< 1 Wathesalonike 5 >
1 Sasa, kwa habari ya muda na nyakati, ndugu, hamna haja kwamba kitu chochote kiandikwe kwenu.
BUT of the times and the seasons, brethren, ye have no need that I write unto you.
2 Kwa kuwa ninyi wenyewe mwajua kwa usahihi ya kuwa siku ya Bwana inakuja kama mwizi ajapo usiku.
For yourselves know perfectly that the day of the Lord so cometh as a thief in the night.
3 Pale wasemapo kuna “Amani na usalama”, ndipo uharibifu huwajia ghafla. Ni kama utungu umjiavyo mama mwenye mimba. Hawataepuka kwa njia yeyote.
For when they shall say, Peace and safety; then sudden destruction cometh upon them, as travail upon a woman with child; and they shall not escape.
4 Lakini ninyi, ndugu hampo kwenye giza hata ile siku iwajie kama mwizi.
But ye, brethren, are not in darkness, that that day should overtake you as a thief.
5 Kwa maana ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi siyo wana wa usiku au wa gizani.
Ye are all the children of light, and the children of the day: we are not of the night, nor of darkness.
6 Hivyo basi, tusilale kama wengine walalavyo. Bali tukeshe na kuwa makini.
Therefore let us not sleep, as do others; but let us watch and be sober.
7 Kwa kuwa wanaolala hulala usiku na wanao lewa hulewa usiku.
For they that sleep sleep in the night; and they that be drunken are drunken in the night.
8 Kwa kuwa sisi ni wana wa mchana, tuwe makini. Tuvae ngao ya imani na upendo, na, kofia ya chuma, ambayo ni uhakika wa wokovu wa wakati ujao.
But let us, who are of the day, be sober, putting on the breastplate of faith and love; and for an helmet, the hope of salvation.
9 Kwa kuwa Mungu hakutuchagua mwanzo kwa ajili ya gadhabu, bali kwa kupata wokovu kwa njia ya Bwana Yesu Kristo.
For God hath not appointed us to wrath, but to obtain salvation by our Lord Jesus Christ,
10 Yeye ndiye aliyetufia ili kwamba, tukiwa macho au tumelala, tutaishi pamoja naye.
Who died for us, that, whether we wake or sleep, we should live together with him.
11 Kwa hiyo, farijianeni na kujengana ninyi kwa ninyi, kama ambavyo tayari mnafanya.
Wherefore comfort yourselves together, and edify one another, even as also ye do.
12 Ndugu, twawaomba muwatambue wale wanaotumika miongoni mwenu na wale walio juu yenu katika Bwana na wale wanao washauri.
And we beseech you, brethren, to know them which labour among you, and are over you in the Lord, and admonish you;
13 Tunawaomba pia muwatambue na kuwapa heshima katika upendo kwa sababu ya kazi yao. Muwe na amani miongoni mwenu ninyi wenyewe.
And to esteem them very highly in love for their work’s sake. And be at peace among yourselves.
14 Twawasihi, ndugu: muwaonye wasio kwenda kwa utaratibu, watieni moyo walio kata tamaa, Wasaidieni walio wanyonge, na muwe wavumilivu kwa wote.
Now we exhort you, brethren, warn them that are unruly, comfort the feebleminded, support the weak, be patient toward all men.
15 Angalieni asiwepo mtu yeyote anayelipa baya kwa baya kwa mtu yeyote. Badala yake, fanyeni yaliyo mema kwa kila mmoja wenu na kwa watu wote.
See that none render evil for evil unto any man; but ever follow that which is good, both among yourselves, and to all men.
18 Mshukuruni Mungu kwa kila jambo, kwa sababu hayo ndiyo mapenzi ya Mungu kwenu katika Yesu Kristo.
In every thing give thanks: for this is the will of God in Christ Jesus concerning you.
Despise not prophesyings.
21 Yajaribuni mambo yote. Mlishike lililo jema.
Prove all things; hold fast that which is good.
22 Epukeni kila mwonekano wa uovu.
Abstain from all appearance of evil.
23 Mungu wa amani awakamilishe katika utakatifu. Roho, nafsi na mwili vitunzwe pasipo mawaa katika kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
And the very God of peace sanctify you wholly; and I pray God your whole spirit and soul and body be preserved blameless unto the coming of our Lord Jesus Christ.
24 Yeye aliyewaita ni mwaminifu, naye ndiye mwenye kutenda.
Faithful is he that calleth you, who also will do it.
26 Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu.
Greet all the brethren with an holy kiss.
27 Nawasihi katika Bwana kwamba barua hii isomwe kwa ndugu wote.
I charge you by the Lord that this epistle be read unto all the holy brethren.
28 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nanyi.
The grace of our Lord Jesus Christ be with you. Amen. The first epistle unto the Thessalonians was written from Athens. THE