< 1 Timotheo 5 >

1 Usimkemee mwanamume mzee. Bali mtiye moyo kama baba yako. Uwatiye moyo vijana wa kiume kana kwamba ni ndugu zako.
不要严厉责备比你年长之人,而是要像自己的父亲一样鼓励他;要像对待自己的兄弟一样,对待年轻人;
2 Uwatiye moyo wanawake wazee kama mama zako, na wanawake vijana kama dada zako kwa usafi wote.
将比你年长的妇人视为母亲,将年轻女人视为姐妹,遵守最高的礼仪标准。
3 Waheshimu wajane, wale walio wajane kweli kweli.
帮助失去家庭的寡妇。
4 Lakini kama mjane ana watoto au wajukuu, waache kwanza wajifunze kuonesha heshima kwa watu wa nyumbani mwao wenyewe. Waache wawalipe wazazi wao mema, kwa kuwa hii inapendeza mbele za Mungu.
如果寡妇有儿孙,应当让儿孙先在自己家里学习孝道,报答父母将其养大的恩情,因为这是基督徒的责任。这会让上帝感到喜悦。
5 Lakini mjane kweli kweli ni yule aliyeachwa peke yake. Naye huweka tegemeo lake kwa Mungu. Siku zote hudumu katika sala na maombi usiku na mchana.
至于真正的寡妇,没有家庭,没有人帮助,孤身一人,她们寄希望于上帝,日夜不停地祷告。
6 Hata hivyo, mwanamke yule aishiye kwa anasa amekufa, ingawaje yu hai.
但寡妇若只想享乐,那么她即使身体活着,也已经死了。
7 Na uyahubiri haya mambo ili kwamba wasiwe na lawama.
要向人们进行这样的指导,让其无可指摘。
8 Ila kama mtu asipowatunza ndugu zake, hususani wale walioko nyumbani mwake, ameikana imani na ni mmbaya kuliko mtu asiye amini.
但人若不照顾自己的亲属,尤其是自己的家人,就等于背弃信仰,比不信之人更糟糕。
9 Basi mwanamke aandikishwe kwenye orodha kama mjane akiwa na umri usiopungua miaka sitini, na ni mke wa mume mmoja.
只有年过六十、忠于自己丈夫的寡妇,才能被列入名单。
10 Lazima awe amejulikana kwa matendo mema, ikiwa ni kwamba amewajali watoto, au ameshakuwa mkarimu kwa wageni, au ameosha miguu ya waaminio, au alimesaidia ambao wamekuwa wakiteswa, au alijitoa kwa kazi yeyote njema.
这样的寡妇应有做善事的声誉:她是否好好地养育儿女?是否会招待客人?是否曾为圣徒洗脚,是否曾救济困苦之人?是否曾尽力行善?
11 Lakini kwa wale wajane vijana, kataa kuwaandikisha kwenye orodha ya wajane. Kwa kuwa wakiingia kwenye matamanio ya kimwili dhidi ya Kristo, wanataka kuolewa.
不能将年轻的寡妇列入这个名单,因为当身体的渴望让她们想要再嫁时,他们就会放弃对基督的献身。
12 Kwa njia hii huingia kwenye hatia kwa kuwa huvunja kujitoa kwao kwa awali.
因此她们因丢弃最初的承诺而有罪。
13 Na pia huingia kwenye mazoea ya uvivu. Wao huzunguka nyumba kwa nyumba. Si tu kwamba ni wavivu, bali pia huwa wasengenyaji na na wenye kuingilia mambo ya wengine. Wao husema mambo wasiyopaswa kuyasema.
而且她们懒惰惯了,走家串户。不但懒惰,而且好说闲话,好管闲事,说不该说的话。
14 Kwa hiyo mimi nataka wanawake vijana waolewe, wazae watoto, wasimamie nyumba zao, ili kutokumpa adui nafasi ya kutushitaki kwa kufanya dhambi.
因此,我非常建议年轻寡妇结婚,生儿育女,照顾家庭,不给敌人以批评的机会;
15 Kwa sababu baadhi yao wameshamgeukia Shetani.
但有些人已经追随了撒旦。
16 Kama mwanamke yeyote aaminiye ana wajane, basi na awasaidie, ili kanisa lisilemewe, ili liweze kuwasaidia wale walio wajane kweli kweli.
任何女基督徒的家中如果有寡妇,就应该救济她们,不要让教会因这责任而受累。这样,教会就可以救济那些真正有需要的寡妇了。
17 Basi wazee wale watawalao vyema wahesabiwe kuwa wamestahili heshima maradufu, hasa wale wanaojishughulisha na kufundisha neno la Mungu.
那些引导教会的长老,他们的价值应该加倍,尤其是那些进行讲道和传授工作的长老
18 Kwa kuwa maandiko yanasema, “Usimfumbe ng'ombe kinywa apulapo nafaka,” na “Mfanya kazi anastahili mshahara wake.”
正如经文所说:“牛在踩谷子的时候,不要笼住它的嘴。”还说:“做工就应该获得工钱。”
19 Usipokee mashitaka dhidi ya mzee isipokuwa kuna mashahidi wawili au watatu.
如果有人控诉长老,除非有两三个证人,否则不要相信。
20 Waonye wakosaji mbele ya watu wote ili wengine waliobaki labda wataogopa.
要当众责备那些罪人,对其他人也是一个警示。
21 Nakuagiza kwa dhati mbele ya Mungu, na mbele ya Kristo Yesu, na malaika wateule, kwamba uzitunze maagizo haya bila ubaguzi wowote, na kwamba usifanye jambo lolote kwa upendeleo.
在上帝和基督耶稣以及圣天使的面前,我指引你们要没有偏心地遵循这些指引,做任何事都不要采取偏袒的态度。
22 Usimwekee mtu yeyote mikono haraka. Usishiriki dhambi ya mtu mwingine. Yakupasa kujitunza mwenyewe uwe usafi.
不要匆忙地为别人按手,也不要陷入他人的罪之中,要保护自己的纯洁。
23 Hakupasi kunywa maji pekee. Badala yake, unywe mvinyo kidogo kwa ajili ya tumbo na magonjwa yako ya mara kwa mara.
如果你的胃不好,而且经常生病,不要只是喝水,可以稍微喝点酒。
24 Dhambi za baadhi ya watu hujulikana kwa uwazi, na huwatangulia hukumuni. Lakini baadhi ya dhambi hufuata baadaye.
有些人的罪非常明显,他们的罪行很确凿;有些人的罪是则是后来才显露出来。
25 Vivyo hivyo, baadhi ya kazi njema hujulikana kwa uwazi, lakini hata zingine hazitafichika.
同样,有些善行也很明显,即使有的善行隐藏起来,不久后也会显露出来。

< 1 Timotheo 5 >