufuata baadaye.
The sins of some men are manifest beforehand, going before to judgment; and some men they also follow after:
25 Vivyo hivyo, baadhi ya kazi njema hujulikana kwa uwazi, lakini hata zingine hazitafichika.
likewise truly are good works manifested beforehand; and those which are otherwise are not able to be hidden.

< 1 Timotheo 5 >