< 1 Samweli 9 >

1 Basi kulikuwa na mtu mmoja kutoka Benyamini, mtu mashuhuri. Jina lake aliitwa Kishi mwana wa Abieli, mwana wa Zerori, mwana wa Bekorathi, mwana wa Afia, mwana wa Mbenyamini.
There was nowe a man of Beniamin, mightie in power named Kish, the sonne of Abiel, the sonne of Zeror, the sonne of Bechorath, the sonne of Aphiah, the sonne of a man of Iemini.
2 Huyu alikuwa na mtoto wa kiume aliyeitwa Sauli, kijana mzuri wa uso. Hapakuwapo mwanaume mzuri wa uso kuliko huyu miongoni mwa watu wote wa Israeli. Kutoka mabegani kwenda juu alikuwa mrefu kuliko watu wengine.
And he had a sonne called Saul, a goodly yong man and a faire: so that among the children of Israel there was none goodlier then he: from the shoulders vpwarde he was hier then any of the people.
3 Na punda wa Kishi, baba yake na Sauli walipotea. hivyo Kishi akamwambia Sauli mwanawe, “Mchukue mmoja wa watumishi; uamke uende kuwatafuta punda,”
And the asses of Kish Sauls father were lost: therefore Kish said to Saul his sonne, Take nowe one of the seruants with thee, and arise, goe, and seeke the asses.
4 Sauli akapita katika nchi ya vilima vilima ya Efraimu na akaenda akapita katika nchi ya Shalisha, lakini hawakuwaona. Kisha walipita katika nchi ya Shaalimu, lakini hawakuwa huko. Baadaye alipita katika nchi ya Wabenyamini, lakini hawakuwaona wale punda.
So he passed through mount Ephraim, and went through the lande of Shalishah, but they found them not. Then they went through the land of Shalim, and there they were not: he went also through ye land of Iemini, but they found the not.
5 Na walipofika nchi ya Sufu, Sauli alimwambia mtumishi wake aliyekuwa naye, “Njoo na turudi, pengine baba aweza kuacha kuchunga punda na kuanza kutuhofia sisi.”
When they came to the lande of Zuph, Saul saide vnto his seruant that was with him, Come and let vs returne, lest my father leaue the care of asses, and take thought for vs.
6 Lakini mtumishi akamwmbia, “Sikiliza, Yupo mtu wa Mungu katika mji huu. Naye ni mtu wa kuheshimiwa sana; kila asemalo huwa kweli. Hebu twende huko; labda anaweza kutuambia tupitie wapi katika safari yetu.”
And he said vnto him, Behold nowe, in this citie is a man of God, and he is an honorable man: all that he saith commeth to passe: let vs nowe goe thither, if so be that he can shewe vs what way we may goe.
7 Ndipo Sauli akamwambia mtumish iwake, “Lakini kama tukienda kwake, twaweza kumpelekea nini? Maana hata mkate katika mfuko wetu umekwisha, na hakuna zawadi ya kumpelekea mtumishi wa Mungu. Tuna kitu gani?
Then saide Saul to his seruant, Well then, let vs goe: but what shall we bring vnto the man? For the bread is spent in our vessels, and there is no present to bring to the man of God: what haue we?
8 Huyo mtumishi akamjibu Sauli na kusema, “Hapa, ninayo robo ya shekeli ya fedha ambayo nitampa mtumishi wa Mungu, atuambie ni njia ipi yatupasa tuiendee.”
And the seruant answered Saul againe, and said, Beholde, I haue founde about me the fourth part of a shekell of siluer: that will I giue the man of God, to tell vs our way.
9 (Zamani katika Israeli, mtu alipotaka kujua neno kuhusu mapenzi ya Mungu, alisema, “Njoo, haya twende kwa mwonaji.” Kwa maana nabii wa leo, zamani aliitwa Mwonaji).
(Beforetime in Israel when a man went to seeke an answere of God, thus he spake, Come, and let vs goe to the Seer: for he that is called nowe a Prophet, was in the olde time called a Seer)
10 Ndipo Sauli akamwambia mtumishi wake, “Umesema vyema. Haya, njoo twende.” Basi wakaenda katika mji ambao mtu wa Mungu alikuwamo.
Then saide Saul to his seruant, Well saide, come, let vs goe: so they went into the citie where the man of God was.
11 Walipopanda mlima kuelekea mjini, walikutana na wasichana wakienda kuteka maji; Sauli na mtumishi wake wakawauliza, “Mwonaji hupo hapa?”
And as they were going vp the hie way to the citie, they found maydes that came out to draw water, and said vnto them, Is there here a Seer?
12 Nao wakawajibu, na kusema, “Yupo; tazameni, yuko mbele yenu. Harakisheni, kwa maana anakuja mjini leo, sababu leo watu wanatoa dhabihu zao mahali pa juu.
And they answered them, and said, Yea: loe, he is before you: make haste nowe, for he came this day to the citie: for there is an offering of the people this day in the hie place.
13 Mara tu mtakapoingia mjini mtamuona, kabla hajapanda mahali pa juu kla chakula. Watu hawatakula hata atakapokuja, kwa sababu ndiye ataibariki dhabihu; na baadaye wale ambao wamealikwa hula. Basi pandeni, mtamuona sasa hivi.”
When ye shall come into the citie, ye shall finde him straightway yet he come vp to the hie place to eate: for the people will not eate vntill he come, because he will blesse the sacrifice: and then eate they that be bidden to the feast: nowe therefore goe vp: for euen now shall ye find him.
