< 1 Samweli 7 >
1 Watu wa Kiriath Yearimu walikuja, wakalichukua sanduku la BWANA, wakalileta ndani ya nyumba ya Abinadabu mlimani iliyokuwa kilimani. Wakamteua Eleazari, mwanawe, kulitunza sanduku la BWANA.
So the people of Kiriath-jearim came and took the Ark of the Lord. They put it in Abinadab's house on the hill. They dedicated his son Eleazar to take care of the Ark of the Lord.
2 Tangu siku ambayo sanduku lilikaa huko Kiiriath Yearimu, ulipita muda mrefu, miaka ishirini. Nyumba yote ya Israeli iliomboleza na ikaazimu kumrudia BWANA.
The Ark remained there in Kiriath-jearim from that day for a long time, in fact for twenty years. Everyone in Israel mourned and in repentance came back to the Lord.
3 Samweli akawaambia watu wote wa Israeli, “Kama mtamrudia BWANA kwa moyo wenu wote, mkaiondoa miungu migeni na Ashtorethi kutoka katikati yenu, igeuzeni mioyo yenu kwa BWANA, na mwabuduni yeye peke yake, ndipo atawaokoa kutoka mkono wa Wafilisti.”
Then Samuel said to all of Israel, “If you sincerely wish to come back to the Lord, then get rid of the foreign gods and the Ashtoreth images you have, and commit yourselves to the Lord and only worship him, and he will save you from the Philistines.”
4 Ndipo watu wa Israeli wakamuondoa Baali na Ashtorethi, na wakamwabudu BWANA peke yake.
The people of Israel got rid of their Baals and Ashtoreth images and worshiped only the Lord.
5 Ndipo Samweli akasema, “Waleteni Israeli wote hadi Mizpa, nami nitamwomba BWANA kwa ajili yenu.”
Then Samuel said, “Have all the people of Israel gather at Mizpah, and I will pray to the Lord for you.”
6 Wakakusanyika Mispa, wakateka maji na kuyamwaga chini mbele za BWANA. Siku hiyo walifunga na kusema, “Tumemfanyia BWANA dhambi.” Hapo Mispa ndipo Samweli aliwaamu na kuwaongoza watu wa Iraeli. -8
Once they had gathered at Mizpah, they drew water and poured it out before the Lord. They fasted that day, and admitted, “We have sinned against the Lord.” Samuel became the leader of the Israelites at Mizpah.
7 Basi Wafilisti waliposikiakwamba Waisraeli wamekusanyika hapo Mispa, viongozi wa Wafilisti waliwashambulia Israeli. Waisraeli waliposikia hivyo, waliwaogopa Wafilisti.
When the Philistines found out that the Israelites had gathered at Mizpah, their rulers led an attack on Israel. When the Israelites heard about this, they were terrified at what the Philistines might do.
8 Ndipo Waisraeli wakamwambia Samweli, “Usiache kumwomba BWANA Mungu wetu kwa ajili yetu, ili atuokoe kutoka mkono wa Wafilisti.”
They told Samuel, “Don't stop pleading with the Lord our God for us so he can save us from the Philistines.”
9 Samweli alimchukua kondoo mchanga nakumtoa sadaka ya kuteketezwa kikamilifu kwa BWANA. Ndipo Samweli akamlilia BWANA kwa ajili ya Israeli, na BWANA akamjibu.
Samuel took a young lamb and presented it as a whole burnt offering to the Lord. He cried out for help to the Lord for Israel, and the Lord responded.
10 Hata Samweli alipokuwa akitoa sadaka ya kuteketezwa, Wafilisti wakasogea karibu kuwashambulia Israeli; lakini BWANA alipiga kwa nguromo ya sauti kubwa siku hiyo dhidi ya Wafilisti na kuwatia kiwewe, na wakashindwa mbele ya Israeli.
While Samuel was presenting the burnt offering, the Philistines approached to attack Israel. But the Lord thundered extremely loudly against the Philistines that day, which totally confused them, and they were defeated as Israel watched.
11 Waisraeli wakaondoka Mispa, wakawafuatia Wafilisti na kuwaua hadi kufika chini ya Beth kari.
Then the men of Israel ran out from Mizpah and chased them, killing them all the way to a place near Beth-car.
12 KIsha Samweli akachukua jiwe akalisimamisha kati ya Mispa na Sheni. Akaliita hilo jiwe Ebeneza, akisema, “Hata sasa BWANA ametusaidia.”
After this Samuel took a stone and placed it between Mizpah and Shen. He called it Ebenezer, saying, “The Lord helped us right up to here!”
13 Kwa hiyo, Wafilisti walishindwa na hawakuingia katika mipaka ya Israeli. Mkono wa BWANA uliwalemea Wafilisti siku zote za Samweli.
In this way the Philistines were kept under control and did not invade Israel again. During Samuel's lifetime the Lord used his power against the Philistines.
14 Miji ambayo Wafilisti waliitwaa kutoka kwa Israeli ilirudishwa, kutokea Ekroni hadi Gathi; Israeli ikarudisha tena sehemu za nchi zake kutoka kwa Wafilisti. Ndipo ikawa amani kati ya Israeli na Waamori.
The towns the Philistines had taken from Israel were restored to Israel, all the way from Ekron to Gath, and Israel also liberated the neighboring territory from the hands of the Philistines. There was also peace between Israel and the Amorites.
15 Samweli akawa mwamuzi wa Israeli siku zote za maisha yake.
Samuel was Israel's leader for the rest of his life.
16 Kila mwaka alienda Betheli kwa kuzunguka, akienda Gilgali, na huko Mispa.
Every year he went around, going to Bethel, Gilgal, and Mizpah. At all these places he ruled Israel.
17 Kisha angerudi Rama, kwa sababu mji wake ulikuwa huko; na huko pia aliwaamua Waisiraeli. Hata huko Rama, pia alimjengea BWANA madhabahu.
Then he would return to Ramah because that was where he lived. He ruled Israel from there, and also built an altar to the Lord.