< 1 Samweli 6 >
1 Basi sanduku la BWANA lilikaa katika nchi ya Wafilisti kwa miezi saba.
I arka PANA przebywała w ziemi Filistynów przez siedem miesięcy.
2 Ndipo Wafilisti wakawaita makuhani na waganga; wakawaambia, “Tulifanyie nini sanduku la BWANA? Twambieni jinsi ambavyo tunapaswa kulirudisha sanduku katika nchi yake.”
Wtedy Filistyni zwołali kapłanów i wróżbitów i zapytali: Co mamy zrobić z arką PANA? Powiedzcie nam, jak mamy ją odesłać na swoje miejsce?
3 Makuhani na waganga wakasema, “Kama mtalirudisha sanduku la Mungu wa Israeli, msilipeleke bila zawadi; kwa namna yoyote ile mpelekeeni sadakaa ya hatia. Hapo ndipo mtapona, na mtajua ni kwanini mkono wake hadi sasa haujaondoka juu yenu.”
Ci odpowiedzieli: Jeśli odsyłacie arkę Boga Izraela, nie odsyłajcie jej z niczym, lecz koniecznie oddajcie mu ofiarę za grzech: wtedy będziecie uzdrowieni i dowiecie się, czemu jego ręka nie odstąpiła od was.
4 Ndipo wakawauliza, “Sadaka ya hatia itakuwa nini kwamba tunampelekea?” Wakawajibu, “Majipu matano ya dhahabu na panya watano wa dhahabu, Idadi hiyo ya watano ni sawa na idadi ya viongozi wa Wafilisti. Kwa sababu tauni ya aina moja iliwashambulia ninyi na viongozi wenu.
I powiedzieli: Jaką ofiarę za grzech mamy mu złożyć? Odpowiedzieli: Według liczby książąt filistyńskich pięć wrzodów złotych i pięć myszy złotych. Ta sama bowiem plaga dotknęła was wszystkich i waszych książąt.
5 Kwa hiyo, nilazima mtengeneze mifano ya majipu yenu, na mifano ya panya wenu ambayo huiharibu nchi, na mpeni utukufu Mungu wa Israeli. Labda ataondoa mkono wake kutoka juu yenu, kutoka juu ya miungu yenu, na kutoka juu ya nchi yenu.
I sporządzicie podobizny waszych wrzodów i podobizny waszych myszy, które niszczą ziemię, i oddacie chwałę Bogu Izraela. Może odejmie swoją rękę od was, waszych bogów i waszej ziemi.
6 Kwanini mfanye mioyo yenu kwa migumu, kama vile Wamisri na Farao walifanya mioyo yao kuwa migumu? Hicho ni kipindi ambacho Mungu wa Israeli aliwashughilikia sana; Je, Wamisri hawakuwaachilia watu, na wakaondoka?
Dlaczego zatwardzacie swoje serca tak, jak Egipcjanie i faraon zatwardzali swoje serca? Czy [nie dopiero] wtedy, gdy czynił wśród nich cudowne rzeczy, wypuścili ich, aby wyszli?
7 Basi sasa, andaeni mkokoteni mpya pamoja na ng'ombe wawili wake wanaonyonyesha, ambao hawajawahi kufungwa nira. Wafungeni ng'ombe hao kwenye mkokoteni, lakini warudisheni wale ndama wao nyumbani.
Teraz więc przygotujcie nowy wóz, weźcie dwie mleczne krowy, na które nie nałożono jarzma, i zaprzęgnijcie te krowy do wozu, a ich cielęta odprowadźcie od nich do domu.
8 Kisha lichukueni sanduku la BWANA na kuliweka ndani ya mkokoteni. Wekeni ndani ya kasha yale maumbo ya dhahabu mnayompelekea ambyo ni sadaka ya hatia kando yake. Ndipo mlipeleke lipate kuondoka.
Weźcie też arkę PANA i włóżcie ją na wóz; a złote przedmioty, które oddajecie jako ofiarę za grzech, włóżcie do skrzynki obok niej. Po czym puśćcie go i niech jedzie.
9 Kisha muwe makini; kama litapanda kwenda kwa njia hadi nchini mwake hadi Beth Shemeshi, basi mjue kuwa BWANA ndiye aliyetenda pigo hili kubwa. Lakini kama halitakwenda, ndipo tutajua kwamba siyo mkono wake uliotupatia mateso; badala yake tutajua kuwa yaliyotupata ilikuwa ni kwa bahati mbaya tu.
Wtedy patrzcie – jeśli pojedzie drogą własnej granicy do Bet-Szemesz, [to PAN] wyrządził nam to wielkie zło. Lecz jeśli nie, to będziemy wiedzieli, że to nie jego ręka nas dotknęła, [ale] to, co nas spotkało, było przypadkiem.
10 Watu hao wakafanya kama walivyoambiwa, walichukuwa ng'ombe wawili wanaonyonyesha, wakawafunga kwenye mkokoteni, na kuwabakiza ndama wao nyumbani.
I ci ludzie tak uczynili: wzięli dwie mleczne krowy i zaprzęgli je do wozu, a ich cielęta zamknęli w domu.
11 Wakaliweka sanduku la BWANA juu ya mkokoteni, pamoja na lile kasha lililobeba panya wa dhahabu na yale maumbo ya majipu yao.
