< 1 Wathesalonike 5 >

1 Sasa, kwa habari ya muda na nyakati, ndugu, hamna haja kwamba kitu chochote kiandikwe kwenu.
But concerning the times and the seasons, brethren, ye have no need that aught be written unto you.
2 Kwa kuwa ninyi wenyewe mwajua kwa usahihi ya kuwa siku ya Bwana inakuja kama mwizi ajapo usiku.
For yourselves know perfectly that the day of the Lord so cometh as a thief in the night.
3 Pale wasemapo kuna “Amani na usalama”, ndipo uharibifu huwajia ghafla. Ni kama utungu umjiavyo mama mwenye mimba. Hawataepuka kwa njia yeyote.
When they are saying, Peace and safety, then sudden destruction cometh upon them, as travail upon a woman with child; and they shall in no wise escape.
4 Lakini ninyi, ndugu hampo kwenye giza hata ile siku iwajie kama mwizi.
But ye, brethren, are not in darkness, that that day should overtake you as a thief:
5 Kwa maana ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi siyo wana wa usiku au wa gizani.
for ye are all sons of light, and sons of the day: we are not of the night, nor of darkness;
6 Hivyo basi, tusilale kama wengine walalavyo. Bali tukeshe na kuwa makini.
so then let us not sleep, as do the rest, but let us watch and be sober.
7 Kwa kuwa wanaolala hulala usiku na wanao lewa hulewa usiku.
For they that sleep sleep in the night; and they that be drunken are drunken in the night.
8 Kwa kuwa sisi ni wana wa mchana, tuwe makini. Tuvae ngao ya imani na upendo, na, kofia ya chuma, ambayo ni uhakika wa wokovu wa wakati ujao.
But let us, since we are of the day, be sober, putting on the breastplate of faith and love; and for a helmet, the hope of salvation.
9 Kwa kuwa Mungu hakutuchagua mwanzo kwa ajili ya gadhabu, bali kwa kupata wokovu kwa njia ya Bwana Yesu Kristo.
For God appointed us not unto wrath, but unto the obtaining of salvation through our Lord Jesus Christ,
10 Yeye ndiye aliyetufia ili kwamba, tukiwa macho au tumelala, tutaishi pamoja naye.
who died for us, that, whether we wake or sleep, we should live together with him.
11 Kwa hiyo, farijianeni na kujengana ninyi kwa ninyi, kama ambavyo tayari mnafanya.
Wherefore exhort one another, and build each other up, even as also ye do.
12 Ndugu, twawaomba muwatambue wale wanaotumika miongoni mwenu na wale walio juu yenu katika Bwana na wale wanao washauri.
But we beseech you, brethren, to know them that labour among you, and are over you in the Lord, and admonish you;
13 Tunawaomba pia muwatambue na kuwapa heshima katika upendo kwa sababu ya kazi yao. Muwe na amani miongoni mwenu ninyi wenyewe.
and to esteem them exceeding highly in love for their work’s sake. Be at peace among yourselves.
14 Twawasihi, ndugu: muwaonye wasio kwenda kwa utaratibu, watieni moyo walio kata tamaa, Wasaidieni walio wanyonge, na muwe wavumilivu kwa wote.
And we exhort you, brethren, admonish the disorderly, encourage the fainthearted, support the weak, be longsuffering toward all.
15 Angalieni asiwepo mtu yeyote anayelipa baya kwa baya kwa mtu yeyote. Badala yake, fanyeni yaliyo mema kwa kila mmoja wenu na kwa watu wote.
See that none render unto any one evil for evil; but alway follow after that which is good, one toward another, and toward all.
16 Furahini siku zote.
Rejoice alway;
17 Ombeni bila kukoma.
pray without ceasing;
18 Mshukuruni Mungu kwa kila jambo, kwa sababu hayo ndiyo mapenzi ya Mungu kwenu katika Yesu Kristo.
in everything give thanks: for this is the will of God in Christ Jesus to you-ward.
19 Msimzimishe Roho.
Quench not the Spirit;
20 Msiudharau unabii.
despise not prophesyings;
21 Yajaribuni mambo yote. Mlishike lililo jema.
prove all things; hold fast that which is good;
22 Epukeni kila mwonekano wa uovu.
abstain from every form of evil.
23 Mungu wa amani awakamilishe katika utakatifu. Roho, nafsi na mwili vitunzwe pasipo mawaa katika kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
And the God of peace himself sanctify you wholly; and may your spirit and soul and body be preserved entire, without blame at the coming of our Lord Jesus Christ.
24 Yeye aliyewaita ni mwaminifu, naye ndiye mwenye kutenda.
Faithful is he that calleth you, who will also do it.
25 Ndugu, tuombeeni pia.
Brethren, pray for us.
26 Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu.
Salute all the brethren with a holy kiss.
27 Nawasihi katika Bwana kwamba barua hii isomwe kwa ndugu wote.
I adjure you by the Lord that this epistle be read unto all the brethren.
28 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nanyi.
The grace of our Lord Jesus Christ be with you.

< 1 Wathesalonike 5 >