< 1 Wathesalonike 5 >

1 Sasa, kwa habari ya muda na nyakati, ndugu, hamna haja kwamba kitu chochote kiandikwe kwenu.
Maar over tijden en stonden, broeders, behoeft u niet te worden geschreven.
2 Kwa kuwa ninyi wenyewe mwajua kwa usahihi ya kuwa siku ya Bwana inakuja kama mwizi ajapo usiku.
Want zelf weet gij goed, dat de Dag des Heren komt als een dief in de nacht.
3 Pale wasemapo kuna “Amani na usalama”, ndipo uharibifu huwajia ghafla. Ni kama utungu umjiavyo mama mwenye mimba. Hawataepuka kwa njia yeyote.
Wanneer men zegt: "Vrede en veiligheid," dan valt op hen het verderf onverwacht, zoals barensweeën op een zwangere vrouw; en ontkomen doen ze zeker niet.
4 Lakini ninyi, ndugu hampo kwenye giza hata ile siku iwajie kama mwizi.
Maar gij broeders, gij verkeert niet in duisternis, zodat de Dag u als een dief zou verrassen.
5 Kwa maana ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi siyo wana wa usiku au wa gizani.
Want allen zijt gij zonen van het licht, zonen ook van de dag; van nacht of duisternis zijn we het niet.
6 Hivyo basi, tusilale kama wengine walalavyo. Bali tukeshe na kuwa makini.
Slapen we dus niet als de anderen, maar laten we waken en nuchter blijven.
7 Kwa kuwa wanaolala hulala usiku na wanao lewa hulewa usiku.
Want wie slapen, slapen ‘s nachts; en die zich bedrinken, bedrinken zich ‘s nachts.
8 Kwa kuwa sisi ni wana wa mchana, tuwe makini. Tuvae ngao ya imani na upendo, na, kofia ya chuma, ambayo ni uhakika wa wokovu wa wakati ujao.
Maar wij moeten nuchter blijven, want we zijn zonen van de dag; toegerust met het pantser van geloof en van liefde, en met de helm, de hoop op de zaligheid.
9 Kwa kuwa Mungu hakutuchagua mwanzo kwa ajili ya gadhabu, bali kwa kupata wokovu kwa njia ya Bwana Yesu Kristo.
Want God heeft ons niet bestemd voor de Toorn, maar tot het verwerven der zaligheid door onzen Heer Jesus Christus,
10 Yeye ndiye aliyetufia ili kwamba, tukiwa macho au tumelala, tutaishi pamoja naye.
die voor ons is gestorven, opdat we, wakend of slapend, samen met Hem zouden leven.
11 Kwa hiyo, farijianeni na kujengana ninyi kwa ninyi, kama ambavyo tayari mnafanya.
Troost dus elkander, sticht ook elkander, zoals gij gewoon zijt te doen.
12 Ndugu, twawaomba muwatambue wale wanaotumika miongoni mwenu na wale walio juu yenu katika Bwana na wale wanao washauri.
We verzoeken u, broeders, hen te waarderen, die onder u arbeiden, die u vóórgaan, en terechtwijzen in den Heer;
13 Tunawaomba pia muwatambue na kuwapa heshima katika upendo kwa sababu ya kazi yao. Muwe na amani miongoni mwenu ninyi wenyewe.
acht ze ook meer dan gewone liefde waardig om hun arbeid. Bewaart de vrede onder elkander.
14 Twawasihi, ndugu: muwaonye wasio kwenda kwa utaratibu, watieni moyo walio kata tamaa, Wasaidieni walio wanyonge, na muwe wavumilivu kwa wote.
Broeders, we sporen u aan: berispt de leeglopers, bemoedigt de kleinmoedigen, ondersteunt de zwakken, weest jegens allen geduldig.
15 Angalieni asiwepo mtu yeyote anayelipa baya kwa baya kwa mtu yeyote. Badala yake, fanyeni yaliyo mema kwa kila mmoja wenu na kwa watu wote.
Past op, dat niemand kwaad met kwaad vergeldt; maar streeft allen het goede na jegens elkander en jegens allen.
16 Furahini siku zote.
Weest altijd blijde.
17 Ombeni bila kukoma.
Bidt zonder ophouden;
18 Mshukuruni Mungu kwa kila jambo, kwa sababu hayo ndiyo mapenzi ya Mungu kwenu katika Yesu Kristo.
brengt dankzegging voor alles; want dit is voor u Gods wil in Christus Jesus.
19 Msimzimishe Roho.
Blust den Geest niet uit,
20 Msiudharau unabii.
versmaadt de profetieën niet;
21 Yajaribuni mambo yote. Mlishike lililo jema.
maar onderzoekt alles, en behoudt het goede.
22 Epukeni kila mwonekano wa uovu.
Onthoudt u van kwaad onder iedere vorm.
23 Mungu wa amani awakamilishe katika utakatifu. Roho, nafsi na mwili vitunzwe pasipo mawaa katika kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
Dan moge de God van de vrede zelf u heiligen heel en al; uw geest, uw ziel en uw lichaam blijve ongerept bewaard en onberispelijk tot de komst van Jesus Christus onzen Heer.
24 Yeye aliyewaita ni mwaminifu, naye ndiye mwenye kutenda.
Hij die roept, is ook getrouw; Hij zal het ook ten uitvoer brengen.
25 Ndugu, tuombeeni pia.
Bidt voor ons, broeders.
26 Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu.
Groet al de broeders met een heilige kus.
27 Nawasihi katika Bwana kwamba barua hii isomwe kwa ndugu wote.
Ik bezweer u bij den Heer, de brief aan al de broeders voor te lezen.
28 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nanyi.
De genade van onzen Heer Jesus Christus zij met u!

< 1 Wathesalonike 5 >