< 1 Wathesalonike 5 >
1 Sasa, kwa habari ya muda na nyakati, ndugu, hamna haja kwamba kitu chochote kiandikwe kwenu.
But concerning the times and the seasons, brothers, you have no need that anything be written to you.
2 Kwa kuwa ninyi wenyewe mwajua kwa usahihi ya kuwa siku ya Bwana inakuja kama mwizi ajapo usiku.
For you yourselves know well that the day of the Lord comes like a thief in the night.
3 Pale wasemapo kuna “Amani na usalama”, ndipo uharibifu huwajia ghafla. Ni kama utungu umjiavyo mama mwenye mimba. Hawataepuka kwa njia yeyote.
Now when they are saying, "Peace and safety," then sudden destruction will come on them, like birth pains on a pregnant woman; and they will in no way escape.
4 Lakini ninyi, ndugu hampo kwenye giza hata ile siku iwajie kama mwizi.
But you, brothers, are not in darkness, that the day should overtake you like a thief.
5 Kwa maana ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi siyo wana wa usiku au wa gizani.
You are all sons of light, and sons of the day. We do not belong to the night, nor to darkness,
6 Hivyo basi, tusilale kama wengine walalavyo. Bali tukeshe na kuwa makini.
so then let us not sleep, as the rest do, but let us watch and be sober.
7 Kwa kuwa wanaolala hulala usiku na wanao lewa hulewa usiku.
For those who sleep, sleep in the night, and those who are drunk are drunk in the night.
8 Kwa kuwa sisi ni wana wa mchana, tuwe makini. Tuvae ngao ya imani na upendo, na, kofia ya chuma, ambayo ni uhakika wa wokovu wa wakati ujao.
But let us, since we belong to the day, be sober, putting on the breastplate of faith and love, and, for a helmet, the hope of salvation.
9 Kwa kuwa Mungu hakutuchagua mwanzo kwa ajili ya gadhabu, bali kwa kupata wokovu kwa njia ya Bwana Yesu Kristo.
For God did not appoint us to wrath, but to the obtaining of salvation through our Lord Jesus Christ,
10 Yeye ndiye aliyetufia ili kwamba, tukiwa macho au tumelala, tutaishi pamoja naye.
who died for us, that, whether we wake or sleep, we should live together with him.
11 Kwa hiyo, farijianeni na kujengana ninyi kwa ninyi, kama ambavyo tayari mnafanya.
Therefore exhort one another, and build each other up, even as you also do.
12 Ndugu, twawaomba muwatambue wale wanaotumika miongoni mwenu na wale walio juu yenu katika Bwana na wale wanao washauri.
But we ask you, brothers, to recognize those who labor among you, and are over you in the Lord, and admonish you,
13 Tunawaomba pia muwatambue na kuwapa heshima katika upendo kwa sababu ya kazi yao. Muwe na amani miongoni mwenu ninyi wenyewe.
and to respect and honor them in love for their work's sake. Be at peace among yourselves.
14 Twawasihi, ndugu: muwaonye wasio kwenda kwa utaratibu, watieni moyo walio kata tamaa, Wasaidieni walio wanyonge, na muwe wavumilivu kwa wote.
We exhort you, brothers, admonish the disorderly, encourage the fainthearted, support the weak, be patient toward all.
15 Angalieni asiwepo mtu yeyote anayelipa baya kwa baya kwa mtu yeyote. Badala yake, fanyeni yaliyo mema kwa kila mmoja wenu na kwa watu wote.
See that no one returns evil for evil to anyone, but always seek what is good both for each other and for all.
18 Mshukuruni Mungu kwa kila jambo, kwa sababu hayo ndiyo mapenzi ya Mungu kwenu katika Yesu Kristo.
In everything give thanks, for this is the will of God in Christ Jesus toward you.
Do not quench the Spirit.
Do not treat prophecies with contempt,
21 Yajaribuni mambo yote. Mlishike lililo jema.
but test all things; hold firmly that which is good.
22 Epukeni kila mwonekano wa uovu.
Abstain from every form of evil.
23 Mungu wa amani awakamilishe katika utakatifu. Roho, nafsi na mwili vitunzwe pasipo mawaa katika kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
May the God of peace himself sanctify you completely. May your whole spirit, soul, and body be preserved blameless at the coming of our Lord Jesus Christ.
24 Yeye aliyewaita ni mwaminifu, naye ndiye mwenye kutenda.
He who calls you is faithful, who will also do it.
Brothers, pray for us also.
26 Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu.
Greet all the brothers with a holy kiss.
27 Nawasihi katika Bwana kwamba barua hii isomwe kwa ndugu wote.
I solemnly command you by the Lord that this letter be read to all the holy brothers.
28 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nanyi.
The grace of our Lord Jesus Christ be with you.