< 1 Wathesalonike 1 >
1 Paulo, Silwano na Timotheo kwa kanisa la Wathesalonike katika Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo. Neema na amani iwe nanyi.
Paul, Silvanus, and Timothy, to the church of the Thessalonians in God the Father and the Lord Jesus (the) Messiah: Grace to you and peace.
2 Tunatoa shukrani kwa Mungu kila mara kwa ajili yenu nyote, wakati tunapowataja katika maombi yetu.
We always give thanks to God for all of you, mentioning you in our prayers,
3 Tunaikumbuka bila kukoma mbele ya Mungu na baba yetu kazi yenu ya imani, juhudi ya upendo, na uvumilivu wenye ujasiri kwa ajili ya baadaye katika Bwana Yesu Kristo.
remembering without ceasing your work of faith and labor of love and patience of hope in our Lord Jesus (the) Messiah, before our God and Father.
4 Ndugu Mnaopendwa na Mungu, tunajua wito wenu.
We know, brothers loved by God, that you are chosen,
5 Na jinsi injili yetu ilivyokuja kwenu si kwa neno tu, bali pia katika nguvu, katika Roho Mtakatifu, na katika uhakika. Kwa namna hiyo, mnajua pia sisi tulikuwa watu wa namna gani miongoni mwenu kwa ajili yenu.
and that our gospel came to you not in word only, but also in power, and in the Holy Spirit, and with much assurance. You know what kind of persons we showed ourselves to be among you for your sake.
6 Mlikuwa watu wa kutuiga sisi na Bwana, kama mlivyopokea neno katika taabu kwa furaha itokayo kwa Roho Mtakatifu.
You became imitators of us, and of the Lord, having received the word in much affliction, with joy of the Holy Spirit,
7 Na matokeo yake, mkawa mfano kwa wote katika Makedonia na Akaiya ambao wanaamini.
so that you became an example to all who believe in Macedonia and in Achaia.
8 Kwa kuwa kutoka kwenu neno la Mungu limeenea kote, na si kwa Mekadonia na Akaiya peke yake. Badala yake, kwa kila mahali imani yenu katika Mungu imeenea kote. Na matokeo yake, hatuhitaji kusema chochote.
For from you the word of the Lord has been declared, not only in Macedonia and Achaia, but also in every place your faith toward God has gone out; so that we do not need to say anything.
9 Kwa kuwa wao wenyewe wanaarifu ujio wetu ulikuwa wa namna gani kati yenu. Wanasimulia jinsi mulivyomgeukia Mungu kutoka katika sanamu na kumtumikia Mungu aliye hai na wa kweli.
For they themselves report concerning us what kind of a reception we had from you; and how you turned to God from idols, to serve a living and true God,
10 Walitoa habari kuwa mnamsubiri Mwana wake kutoka mbinguni, aliyefufuliwa kutoka kwa wafu. Na huyu ni Yesu, anayetuweka huru kutoka kwenye ghadhabu ijayo.
and to wait for his Son from heaven, whom he raised from the dead—Jesus, who delivers us from the wrath to come.