< 1 Timotheo 1 >
1 Paulo, Mtume wa Kristo Yesu, kulingana na amri ya Mungu na Mwokozi wetu Yesu Kristo aliye ujasiri wetu,
Paul, an Apostle of Christ Jesus by the will of God our Saviour and Christ Jesus our hope:
2 kwa Timotheo mwanangu wa kweli katika imani: Neema, rehema na amani zitokazo kwa Mungu Baba na Kristo Yesu Bwana wetu.
To Timothy, my own true son in the faith. May grace, mercy and peace be granted to you from God the Father and Christ Jesus our Lord.
3 Kama nilivyokusihi nilipoondoka kwenda Makedonia, ubaki Efeso ili kwamba uweze kuwaamru watu fulani wasifundishe mafundisho tofauti.
When I was on my journey to Macedonia I begged you to remain on in Ephesus that you might remonstrate with certain persons because of their erroneous teaching
4 Pia wasisikilize hadithi na orodha za nasaba zisizo na mwisho. Haya husababisha mabishano zaidi kuliko kuwasaidia kuendeleza mpango wa Mungu wa imani.
and the attention they bestow on mere fables and endless pedigrees, such as lead to controversy rather than to a true stewardship for God, which only exists where there is faith. And I make the same request now.
5 Basi lengo la agizo hili ni upendo utokao katika moyo safi, katika dhamiri nzuri na katika imani ya kweli.
But the end sought to be secured by exhortation is the love which springs from a pure heart, a clear conscience and a sincere faith.
6 Baadhi ya watu wamelikosa lengo wakayaacha mafundisho haya na kugeukia mazungumzo ya kipumbavu.
From these some have drifted away, and have wandered into empty words.
7 Wanataka kuwa waalimu wa sheria, lakini hawafahamu wanachosema au wanachosisitiza.
They are ambitious to be teachers of the Law, although they do not understand either their own words or what the things are about which they make such confident assertions.
8 lakini tunajua kwamba sheria ni njema kama mtu ataitumia kwa usahihi.
Now we know that the Law is good, if a man uses it in the way it should be used,
9 Tunajua kuwa, sheria haikutungwa kwa ajili ya mtu mwenye haki, bali kwa ajili ya wavunja sheria na waasi, watu wasio wataua na wenye dhambi, na ambao hawana Mungu na waovu. Imetungwa kwa ajili ya wauao baba na mama zao, kwa ajili ya wauaji,
and remembers that a law is not enacted to control a righteous man, but for the lawless and rebellious, the irreligious and sinful, the godless and profane--for those who strike their fathers or their mothers, for murderers,
10 kwa ajili ya waasherati, kwa ajili ya watu wazinzi, kwa ajili ya wale wanaoteka watu na kuwafanya watumwa, kwa ajili ya waongo, kwa ajili ya mashahidi wa uongo, na yeyote aliye kinyume na maelekezo ya uaminifu.
fornicators, sodomites, slave-dealers, liars and false witnesses; and for whatever else is opposed to wholesome teaching
11 Malekezo haya yanatokana na injili yenye utukufu ya Mungu mwenye kubarakiwa ambayo kwayo nimeaminiwa.
and is not in accordance with the Good News of the blessed God with which I have been entrusted.
12 Ninamshukuru Yesu Kristo Bwana wetu. Alinitia nguvu, kwa kuwa alinihesabu mimi kuwa mwaminifu, na akaniweka katika huduma.
I am thankful to Him who made me strong--even Christ Jesus our Lord--because He has judged me to be faithful and has put me into His service,
13 Nilikuwa mtu wa kukufuru, mtesaji na mtu wa vurugu. Lakini nilipata rehema kwa sababu nilitenda kwa ujinga kwa kutoamini.
though I was previously a blasphemer and a persecutor and had been insolent in outrage. Yet mercy was shown me, because I had acted ignorantly, not having as yet believed;
14 Lakini neema ya Mungu wetu imejaa imani na upendo ulio katika Kristo Yesu.
and the grace of our Lord came to me in overflowing fulness, conferring faith on me and the love which is in Christ Jesus.
15 Ujumbe huu ni wa kuaminika na unastahili kupokelewa na wote, ya kuwa Kristo Yesu alikuja duniani kuokoa wenye dhambi. Mimi ni mbaya zaidi ya wote.
Faithful is the saying, and deserving of universal acceptance, that Christ Jesus came into the world to save sinners; among whom I stand foremost.
16 Lakini kwa sababu hii mimi nilipewa rehema ili kwamba ndani yangu mimi, awali ya yote, Kristo Yesu adhihirishe uvumilivu wote. Alifanya hivyo kama kielelezo kwa wote watakaomtumaini Yeye kwa ajili ya uzima wa milele. (aiōnios )
But mercy was shown me in order that in me as the foremost of sinners Christ Jesus might display the fulness of His long-suffering patience as an example to encourage those who would afterwards be resting their faith on Him with a view to the Life of the Ages. (aiōnios )
17 Na sasa kwa Mfalme asiye na ukomo, asiyekufa, asiyeonekana, Mungu pekee, iwe heshima na utukufu milele na milele. Amina. (aiōn )
Now to the immortal and invisible King of the Ages, who alone is God, be honour and glory to the Ages of the Ages! Amen. (aiōn )
18 Ninaliweka agizo hili mbele yako Timotheo, mtoto wangu. Nafanya hivi kulingana na unabii uliotolewa hapo kwanza kukuhusu wewe, ili kwamba uhusike katika vita njema.
This is the charge which I entrust to you, my son Timothy, in accordance with the inspired instructions concerning you which were given me long ago, that being equipped with them as your armour you may be continually fighting the good fight,
19 Fanya hivyo ili kwamba uwe na imani na dhamiri njema. Baadhi ya watu wameyakataa haya wakaangamiza imani.
holding fast to faith and a clear conscience, which some have cast aside and have made shipwreck of their faith.
20 Kama vile Himeneyo na Alekizanda ambao nimempa shetani ili wafundishwe wasikufuru.
Among these are Hymenaeus and Alexander, whom I have delivered to Satan so that they may be taught not to blaspheme.