< 1 Wathesalonike 4 >

1 Hatimaye, ndugu, twawatia moyo na kuwasihi kwa Yesu Kristo. Kama mlivyopokea maelekezo toka kwetu namna iwapasavyo kuenenda na kumpendeza Mungu, kwa njia hiyo pia muenende na kutenda zaidi.
ARI, ri ai kan, je pil poeki re omail o panaui kin komail Kaun Iejuj, duen me komail aleer jan kit, o duen me komail en kekeideki wei, o kaperenda Kot, iduen omail kakairida.
2 Kwa kuwa mwajua ni maelekezo gani tuliyowapa kupitia Bwana Yesu.
Pwe komail aja duen kujoned akan, me je pan on komail ren Kaun Iejuj.
3 Kwa kuwa haya ndiyo mapenzi ya Mungu: utakaso wenu - kwamba muepuke zinaa,
Pwe iet kupur en Kot, omail jarauila, pwe komail en liki jan nenek.
4 Kwamba kila mmoja wenu anajua namna ya kumiliki mke wake mwenyewe katika utakatifu na heshima.
Amen amen en kanai on pein war a, pwen jaraui o wau o liki jan inon jued,
5 Usiwe na mke kwa ajili ya tamaa za mwili (kama Mataifa wasiomjua Mungu).
Kaidin ni dender on inon jued duen men liki kan, me jo aja Kot;
6 Asiwepo mtu yeyote atakaye vuka mipaka na kumkosea nduguye kwa ajili ya jambo hili. Kwa kuwa Bwana ndiye mwenye kulipa kisasi kwa mambo yote haya, kama tulivyo tangulia kuwaonya na kushuhudia.
O jota me pan piti de kajapuni on ri a ni meakot, pwe Kaun o pan kotin iki on i, duen me kit inda o kadede on komail er maj o.
7 Kwa kuwa Bwana hakutuita kwa uchafu, bali kwa utakatifu.
Pwe Kot jota molipei kitail on jamin, a pwen jaraui.
8 Kwa hiyo anayelikataa hili hawakatai watu, bali anamkataa Mungu, anayewapa Roho Mtakatifu wake.
A ma amen komail pan mamaleki mepukat, kaidin aramaj me a pan mamaleki pwe Kot, me pil kotiki on komail er japwilim a Nen jaraui.
9 Kuhusu upendo wa ndugu, hakuna haja ya mtu yeyote kukuandikia, kwa kuwa mmefundishwa na Mungu kupendana ninyi kwa ninyi.
A duen limpok en jaulan, menda i en intinki won komail, pwe pein komail padakki jan ren Kot, me komail en pokepena.
10 Hakika, mlifanya haya yote kwa ndugu walioko Makedonia yote, lakini twawasihi, ndugu, mfanye hata na zaidi.
Nan met komail kin wiai on jaulan karoj, me mimi Majetonien pon. A je panaui kin komail ri at akan, komail en kakairida.
11 Twawasihi mtamani kuishi maisha ya utulivu, kujali shughuli zenu, na kufanya kazi kwa mikono yenu, kama tulivyowaamuru.
O komail nenenla o inon ion apwali pein omail dodok, kadokeki pein pa omail, duen me je padaki on komail er,
12 Fanya haya ili uweze kuenenda vizuri na kwa heshima kwa hao walio nje ya imani, ili usipungukiwe na hitaji lolote.
Pwe komail en janjal mau mon me mi liki kan, o komail der mau on amen en apwali komail.
13 Hatutaki ninyi muelewe isivyo sahihi, enyi ndugu, juu ya hao waliolala, ili msije mkahuzunika kama wengine wasio na uhakika kuhusu wakati ujao.
Ri ai kan, je jota men oki jan komail duen me mairelar akan, pwe komail der injenjued dueta irail, me jota ar kaporopor.
14 Iwapo tunaamini kuwa Yesu alikufa na akafufuka tena, vivyo hivyo Mungu atawaleta pamoja na Yesu hao waliolala mauti katika yeye.
Pwe ma kitail kamelele, me Iejuj matala ap iajadar, nan iduen me mairelar ren Iejuj, Kot pil pan kalua ir ala re a.
15 Kwa ajili ya hayo twawaambia ninyi kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaokuwepo wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wale waliolala mauti.
Pwe ieteten me je indan komail ni majan en Kaun o, kit me memaureta lao Kaun o pan kotin pwarado, jota pan ko wei mon me mair akan.
16 Kwa kuwa Bwana mwenyewe atashuka toka mawinguni. Atakuja na sauti kuu, pamoja na sauti ya malaika mkuu, pamoja na parapanda ya Mungu, nao waliokufa katika Kristo watafufuka kwanza.
Pwe pein Kaun o pan kotido jan nanlan ki majan laud, o kapiti en toulan lapalap amen, o koronete en Kot; me melar akan ren Krijtuj ap pan maureda maj.
17 Kisha sisi tulio hai, tuliobaki, tutaungana katika mawingu pamoja nao kumlaki Bwana hewani. Kwa njia hii tutakuwa na Bwana siku zote.
Kit me memaureta luadi ap pan ian ir peukadala nan dapok kan, ko on ren Kaun o nan wawa, kitail ap pan mimieta ren Kaun o kokolata.
18 Kwa hiyo, mfarijiane ninyi kwa ninyi kwa maneno haya.
Komail ari kamaiteki komail la padak pot et.

< 1 Wathesalonike 4 >