14 Kwa hiyo walikwea kwenda mjini. Walipokuwa wakiingia mjini, walimuona Samweli akija mbele yao, akipanda kwenda mahali pa juu.
Then they went vp into the citie, and when they were come into the middes of the citie, Samuel came out against them, to goe vp to the hie place.
15 Siku moja kabla Sauli hajafika, BWANA alikuwa amemfunulia Samweli:
But the Lord had reueiled to Samuel secretly (a day before Saul came) saying,
16 “Kesho wakati kama huu nitakutumia mtu kutoka nchi ya Benyamini, nawe utamtia mafuta awe mfalme juu ya watu wangu Israeli. Atawaokoa watu wangu kutoka mkono wa Wafilisti. Kwa kuwa nimewaonea huruma watu wangu na kilio cha kutaka msaada kimenifikia.”
To morow about this time I will send thee a man out of the land of Beniamin: him shalt thou anoint to be gouernour ouer my people Israel, that he may saue my people out of the hands of the Philistims: for I haue looked vpon my people, and their crie is come vnto me.
17 Samweli alipomuona Sauli, BWANA akamwambia, “Huyu ndiye mtu niliyekwambia habari zake! Yeye ndiye atakayewatawala watu wangu.”
When Samuel therefore sawe Saul, the Lord answered him, See, this is the man whom I spake to thee of, he shall rule my people.
18 Ndipo Sauli akaja karibu na Samweli katika lango na kusema, “Niambie nyumba ya Mwonaji iko wapi?
Then went Saul to Samuel in the middes of the gate, and said, Tell me, I pray thee, where the Seers house is.
19 Samweli akamjibu Sauli akisema, “Mimi ndiye mwonaji. Tangulia mbele hadi mahali pa juu, nami nitakueleza kila kitu kilichomoyoni mwako.
And Samuel answered Saul, and saide, I am the Seer: goe vp before me vnto the hie place: for ye shall eate with me to day. and to morowe I will let thee goe, and will tell thee all that is in thine heart.
20 Kama punda wenu waliopotea siku tatu zilizopita, msihofu kuhusu hao punda, kwa kuwa wamekwishapatikana. Na yote yaliyotamanika kwa ajili ya Israeli yanamwangukia nani? Siyo kwako na nyumba ya baba yako yote?”
And as for thine asses that were lost three dayes ago, care not for them: for they are founde. and on whom is set all the desire of Israel? is it not vpon thee and on all thy fathers house?
21 Sauli akamjibu na kusema, Siyo mimi Mbenyamini, kutoka kabila lililo dogo sana kwa makabila ya Israeli? Siyo ukoo wangu ulio mdogo sana kwa kabila la Benyamini? Kwa nini basi unaniambia kwa namna hii?”
But Saul answered, and said, Am not I the sonne of Iemini of the smallest tribe of Israel? and my familie is the least of all the families of the tribe of Beniamin. Wherefore then speakest thou so to me?
22 Hivyo Samweli akamchukua Sauli na mtumishi wake, akawaingiza ukumbini, akawakalisha mahali pa heshima pa wale walioalikwa, idadi yao takribani watu thelathini.
And Samuel tooke Saul and his seruant, and brought them into the chamber, and made them sit in the chiefest place among them that were bidden: which were about thirtie persons.
23 Samweli akamwambia mpishi, “Lete sehemu niliyokupatia, sehemu ambayo nilikwambia hivi, “Itenge.”'
And Samuel saide vnto the cooke, Bring foorth the portion which I gaue thee, and whereof I said vnto thee, Keepe it with thee.
24 Basi mpishi alichukua paja lililokuwa limeinuliwa katika dhabihu na kile kilichokuwa pamoja nalo, akaitenga mbele ya Sauli. Kisha Samweli akasema, “Angalia kile kilichokuwa kimetunzwa kwa ajili yako! Kula, kwa sababu kilitunzwa hadi wakati maalum ufike kwa ajili yako. Na kwa sasa waweza kusema, 'Nimewaalika watu.”' Kwa hiyo Sauli alikula pamoja na Samweli siku hiyo.
And the cooke tooke vp the shoulder, and that which was vpon it, and set it before Saul. And Samuel said, Beholde, that which is left, set it before thee and eate: for hitherto hath it bene kept for thee, saying, Also I haue called the people. So Saul did eate with Samuel that day.
25 Walipokuwa wamekwisha shuka chini kutoka sehemu ya juu na kuingia mjini, Samweli akazungumza na Sauli darini.
And when they were come downe from the hie place into the citie, he communed with Saul vpon the top of the house.
26 Na kulipopambazuka, Samweli alimwita Sauli darini na kusema, “Amka, kusudi nikusindikize uende zako,” Hivyo Sauli aliamka, na wote wawili, yeye na Samweli walitoka kwenda mtaani.
And when they arose early about ye spring of the day, Samuel called Saul to the top of the house, saying, Vp, that I may send thee away. And Saul arose, and they went out, both he, and Samuel.
27 Walipokuwa wakienda nje ya viunga vya mji, Samweli akamwambia Sauli, “Mwambie mtumishi wako atanguliye mbele yetu(na alitangulia mbele), Lakini wewe sharti usubiri kidogo, nipate kukuambia ujumbe wa Mungu.”
And when they were come downe to the ende of the citie, Samuel said to Saul, Bid the seruant goe before vs, (and he went) but stand thou still nowe, that I may shewe thee the worde of God.

< 1 Samweli 9 >