< 1 Wathesalonike 1 >
1 Paulo, Silwano na Timotheo kwa kanisa la Wathesalonike katika Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo. Neema na amani iwe nanyi.
Pavel in Silvan in Timotej občini Tesaloničanov v Bogu očetu in Gospodu Jezusu Kristusu; milost vam in mir od Boga očeta našega in Gospoda Jezusa Kristusa!
2 Tunatoa shukrani kwa Mungu kila mara kwa ajili yenu nyote, wakati tunapowataja katika maombi yetu.
Zahvaljujemo se Bogu vedno za vas vse, spominjajoč se vas v molitvah svojih,
3 Tunaikumbuka bila kukoma mbele ya Mungu na baba yetu kazi yenu ya imani, juhudi ya upendo, na uvumilivu wenye ujasiri kwa ajili ya baadaye katika Bwana Yesu Kristo.
Neprestano spominjajoč se dela vašega v veri in truda v ljubezni, in stanovitnosti v tipanji Gospoda našega Jezusa Kristusa, pred Bogom in očetom našim;
4 Ndugu Mnaopendwa na Mungu, tunajua wito wenu.
Vedóč, bratje ljubljeni od Boga, za izvoljenje vaše;
5 Na jinsi injili yetu ilivyokuja kwenu si kwa neno tu, bali pia katika nguvu, katika Roho Mtakatifu, na katika uhakika. Kwa namna hiyo, mnajua pia sisi tulikuwa watu wa namna gani miongoni mwenu kwa ajili yenu.
Da evangelj naš ni prišel samo v besedi do vas, nego tudi v moči in v Duhu svetem, in v mnogem prepričanji, kakor veste, kakošni smo med vami postali za vas.
6 Mlikuwa watu wa kutuiga sisi na Bwana, kama mlivyopokea neno katika taabu kwa furaha itokayo kwa Roho Mtakatifu.
In vi ste postali posnemalci naši in Gospodovi, sprejemši besedo, v mnogi stiski z veseljem Duha svetega,
7 Na matokeo yake, mkawa mfano kwa wote katika Makedonia na Akaiya ambao wanaamini.
Tako da ste postali zgled vsem verujočim v Macedoniji in Ahaji.
8 Kwa kuwa kutoka kwenu neno la Mungu limeenea kote, na si kwa Mekadonia na Akaiya peke yake. Badala yake, kwa kila mahali imani yenu katika Mungu imeenea kote. Na matokeo yake, hatuhitaji kusema chochote.
Kajti od vas je zadonela beseda Gospodova ne samo po Macedoniji in Ahaji, nego tudi v vsakem kraji razširila se je vaša vera v Boga, tako da nam ni treba kaj govoriti.
9 Kwa kuwa wao wenyewe wanaarifu ujio wetu ulikuwa wa namna gani kati yenu. Wanasimulia jinsi mulivyomgeukia Mungu kutoka katika sanamu na kumtumikia Mungu aliye hai na wa kweli.
Kajti sami oznanjajo za nas, kak smo imeli prihod k vam, in kako ste se obrnili k Bogu od malikov, služit Bogu živemu in resničnemu,
10 Walitoa habari kuwa mnamsubiri Mwana wake kutoka mbinguni, aliyefufuliwa kutoka kwa wafu. Na huyu ni Yesu, anayetuweka huru kutoka kwenye ghadhabu ijayo.
In čakat sina njegovega iz nebés, katerega je zbudil izmed mrtvih, Jezusa, ki nas rešuje jeze prihodnje.