< 1 Wathesalonike 1 >

1 Paulo, Silwano na Timotheo kwa kanisa la Wathesalonike katika Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo. Neema na amani iwe nanyi.
Paul, Silvanus, and Timothy, to the church of the Thessalonians in God the Father and the Lord Jesus Christ: Grace to you and peace from God our Father and the Lord Jesus Christ.
2 Tunatoa shukrani kwa Mungu kila mara kwa ajili yenu nyote, wakati tunapowataja katika maombi yetu.
We always give thanks to God for you all, making mention of you in our prayers,
3 Tunaikumbuka bila kukoma mbele ya Mungu na baba yetu kazi yenu ya imani, juhudi ya upendo, na uvumilivu wenye ujasiri kwa ajili ya baadaye katika Bwana Yesu Kristo.
remembering without ceasing, in the presence of our God and Father, your work of faith, your labor of love, and your endurance of hope in our Lord Jesus Christ.
4 Ndugu Mnaopendwa na Mungu, tunajua wito wenu.
For we know, brothers beloved by God, that you have been chosen,
5 Na jinsi injili yetu ilivyokuja kwenu si kwa neno tu, bali pia katika nguvu, katika Roho Mtakatifu, na katika uhakika. Kwa namna hiyo, mnajua pia sisi tulikuwa watu wa namna gani miongoni mwenu kwa ajili yenu.
because our gospel did not come to you in word only, but also in power and in the Holy Spirit and with much conviction. You know what sort of men we proved to be among you for your sake.
6 Mlikuwa watu wa kutuiga sisi na Bwana, kama mlivyopokea neno katika taabu kwa furaha itokayo kwa Roho Mtakatifu.
And you became imitators of us and of the Lord when you received the word in much affliction with the joy of the Holy Spirit.
7 Na matokeo yake, mkawa mfano kwa wote katika Makedonia na Akaiya ambao wanaamini.
As a result you have become examples to all the believers in Macedonia and Achaia.
8 Kwa kuwa kutoka kwenu neno la Mungu limeenea kote, na si kwa Mekadonia na Akaiya peke yake. Badala yake, kwa kila mahali imani yenu katika Mungu imeenea kote. Na matokeo yake, hatuhitaji kusema chochote.
For not only has the word of the Lord sounded forth from you in Macedonia and Achaia, but reports of your faith in God have gone out everywhere, so that we have no need to say anything about it.
9 Kwa kuwa wao wenyewe wanaarifu ujio wetu ulikuwa wa namna gani kati yenu. Wanasimulia jinsi mulivyomgeukia Mungu kutoka katika sanamu na kumtumikia Mungu aliye hai na wa kweli.
For the people themselves report what kind of reception we had among you, and how you turned away from idols to serve the living and true God,
10 Walitoa habari kuwa mnamsubiri Mwana wake kutoka mbinguni, aliyefufuliwa kutoka kwa wafu. Na huyu ni Yesu, anayetuweka huru kutoka kwenye ghadhabu ijayo.
as you wait for his Son Jesus to return from heaven, whom God raised from the dead, and who rescues us from the coming wrath.

< 1 Wathesalonike 1 >