< 1 Timotheo 4 >

1 Sasa Roho anasema waziwazi kwamba katika nyakati zijazo baadhi ya watu wataiacha imani na kuwa makini kusikiliza roho zidanganyazo na mafundisho ya kipepo yatakayofundishwa
But the Spirit says expressly that in later times some will fall away from the faith, paying attention to seducing spirits and doctrines of demons,
2 katika uongo na unafiki. Dhamiri zao zitabadilishwa.
through the hypocrisy of liars, branded in their own conscience as with a hot iron;
3 Watawazuia kuoa na kupokea vyakula ambavyo Mungu aliviumba vitumiwe kwa shukrani miongoni mwao waaminio na wenye kuijua kweli.
forbidding marriage and commanding to abstain from foods which God created to be received with thanksgiving by those who believe and know the truth.
4 Kwa sababu kila kitu ambacho Mungu amekiumba ni chema. Hakuna ambacho tunapokea kwa shukrani kinastahili kukataliwa.
For every creature of God is good, and nothing is to be rejected, if it is received with thanksgiving.
5 Kwa sababu kinatakaswa kupitia neno la Mungu na kwa njia ya maombi.
For it is sanctified through the word of God and prayer.
6 Kama utayaweka mambo haya mbele ya ndugu, utakuwa mtumishi mzuri wa Yesu Kristo. Kwa sababu umestawishwa kwa maneno ya imani na kwa mafundisho mazuri ambayo umeyafuata.
If you instruct the brothers of these things, you will be a good servant of Christ Jesus, nourished in the words of the faith, and of the good doctrine which you have followed.
7 Lakini zikatae hadithi za kidunia ambazo zinapendwa na wanawake wazee. Badala yake, jifunze mwenyewe katika utaua.
But have nothing to do with irreverent and silly myths. And train yourself for godliness.
8 Kwa maana mazoezi ya mwili yafaa kidogo, bali utauwa wafaa sana kwa mambo yote. Hutunza ahadi kwa maisha ya sasa na yale yajayo.
For bodily exercise has some value, but godliness has value in all things, having the promise of the life which is now, and of that which is to come.
9 Ujumbe huu ni wakuaminiwa na unastahili kukubaliwa kabisa.
This saying is faithful and worthy of all acceptance.
10 Kwa kuwa ni kwa sababu hii tunataabika na kufanya kazi kwa bidii sana. Kwa kuwa tunao ujasiri katika Mungu aliye hai, ambaye ni Mwokozi wa watu wote, lakini hasa kwa waaminio.
For to this end we both labor and strive, because we have set our trust in the living God, who is the Savior of all people, especially of those who believe.
11 Uyaseme na kuyafundisha mambo haya.
Command and teach these things.
12 Mtu yeyote asiudharau ujana wako. Badala yake, uwe mfano kwa wote waaminio, katika usemi, mwenendo, upendo, uaminifu, na usafi.
Let no one despise your youth; but be an example to those who believe, in word, in your way of life, in love, in faith, and in purity.
13 Mpaka nitakapokuja, dumu katika kusoma, katika kuonya, na katika kufundisha.
Until I come, pay attention to reading, to exhortation, and to teaching.
14 Usiipuuze karama iliyomo ndani yako, ambayo ulipewa kupitia unabii, kwa kuwekewa mikono na wazee.
Do not neglect the gift that is in you, which was given to you by prophecy, with the laying on of the hands of the elders.
15 Uyajali mambo haya. Ishi katika hayo ili kukua kwako kuwe dhahiri kwa watu wote. Zingatia sana mwenendo wako na mafundisho.
Be diligent in these things. Give yourself wholly to them, that your progress may be revealed to all.
16 Dumu katika mambo haya. Maana kwa kufanya hivyo utajiokoa mwenyewe na wale wanaokusikiliza.
Pay attention to yourself, and to your teaching. Continue in these things, for in doing this you will save both yourself and those who hear you.

< 1 Timotheo 4 >