< 1 Samweli 7 >

1 Watu wa Kiriath Yearimu walikuja, wakalichukua sanduku la BWANA, wakalileta ndani ya nyumba ya Abinadabu mlimani iliyokuwa kilimani. Wakamteua Eleazari, mwanawe, kulitunza sanduku la BWANA.
And the men of Kirjath-Jearim come and bring up the Ark of YHWH, and bring it into the house of Abinadab, in the height, and they have sanctified his son Eleazar to keep the Ark of YHWH.
2 Tangu siku ambayo sanduku lilikaa huko Kiiriath Yearimu, ulipita muda mrefu, miaka ishirini. Nyumba yote ya Israeli iliomboleza na ikaazimu kumrudia BWANA.
And it comes to pass, from the day of the dwelling of the Ark in Kirjath-Jearim, that the days are multiplied—indeed, they are twenty years—and all the house of Israel wails after YHWH.
3 Samweli akawaambia watu wote wa Israeli, “Kama mtamrudia BWANA kwa moyo wenu wote, mkaiondoa miungu migeni na Ashtorethi kutoka katikati yenu, igeuzeni mioyo yenu kwa BWANA, na mwabuduni yeye peke yake, ndipo atawaokoa kutoka mkono wa Wafilisti.”
And Samuel speaks to all the house of Israel, saying, “If you are turning back to YHWH with all your heart—turn aside the gods of the stranger from your midst, and Ashtaroth; and prepare your heart for YHWH, and serve Him only, and He delivers you out of the hand of the Philistines.”
4 Ndipo watu wa Israeli wakamuondoa Baali na Ashtorethi, na wakamwabudu BWANA peke yake.
And the sons of Israel turn aside the Ba‘alim and Ashtaroth, and serve YHWH alone;
5 Ndipo Samweli akasema, “Waleteni Israeli wote hadi Mizpa, nami nitamwomba BWANA kwa ajili yenu.”
and Samuel says, “Gather all Israel to Mizpeh, and I pray to YHWH for you.”
6 Wakakusanyika Mispa, wakateka maji na kuyamwaga chini mbele za BWANA. Siku hiyo walifunga na kusema, “Tumemfanyia BWANA dhambi.” Hapo Mispa ndipo Samweli aliwaamu na kuwaongoza watu wa Iraeli. -8
And they are gathered to Mizpeh, and draw water, and pour out before YHWH, and fast on that day, and say there, “We have sinned against YHWH”; and Samuel judges the sons of Israel in Mizpeh.
7 Basi Wafilisti waliposikiakwamba Waisraeli wamekusanyika hapo Mispa, viongozi wa Wafilisti waliwashambulia Israeli. Waisraeli waliposikia hivyo, waliwaogopa Wafilisti.
And the Philistines hear that the sons of Israel have gathered themselves to Mizpeh; and the princes of the Philistines go up against Israel, and the sons of Israel hear, and are afraid of the presence of the Philistines.
8 Ndipo Waisraeli wakamwambia Samweli, “Usiache kumwomba BWANA Mungu wetu kwa ajili yetu, ili atuokoe kutoka mkono wa Wafilisti.”
And the sons of Israel say to Samuel, “Do not keep silent for us from crying to our God YHWH, and He saves us out of the hand of the Philistines.”
9 Samweli alimchukua kondoo mchanga nakumtoa sadaka ya kuteketezwa kikamilifu kwa BWANA. Ndipo Samweli akamlilia BWANA kwa ajili ya Israeli, na BWANA akamjibu.
And Samuel takes a fat lamb, and causes it to go up—a whole burnt-offering to YHWH; and Samuel cries to YHWH for Israel, and YHWH answers him;
10 Hata Samweli alipokuwa akitoa sadaka ya kuteketezwa, Wafilisti wakasogea karibu kuwashambulia Israeli; lakini BWANA alipiga kwa nguromo ya sauti kubwa siku hiyo dhidi ya Wafilisti na kuwatia kiwewe, na wakashindwa mbele ya Israeli.
and Samuel is causing the burnt-offering to go up—and the Philistines have drawn near to battle against Israel—and YHWH thunders with a great noise, on that day, on the Philistines, and troubles them, and they are struck before Israel.
11 Waisraeli wakaondoka Mispa, wakawafuatia Wafilisti na kuwaua hadi kufika chini ya Beth kari.
And the men of Israel go out from Mizpeh, and pursue the Philistines, and strike them to the place of Beth-Car.
12 KIsha Samweli akachukua jiwe akalisimamisha kati ya Mispa na Sheni. Akaliita hilo jiwe Ebeneza, akisema, “Hata sasa BWANA ametusaidia.”
And Samuel takes a stone, and sets [it] between Mizpeh and Shen, and calls its name Eben-Ezer, saying, “Until now YHWH has helped us.”
13 Kwa hiyo, Wafilisti walishindwa na hawakuingia katika mipaka ya Israeli. Mkono wa BWANA uliwalemea Wafilisti siku zote za Samweli.
And the Philistines are humbled, and have not added anymore to come into the border of Israel, and the hand of YHWH is on the Philistines all the days of Samuel.
14 Miji ambayo Wafilisti waliitwaa kutoka kwa Israeli ilirudishwa, kutokea Ekroni hadi Gathi; Israeli ikarudisha tena sehemu za nchi zake kutoka kwa Wafilisti. Ndipo ikawa amani kati ya Israeli na Waamori.
And the cities which the Philistines have taken from Israel are restored to Israel—from Ekron even to Gath—and Israel has delivered their border out of the hand of the Philistines; and there is peace between Israel and the Amorite.
15 Samweli akawa mwamuzi wa Israeli siku zote za maisha yake.
And Samuel judges Israel all the days of his life,
16 Kila mwaka alienda Betheli kwa kuzunguka, akienda Gilgali, na huko Mispa.
and he has gone from year to year, and gone around Beth-El, and Gilgal, and Mizpeh, and judged Israel [in] all these places;
17 Kisha angerudi Rama, kwa sababu mji wake ulikuwa huko; na huko pia aliwaamua Waisiraeli. Hata huko Rama, pia alimjengea BWANA madhabahu.
and his returning [is] to Ramath, for his house [is] there, and he has judged Israel there, and he builds an altar to YHWH there.

< 1 Samweli 7 >