Potem włożyli arkę PANA na wóz oraz skrzynkę ze złotymi myszami i z podobiznami swoich wrzodów.
12 Hao ng'ombe waliondoka moja kwa moja kuelekea Beth Shemeshi. Walikwenda kwa kuifuata nija moja kuu, wakiteremka walipokuwa wakienda, na hwakugeuka upande wa kushoto au kulia. Viongozi wa Wafilisti walifuata kwa nyuma hadi mpaka wa Beth Shemeshi.
I krowy poszły prostą drogą ku Bet-Szemesz. Szły jednym gościńcem, a idąc, ryczały i nie zbaczały ani w prawo, ani w lewo. A książęta filistyńscy szli za nimi aż do granicy Bet-Szemesz.
13 Nao watu wa Beth Shemeshi walikuwa wakivuna ngano yao katika bonde. Waliponyanyua macho yao juu na kuliona sanduku, wakafurahi.
W tym czasie mieszkańcy Bet-Szemesz żęli pszenicę w dolinie, a gdy podnieśli swe oczy, zobaczyli arkę i uradowali się na jej widok.
14 Huo mkokoteni ulifikia ndani ya shamba la Yoshua wa Beth Shemeshi na ukasimama hapo. Kulikuapo jiwe kubwa mahali hapo, wakatayarisha kuni kutokana na mkokoteni huo, na wakawatoa ng'ombe hao kama sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya BWANA.
Wóz zaś dotarł na pole Jozuego z Bet-Szemesz i tam się zatrzymał, tam też był wielki kamień. Wtedy porąbali drewno [z tego] wozu i złożyli PANU krowy na ofiarę całopalną.
15 Walawi walilitelemsha sanduku la BWANA chini pamoja na kasha lake lililoyatunza yale maumbo ya dhahabu, wakaweka vitu hivyo juu ya hilo jiwe kubwa. Watu wa Beth Shemeshi walitoa sadaka za kuteketezwa na kutoa dhabihu kwa BWANA siku iyo hiyo.
Lewici zdjęli arkę PANA oraz skrzynkę obok niej, w której [były] złote przedmioty, i postawili to na tym wielkim kamieniu. Ludzie zaś z Bet-Szemesz w tym dniu złożyli PANU całopalenia i ofiary.
16 Hao viongozi watano wa Wafilisti walipoona hayo, walirejea Ekroni siku iyo hiyo.
Gdy pięciu książąt filistyńskich zobaczyło to [wszystko], tego samego dnia powrócili do Ekronu.
17 Haya ndiyo majipu ya dhahabu ambayo Wafilisti walirudisha kama sadaka ya hatia kwa BWANA: moja kwa ajili ya Ashdodi, moja kwa Gaza, moja kwa Ashkeloni, moja kwa Gathi, na moja kwa Ekroni.
A oto złote wrzody, które Filistyni oddali PANU jako ofiarę za grzech: za Aszdod – jeden, za Gazę – jeden, za Aszkelon – jeden, za Gat – jeden i za Ekron – jeden.
18 Idadi ya wale panya wa dhahabu ilikuwa sawa na ile ya idadi ya miji yote ya Wafilisti inayomilikiwa na viongozi watano, kwa miji iliyojengewa maboma na vijiji vya mashambani. Lile jiwe kubwa, ambalo kando yake waliweka sanduku la BWANA, lipo kama ushuhuda hadi leo katika shamba la Yoshua Mbeth- Shemeshi.
Dodatkowo złote myszy według liczby wszystkich miast filistyńskich [należących] do pięciu książąt, [zarówno] warownych miast, jak i wiosek bez muru, i aż do [tego] wielkiego kamienia, na którym postawili arkę PANA. [Znajduje się] aż do dziś na polu Jozuego z Bet-Szemesz.
19 BWANA akawashambulia baadhi ya watu wa Bethi Shemeshi kwa sababu walichungulia ndani ya sanduku lake. Aliwaua watu sabini. Watu wakaomboleza, kwa sababu BWANA aliwapa watu pigo kubwa mno.
Lecz PAN wytracił spośród ludzi z Bet-Szemesz, ponieważ zaglądali do arki PANA, zabił z ludu pięćdziesiąt tysięcy siedemdziesiąt osób. I lud [ich] opłakiwał, ponieważ PAN zadał ludowi wielką klęskę.
20 Watu wa Bethi Shemeshi wakasema, “Ni nani mwenye uwezo wa kushindana na BWANA, huyu Mungu mtakatifu? Na atampandia nani akitoka kwetu.”” Je, ni nani awezaye kusimama mbele ya BWANA, huyu Mungu mtakatifu? Na ni kwa nani ambako sanduku litaenda likitoka hapa.”
Ludzie z Bet-Szemesz mówili: Któż zdoła ostać się przed tym świętym PANEM Bogiem? I do kogo on pójdzie od nas?
21 Wakawatuma wajumbe kwenda kwa wenyeji wa Kiriath Yearimu, wakisema, “Wafilisti wamelirudisha sanduku la BWANA; teremkeni na mkalipeleke kwenu.”
Wyprawili więc posłańców do mieszkańców Kiriat-Jearim z wiadomością: Filistyni zwrócili arkę PANA. Przyjdźcie i zabierzcie ją do siebie.